Viongozi wa sasa ni zao la uovu, wasipewe uongozi kwa Miaka 10

Bams

JF-Expert Member
Oct 19, 2010
16,547
41,059
Tanzania haiendelei na haiwezi kuendelea kwa sababu waovu waliostahili adhabu, ndiyo viongozi wa kuwasimamia watu wema na kuwaonesha njia kuhusiana na maisha yao ya kila siki. Ukimpa nafasi mtu mwovu akuongoze, unatarajia atakuongoza kupeleka wapi?

Hivi karibuni, viongozi mbalimbali wa CCM na Serikali wamekuwa wakikiri kuwa wao na wabunge ni zao la uovu.

Ni watu ambao hawakuchaguliwa na umma kwa sababu uchaguzi wa mwaka 2019 na 2020 haukuwa uchaguzi huru wala wa haki. Lakini pia mahakama kuu ilitoa hukumu inayosema kuwa wabunge wote waliotangazwa kuwa walipita bila kupingwa, akiwemo na Waziri Mkuu Majaliwa, ni wabunge batili. Cha ajabu, bila aibu watu hawa bado wameng'ang'ania madaraka.

Ukweli ni kwamba, kila mmoja anajua kuwa uchaguzi wa 2020 ulizidi katika kiwango cha uovu. Lakini tunajua kuwa hata kabla ya 2020, Tanzania haijawahi kuwa na uchaguzi huru na wa haki chini ya CCM.

Wote waliopo bungeni kuanzia PM, mawaziri mpaka wabunge ni mazao ya uovu. Rais yupo kwenye nafasi hiyo siyo kwa kuchaguliwa bali kwa mujibu wa katiba iliyokanyagwa kwa kiwango cha ajabu mwaka 2020.

Tena kwa kauli yake mpaka alifikia kutoa kauli ya kuwabeza wapiga kura pale aliposema kuwa hata kama wananchi wakiwapigia kura vyama vingine, zitahesabika kwa CCM.

Kwa kuwa wote, wakiwemo viongozi wa CCM, Serikali, vyama vya upinzani na wananchi mmoja mmoja, tunakiri kuwa Waziri Mkuu, mawaziri, wabunge na madiwani, ni mazao na ni washirika wa uovu, kwa nini tusingekubaliana kuwa kwa sababu watu hawa ni zao la uovu na ni washiriki wa uovu, basi nao wanastahili kuadhibiwa, ili kujenga mfumo wa kuwawajibisha watu wanaodharau na kupora mamlaka ya umma katika kuwachagua watu wanaotaka wawaongoze.

PENDEKEZO:
Waziri Mkuu, Mawaziri, Wabunge, Madiwani, Wenyeviti wa Serikali za Mitaa na vijiji aa sasa, kwa kushiriki uovu na kuwa zao la uovu mwaka 2020, wasiruhusiwe kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya miaka 10 kuanzia 2025.
 
Hivi karibuni, viongozi mbalimbali wa CCM na Serikali wamekuwa wakikiri kuwa wao na wabunge ni zao la uovu.
Hao wote waliokiri, wawajibike.

Sheria iwe msumeno, yaani wajiuzulu, watoe ushirikiano polisi na uchunguzi, ufanyike mamlaka na vyombo vya Usalama viwafikishe Mahakamani.

Zaidi ya hapo, waache maigizo kuelekea Uchaguzi 2024-2025

Wengine wote Nendeni mahakamani.

Awe ni Waziri-ajiuzulu
Awe ni mwanasiasa- ajiuzulu
Awe ni kiongozi wa Taasisi-ajiuzulu.

Haiwezekani kabisa kwamba hawa wote walikuwa ni mazuzu. (Sasa naanza kusikia sauti ya Jenerali Ulimwengu) Haiwezekani.

Na kama ndivyo hivyo, basi hii itakuwa ndio live cinema ambayo imeshawahi kulitokea Taifa lelote ile Duniani-hata yale ya Hollywood, Nollywood, Bollywood combined, hakuna mfano wake.

Wapewe tuzo zote. Wapewe maua yao.

Aisee.
 
PENDEKEZO:
Waziri Mkuu, Mawaziri, Wabunge, Madiwani, Wenyeviti wa Serikali za Mitaa na vijiji aa sasa, kwa kushiriki uovu na kuwa zao la uovu mwaka 2020, wasiruhusiwe kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya miaka 10 kuanzia 2025.
Hili pendekezo ni la kinafiki.
 
