Synthesizer
JF-Expert Member
- Feb 15, 2010
- 11,143
- 18,774
Imefikia mahali ambapo Mtanzania yeyote mwenye akili ataona kwamba serikali ya awamu ya tano imekithiri kwa kutumia uongo katika mambo ya kila siku yanayohusu uongozi wa nchi. Wananchi wanadanganywa hadi watu weye akili zao wanashikwa na hasira kama sio kichefuchefu!
Mimi naona ni vema basi serikali ilifanye hili suala la kudanganya watu liwe na wizara rasmi - kuwe na Waziri wa Propaganda katika wizara za serikali. Katika enzi za utawala wa Hitler, yeye alikuwa na waziri wa propaganda, Paul Joseph Goebbels, na akafanya kazi nzuri sana.
Kama Hitler alifanikiwa kwa nini serikali hii isifanikiwe? Kwanza watu wa chama tawala ambao wana sifa zote kuwa mawaziri wa Propaganda wapo wengi sana!
Mimi naona ni vema basi serikali ilifanye hili suala la kudanganya watu liwe na wizara rasmi - kuwe na Waziri wa Propaganda katika wizara za serikali. Katika enzi za utawala wa Hitler, yeye alikuwa na waziri wa propaganda, Paul Joseph Goebbels, na akafanya kazi nzuri sana.
Kama Hitler alifanikiwa kwa nini serikali hii isifanikiwe? Kwanza watu wa chama tawala ambao wana sifa zote kuwa mawaziri wa Propaganda wapo wengi sana!