Serikali: Sanamu ya Nyerere imemlenga Nyerere wa miaka ya 60-80, imefanana naye kwa 92%. Serikali imeridhika yule ni Nyerere

Precious Diamond

JF-Expert Member
Jun 9, 2023
397
993
nyerere.jpg

Balozi Said Shaibu Mussa, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akijibu swali kuhusu sintofahamu ya sanamu la Mwl. Nyerere amesema;

Kwenye sintofahamu hiyo kuna waokubali kuwa sanamu lile linafafa na Nyeyrere na wengine wanaokataa.

Akisema kuwa Serikali imefuata maelezo ya kitaalamu yaliyotolewa na kamati maalum ya wataalamu ambayo ilishirikia kuanzia kwenye mjadala mpaka kupatikana kwa sanamu hiyo na, sanamu hiyo imefadhiliwa na SADC, lengo likiwa kutambua mchango wa Nyerere katika Ukombozi wa Bara la Afrika hususan Kusini mwa Afrika.

Kamati hiyo ilihusisha watu mbalimbali ikiwemo; familia ya Nyerere akiwemo Madaraka Nyerere, wizara ya mambo ya nje, wizara ya utamaduni sanaa na michezo, Wataalamu kutoka UDSM, pamoja na watu wengine.

Kuanzia hatua ya awali mpaka sananu linakamilika Kamati ililidhika.

Vigezo vilivyotumika kupatikana sanamu ile ni:

1. Kumlenga Nyerere wa miaka 60 na miaka 80, wakati Nyerere akiwa 'active' katika mapambano ya kusaidia kupatikana kwa uhuru na maendeleo katika nchi za Kusini mwa Afrika.

2. Kaiuli ya mtoto wa Nyerere, Madaraka Nyerere mara kadhaa na siku ya uzinduzi ameongea kwa kusisitiza kwamba yule ni baba yake, kama kuna mtu anabisha amuulize yeye.

3. Taratibu za kitaalamu zinasema unapotengeneza sanamu unatakiwa uipatie angalau kufikia 75%, lakini sanamu la Nyerere Addis Ababa kwa matokeo yake ni 92%, na Waziri wa Utamaduni na Michezo alitoa ufafanuzi wa kina juu ya hili.

Hivyo mapokeo ya wizara ya Utamaduni ndio mapokeo ya Serikali, ile ni sanamu ya Nyerere
 
Picha zake za. Miaka 60 zipo Wala hafanani nazo si ajabu hiyo tenda. Walipeana wanaona aibu.
Mradi ulitekelezwa na Kampuni ya SAMCRO ya nchini Afrika Kusini chini ya usimamizi wa SADC na Tanzania na uĺigharimu takriban Dola za Marekani 267,992.60 ambazo ni sawa na takriban Shilingi 615,000,000 ambazo zilitolewa na SADC na gharama za usimamizi kutolewa na Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.
 

Balozi Said Shaibu Mussa, Naibu Katibu Mkuu Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki akijibu swali kuhusu sintofahamu ya sanamu la Mwl. Nyerere amesema;

Kwenye sintofahamu hiyo kuna waokubali kuwa sanamu lile linafafa na Nyeyrere na wengine wanaokataa.

Akisema kuwa Serikali imefuata maelezo ya kitaalamu yaliyotolewa na kamati maalum ya wataalamu ambayo ilishirikia kuanzia kwenye mjadala mpaka kupatikana kwa sanamu hiyo na, sanamu hiyo imefadhiliwa na SADC, lengo likiwa kutambua mchango wa Nyerere katika Ukombozi wa Bara la Afrika hususan Kusini mwa Afrika.

Kamati hiyo ilihusisha watu mbalimbali ikiwemo; familia ya Nyerere akiwemo Madaraka Nyerere, wizara ya mambo ya nje, wizara ya utamaduni sanaa na michezo, Wataalamu kutoka UDSM, pamoja na watu wengine.

Kuanzia hatua ya awali mpaka sananu linakamilika Kamati ililidhika.

Vigezo vilivyotumika kupatikana sanamu ile ni:

1. Kumlenga Nyerere wa miaka 60 na miaka 80, wakati Nyerere akiwa 'active' katika mapambano ya kusaidia kupatikana kwa uhuru na maendeleo katika nchi za Kusini mwa Afrika.

2. Kaiuli ya mtoto wa Nyerere, Madaraka Nyerere mara kadhaa na siku ya uzinduzi ameongea kwa kusisitiza kwamba yule ni baba yake, kama kuna mtu anabisha amuulize yeye.

3. Taratibu za kitaalamu zinasema unapotengeneza sanamu unatakiwa uipatie angalau kufikia 75%, lakini sanamu la Nyerere Addis Ababa kwa matokeo yake ni 92%, na Waziri wa Utamaduni na Michezo alitoa ufafanuzi wa kina juu ya hili.

Hivyo mapokeo ya wizara ya Utamaduni ndio mapokeo ya Serikali, ile ni sanamu ya Nyerere
Huku ni kuchanganyikiwa..hahahaha..ina maana wao peke yao ndio wanaijua sura ya Julius Nyerere wa miaka hiyo....
Kama ingekuwa hiyo 92% watu wangekosa hoja.
Heshima aliyopewa Baba wa Taifa ni kubwa sana...kiukweli kwa sura ile hatujamtendea haki yeye na Taifa kwa ujumla
Mambo ya aibu sana haya .....dunia nzima inatucheka
 
Teknolojia imekua sana kwa sasa, kuna app za kutambua sura ya mtu, yaani unacheza tu na keyboard na unapata majibu.

Nina mashaka na akili za hao wanaokaza fuvu kuwa hilo sanamu ni la Nyerere kwa uthibitisho wa Madaraka Nyerere 😂😂

Hivi kweli wameshindwa hata kuingia huko store kupata uthibitisho kama hilo lisanamu lina sura halisi ya Nyerere, na badala yake wakamchukua Madaraka Nyerere awathibitishie?

Hivi hawajui kuwa Madaraka ni msela fulani tu wa enzi na enzi?

Kweli hatuna viongozi.
 
Back
Top Bottom