Mtoa hoja ana mantiki sana. Najua hata yeye anajua kuwa utekelezaji wa pendekezo lake ni ngumu kutekelezwa. Lakini ujumbe wake umefika vizuri kwa watu wanaojielewa.

Shida ni kuwa bado watu wengi sana hawajielewi. Kiongozu mkubwa kabisa anathubutu kusema hata hizo kura mpigie upinzani, zitahesabiwa CCM.

Halafu inaonekana ni sawa kabisa na uchaguzi unaendelea.

Hatari sana.
 
Mtoa hoja ana mantiki sana. Najua hata yeye anajua kuwa utekelezaji wa pendekezo lake ni ngumu kutekelezwa. Lakini ujumbe wake umefika vizuri kwa watu wanaojielewa.

Shida ni kuwa bado watu wengi sana hawajielewi. Kiongozu mkubwa kabisa anathubutu kusema hata hizo kura mpigie upinzani, zitahesabiwa CCM.

Halafu inaonekana ni sawa kabisa na uchaguzi unaendelea.

Hatari sana.

Wananchi tungekuwa na umoja, halafu tukawa na uzalendo wa kweli kwa Taifa letu, hata kama hawa wahalifu wangeamua kupuuza pendekezo la wao kutoruhusiwa kugombea nafasi za uongozi, wananchi tungehasishana na kuelezana na kukubakiana kuwa yeyote aliyekuwa kwenye uongozi awamu ya 5 na ya 6, ambaye alistahili kuchaguliwa na wananchi lakini alipora maamuzi ya wananchi, hafai kuchaguliwa. Kwa baadhi ya mataifa jili lingewezekana kabisa.
 
Hivi tunataka tuongozwe kwenda wapi ? Tatizo ni Viongozi pekee au kukosekana kwa Dira Pia ?

Kwahio kama tunaelekea nyuma hata kiongozi mzuri atatupeleka nyuma; Kwanda tufahamu na kujua njia sahihi ya kwenda, Hata tukipewa Robot tutafikishana pamoja huko tunapotaka kuelekea...; Zaidi ya hivyo ni mwendo wa kubadilisha chupa wakati mvinyo ni uleule....
 
Tanzania haiendelei na haiwezi kuendelea kwa sababu waovu waliostahili adhabu, ndiyo viongozi wa kuwasimamia watu wema na kuwaonesha njia kuhusiana na maisha yao ya kila siki. Ukimpa nafasi mtu mwovu akuongoze, unatarajia atakuongoza kupeleka wapi?

Hivi karibuni, viongozi mbalimbali wa CCM na Serikali wamekuwa wakikiri kuwa wao na wabunge ni zao la uovu.

Ni watu ambao hawakuchaguliwa na umma kwa sababu uchaguzi wa mwaka 2019 na 2020 haukuwa uchaguzi huru wala wa haki. Lakini pia mahakama kuu ilitoa hukumu inayosema kuwa wabunge wote waliotangazwa kuwa walipita bila kupingwa, akiwemo na Waziri Mkuu Majaliwa, ni wabunge batili. Cha ajabu, bila aibu watu hawa bado wameng'ang'ania madaraka.

Ukweli ni kwamba, kila mmoja anajua kuwa uchaguzi wa 2020 ulizidi katika kiwango cha uovu. Lakini tunajua kuwa hata kabla ya 2020, Tanzania haijawahi kuwa na uchaguzi huru na wa haki chini ya CCM.

Wote waliopo bungeni kuanzia PM, mawaziri mpaka wabunge ni mazao ya uovu. Rais yupo kwenye nafasi hiyo siyo kwa kuchaguliwa bali kwa mujibu wa katiba iliyokanyagwa kwa kiwango cha ajabu mwaka 2020.

Tena kwa kauli yake mpaka alifikia kutoa kauli ya kuwabeza wapiga kura pale aliposema kuwa hata kama wananchi wakiwapigia kura vyama vingine, zitahesabika kwa CCM.

Kwa kuwa wote, wakiwemo viongozi wa CCM, Serikali, vyama vya upinzani na wananchi mmoja mmoja, tunakiri kuwa Waziri Mkuu, mawaziri, wabunge na madiwani, ni mazao na ni washirika wa uovu, kwa nini tusingekubaliana kuwa kwa sababu watu hawa ni zao la uovu na ni washiriki wa uovu, basi nao wanastahili kuadhibiwa, ili kujenga mfumo wa kuwawajibisha watu wanaodharau na kupora mamlaka ya umma katika kuwachagua watu wanaotaka wawaongoze.

