Kwanza tufahamu kuwa yaliyotokea na yanayotokea hayana budi kutokea na hakuna mwenye uwezo wa kuyazuia yasitokee.
Pili yote anayoyafanya Kwasasa Slaa hana hiari nayo si kwa maana ya ccm au wale wanaomfadhili kwa sasa bali ni laana ya kiapo na nadhiri zake...hawa wanaomfadhili ni kiambishi tu cha nguvu iliyo nje ya uwezo wa kibinadamu .
Slaa anateswa na haiba na kiapo, nadhiri na ahadi ya kutumikia kiapo.. Nimekutana na viapo Nimeishi maisha ya viapo lakini SIKUAPA. viapo ni vibaya na viapo havifi na kuviuwa kunahitaji mlolongo mrefu na wenye mambo mengi.
Slaa Aliitwa kwa wito kuonyesha na kutumia vipawa vyake kwa njia ya upadri akakubali na kupokea mpaka daraja la upadirisho mbele ya mimbari takatifu...aliingia mkataba na Mungu na kukamilisha wito.
Bahati mbaya sana akakengeuka nakuanguka moja kwa moja na tangu hapo viapo nadhiri na laana vikaanza kumuandama.
Siasa sio dini siasa ni propaganda siasa ni unafiki siasa haina kweli na Siasa haiongozwi na roho mtakatifu.
Kwa laana ile ya kiapo na nadhiri akajikuta anaangukia kwenye Ulimwengu wa mapepo na roho za kutangatanga.. Na tangu hapo ameendelea kutangatanga kuanzia kwenye mahusiano mpaka kwenye maisha.
Hakuna ambacho ameweza kufanya kikakamilika, amekosa ndoa takatifu amekosa maisha ya kudumu Kwenye siasa amekosa Kuacha Heshima na historia ya kutukuka kwenye lolote alilolifanya.
Kila alipoanza alianza vizuri kwa mafanikio na kupendwa sana lakini mwishoni kila kitu kikaenda kombo na kugeuka ubatili.... Kiapo kinamtesa.. Na haya ndio atakuwa maisha yake mpaka kaburini .
Viapo ni vibaya hakikisha unatengua kama hutaki kuendelea nacho viapo vina roho na roho haifi, mengi mabaya yatamtokea Dr na hii ni kanuni ya kidunia katika Ulimwengu wa roho.
Kwa Waliosoma walau classical philosophy wanaelewa fallacy maarufu iitwayo "Post Hoc Ego Propter Hoc" - Because of this therefore this!
Nilitamani vigezo JF wanavyotumia kuwapa watu Expert Member...sijui ni expert katika kila jambo au katika specialization Fulani...maana wakati mwingine ni ujinga shehe na padre kurumbana kuhusu nguruwe, maana hatima ya majdiliano hayo inajulikana.
Mimi ni bingwa wa TaaliMungu au Tahuidi au Theology. Na kabla ya hapo ni mbobezi katika Falsafa ya Kiyunani.
Sio kweli kwamba padre akiacha upadre anapata mikosi.....yaani sio de facto! Ndio maana kanisa lenyewe limeweka taratibu za padre kuwacha kuwa padre. Muhusika anaomba laicization ambayo hutolewa na papa peke yake.Majuzi tulishuhudia padre Karugendo akifunga ndoa katika parokia ya Oysterbay. Hapa Tanzania wengi wamepewa hiyo ruhusa na waaendelea na maisha yao kma kawaida. Padre pia anaweza kupokwa hadhi yake ya upadre ndio wanasema amefukuzwa.
Ni kwamba tu Dr.Slaa alikuwa anajishughulisha na siasa ndio maana suala lake linatungiwa nahau na waganga wa kienyeji. Na kwa sababu watanzania tulio wengi hatuna udadisi tunaamini tu....Tunaamini mambo mengi ya kijinga..tunaamini dawa za kuongeza nguvu za kiume...kuongeza makalio nk. ilhali wachina wanaozitengeneza tunaona maumbile yao.
Kwanza kufanya kazi supermarket au hata kuosha vyombo ni kazi azifanyazo mwanadamu kuwa padre hakukufanyi kuwa mtu wa daraja Fulani....pia mwelewe mapadre wa nchi zetu hawana mishahara hivyo kufanya kazi na kupata kipato ni hatua kubwa sana ya kimaendeleo.
Tuache kueneza uongo. Papa Benedict XVI alipojiuzuru jaambo ambalo alikuwahi kufanywa huko nyumba kwa karne 6 watu walidhani ni mwisho wa dunia.....Pope mstaafu yupo mpaka leo...ingawaje waganga wa kienyeji walisema Yesu hakushuka msalabani...hakujiuzuru!
Hakuna jimbo katoliki hata moja hapa Tanzania ambalo halina padre aliyewahi kuacha. jimbo langu Dar es Salaam mapadre wafuatao wameacha na wanaendelea na maisha yao Ngirwa, Matage, Luanda, Lingamila nk nk nk hali kadhalika na majimbo mengine wakiongozwa na jimbo kuu la Mwanza. Mnamkumbuka Askofu Mkuu Millingo wa Zambia.
Tuache ujinga wa kuwajengea watu hofu. Kujadili watu badala ya ideas nk