PENDEKEZO:
Waziri Mkuu, Mawaziri, Wabunge, Madiwani, Wenyeviti wa Serikali za Mitaa na vijiji aa sasa, kwa kushiriki uovu na kuwa zao la uovu mwaka 2020, wasiruhusiwe kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya miaka 10 kuanzia 2025.
nani sasa wa kuwazuia wasishiriki uchaguzi?
na uthibitisho wa hayo malalamuko yako uko wap🐒

maoni na mtazamo wako juu ya hayo yote usaidie tu kukupa relief moyoni but hakuna mashiko kwenye hoja na maoni yako 🐒
 
nani sasa wa kuwazuia wasishiriki uchaguzi?
na uthibitisho wa hayo malalamuko yako uko wap

maoni na mtazamo wako juu ya hayo yote usaidie tu kukupa relief moyoni but hakuna mashiko kwenye hoja na maoni yako

Umefika mjini leo hata uulize uthibitisho wa niliyoyasema? Hujawahi kumsikia Kinana akizungumzia uchaguzi wa 2020? Hujawahi kumsikia January, Nape, na hata Mh. Rais? Au unaishi mashambani kusiko na network?

Nakushauri, hata kama unaishi porini, ukifika mjini waulize wenzako juu ya yaliyojili wakati ukiwa porini ili usionekane mtu wa ajabu wa kutokutambua hata yaliyo dhahiri kwa kila mtu.
 
Umefika mjini leo hata uulize uthibitisho wa niliyoyasema? Hujawahi kumsikia Kinana akizungumzia uchaguzi wa 2020? Hujawahi kumsikia January, Nape, na hata Mh. Rais? Au unaishi mashambani kusiko na network?

Nakushauri, hata kama unaishi porini, ukifika mjini waulize wenzako juu ya yaliyojili wakati ukiwa porini ili usionekane mtu wa ajabu wa kutokutambua hata yaliyo dhahiri kwa kila mtu.
kwakuwa watu fulani wametoa maoni ma mitazamo yao jua ya jamabo fulani, eti ndio sasa wakuskize wewe unae ona aibu hata kutaja nani awazuie wananchi kushiriki uchaguzi...

kwahiyo,
kwa mtazamo na maoni yako ya kinyonge sana, unaamini kwamba maoni na mitazamo ya ulowataja ndio uelekeo wa nchi right?...

kwanba hao ndio kusema Tanzania....

my friend,
bila kua na mawazo mbadala, mipango mikakati, uelekeo na dira isiyotegemea kauli za watu ambao mnao waamini kua hao ndio nchi kutoboa ni ndroto za mchana kweupe....
 
Tanzania haiendelei na haiwezi kuendelea kwa sababu waovu waliostahili adhabu, ndiyo viongozi wa kuwasimamia watu wema na kuwaonesha njia kuhusiana na maisha yao ya kila siki. Ukimpa nafasi mtu mwovu akuongoze, unatarajia atakuongoza kupeleka wapi?

Hivi karibuni, viongozi mbalimbali wa CCM na Serikali wamekuwa wakikiri kuwa wao na wabunge ni zao la uovu.

Ni watu ambao hawakuchaguliwa na umma kwa sababu uchaguzi wa mwaka 2019 na 2020 haukuwa uchaguzi huru wala wa haki. Lakini pia mahakama kuu ilitoa hukumu inayosema kuwa wabunge wote waliotangazwa kuwa walipita bila kupingwa, akiwemo na Waziri Mkuu Majaliwa, ni wabunge batili. Cha ajabu, bila aibu watu hawa bado wameng'ang'ania madaraka.

Ukweli ni kwamba, kila mmoja anajua kuwa uchaguzi wa 2020 ulizidi katika kiwango cha uovu. Lakini tunajua kuwa hata kabla ya 2020, Tanzania haijawahi kuwa na uchaguzi huru na wa haki chini ya CCM.

Wote waliopo bungeni kuanzia PM, mawaziri mpaka wabunge ni mazao ya uovu. Rais yupo kwenye nafasi hiyo siyo kwa kuchaguliwa bali kwa mujibu wa katiba iliyokanyagwa kwa kiwango cha ajabu mwaka 2020.

Tena kwa kauli yake mpaka alifikia kutoa kauli ya kuwabeza wapiga kura pale aliposema kuwa hata kama wananchi wakiwapigia kura vyama vingine, zitahesabika kwa CCM.

Kwa kuwa wote, wakiwemo viongozi wa CCM, Serikali, vyama vya upinzani na wananchi mmoja mmoja, tunakiri kuwa Waziri Mkuu, mawaziri, wabunge na madiwani, ni mazao na ni washirika wa uovu, kwa nini tusingekubaliana kuwa kwa sababu watu hawa ni zao la uovu na ni washiriki wa uovu, basi nao wanastahili kuadhibiwa, ili kujenga mfumo wa kuwawajibisha watu wanaodharau na kupora mamlaka ya umma katika kuwachagua watu wanaotaka wawaongoze.

PENDEKEZO:
Waziri Mkuu, Mawaziri, Wabunge, Madiwani, Wenyeviti wa Serikali za Mitaa na vijiji aa sasa, kwa kushiriki uovu na kuwa zao la uovu mwaka 2020, wasiruhusiwe kugombea nafasi yoyote ya uongozi ndani ya miaka 10 kuanzia 2025.
Mmewakamia.....hawapumui
 
Hakika. Maana CCM wanachofanya sasa, ni sawa na kusimama mbele ya umma na kuwaambia wananchi kuwa, oneni sisi hamkutuchagua ila kwa ubabe wetu, na kwa vile ninyi ni wajinga, tunawatawala.
Kikwazo cha maendeleo na kutoweka kwa amani kwa nchi hii kwa Sasa ni CCM. Viongozi wanang'ang'ania madaraka si kwasababu wana nia thabiti ya kuwatumikia wananchi bali kugawana madaraka kwa kujuana na kukwapua siyo tu pesa ya walipa kodi bali hata kuuza rasilimali za nchi kifisadi kwa manufaa yao binafsi msingi mkubwa ukiwa ni kulindana. Ni chama ambacho kwa jicho la ndani linatengeneza kamfumo fulani ka kifalme kwa kurithishana madaraka.

Pamoja na rafu ktk chaguzi baada ya mfumo wa vyama vvingi, lakini hii ya 2019/2020 haikuwa rafu bali uhaini. Walifanya mapinduzi ya nguvu kwenye matakwa ya wananchi wa taifa hili. Kama si kulindana, kuanzia Mkurugenzi wa tume ya uchaguzi na maafisa wake wote wa uchaguzi hadi kwenye ngazi za majimbo, kata na vijiji walipaswa kuwa magerezani.

Serikali tuliyonayo haitokani na ridhaa ya wananchi. Ni zao la uhalifu.
 
kwakuwa watu fulani wametoa maoni ma mitazamo yao jua ya jamabo fulani, eti ndio sasa wakuskize wewe unae ona aibu hata kutaja nani awazuie wananchi kushiriki uchaguzi...

kwahiyo,
kwa mtazamo na maoni yako ya kinyonge sana, unaamini kwamba maoni na mitazamo ya ulowataja ndio uelekeo wa nchi right?...

kwanba hao ndio kusema Tanzania....

my friend,
bila kua na mawazo mbadala, mipango mikakati, uelekeo na dira isiyotegemea kauli za watu ambao mnao waamini kua hao ndio nchi kutoboa ni ndroto za mchana kweupe..
Ni sawa na kumpa shoka mbuzi au ng'ombe halafu umwambie ajichinje mwenyewe na utegemee kabisa kuwa atafanya hivyo.

Wishful thinking.
 
Kikwazo cha maendeleo na kutoweka kwa amani kwa nchi hii kwa Sasa ni CCM. Viongozi wanang'ang'ania madaraka si kwasababu wana nia thabiti ya kuwatumikia wananchi bali kugawana madaraka kwa kujuana na kukwapua siyo tu pesa ya walipa kodi bali hata kuuza rasilimali za nchi kifisadi kwa manufaa yao binafsi msingi mkubwa ukiwa ni kulindana. Ni chama ambacho kwa jicho la ndani linatengeneza kamfumo fulani ka kifalme kwa kurithishana madaraka.

Pamoja na rafu ktk chaguzi baada ya mfumo wa vyama vvingi, lakini hii ya 2019/2020 haikuwa rafu bali uhaini. Walifanya mapinduzi ya nguvu kwenye matakwa ya wananchi wa taifa hili. Kama si kulindana, kuanzia Mkurugenzi wa tume ya uchaguzi na maafisa wake wote wa uchaguzi hadi kwenye ngazi za majimbo, kata na vijiji walipaswa kuwa magerezani.

Serikali tuliyonayo haitokani na ridhaa ya wananchi. Ni zao la uhalifu.
no one can do anything to ccm ukitegemea kujibu mapigo ya hoja na mipango yake ya kusurvive na kutawala kwa kulalamika na kulaumu tu, hali ya kua uko rudderless na clueles mbele kiza totoro...
 
Back
Top Bottom