Kwa jicho la kiroho: Sakata la Dr. Slaa

Kwa jicho la kiroho: Sakata la Dr. Slaa

Kama atakuwa na ujasiri huo atatubu na kujirudi lakini sio leo wala kesho ni mpaka pale atakapogundua kuwa alitumika kwa malengo yaliyo wazi


Kaka Mshana Jr,sina budi nikupongeze kwa hili bandiko hapo juu. Maana hiki kitu niliwahi elezwa na mzee wangu kwamba Dr. w Slaa kamwe hatofika mbali au kupata mamlaka ya juu ya nchi kisiasa au katika utawala kwani tayari amekiuka kiapo. Niwazi hichi kinachotokea si kwa mamlaka yake yy bali ni nguvu ya rohoni inamtesa. Tutegemee makubwa kumfika na kudhihirisha nadhiri aliyofunga na Mungu wake haikupaswa kutenguliwa na Mwanadamu kwa matamanio yasioweka hazina Mbinguni.

Ni wakati wa wanasiasa wa Chama cha Mapinduzi na Chama cha demokrasia na Maendeleo kulianagalia hilo suala kwa umakini mkubwa.Ili basi pale wanapoamua kujibu hoja zake au kumtumia kisiasa waangalie na madhara yake kwa mama Tanzania. Hatuhitaji alete mpasuko kwa Taifa letu kama alivyonena tarehe mosi juu ya maaskofu na kanisa la kilutheri
 
Mbona slaa aliwahi kuonekana huko Israel yeye na Josephine inamaana hakutubu,?

Ni kweli alikwenda hija. Lakini Mwenyezi Mungu anautaratibu wake wa kuyajibu maombi yetu na hutenda kwa majira/wakati wake. Huu ndio wakati wake wa kudhihirisha kuwa bado hakupata msamaha na yampasa kuirudia familia yake ili apate kuikiri imani ya kanisa alimokuwa mtendaji mkuu wa TEC,kumbuka huyu Dr. ni wazi nadhiri mbili za kidunia ambazo hufungwa duniani na mbinguni zote kwa imani ya kikristu amezikiuka. Inatupasa tumpe Mungu sifa kwa kutuonesha aina ya viongozi tuliokuwa nao na pia ametuokoa kwenye mikono yake inayoteswa na uovu aliomtendea muumba wake,tumwombe mungu amhurumie na kumsamehe Makosa yake.
 
Kwani kiapo cha upadre kinazidi kiapo cha nadhiri!
Kwanza tufahamu kuwa yaliyotokea na yanayotokea hayana budi kutokea na hakuna mwenye uwezo wa kuyazuia yasitokee.

Pili yote anayoyafanya Kwasasa Slaa hana hiari nayo si kwa maana ya ccm au wale wanaomfadhili kwa sasa bali ni laana ya kiapo na nadhiri zake...hawa wanaomfadhili ni kiambishi tu cha nguvu iliyo nje ya uwezo wa kibinadamu .

Slaa anateswa na haiba na kiapo, nadhiri na ahadi ya kutumikia kiapo.. Nimekutana na viapo Nimeishi maisha ya viapo lakini SIKUAPA. viapo ni vibaya na viapo havifi na kuviuwa kunahitaji mlolongo mrefu na wenye mambo mengi.

Slaa Aliitwa kwa wito kuonyesha na kutumia vipawa vyake kwa njia ya upadri akakubali na kupokea mpaka daraja la upadirisho mbele ya mimbari takatifu...aliingia mkataba na Mungu na kukamilisha wito.

Bahati mbaya sana akakengeuka nakuanguka moja kwa moja na tangu hapo viapo nadhiri na laana vikaanza kumuandama.

Siasa sio dini siasa ni propaganda siasa ni unafiki siasa haina kweli na Siasa haiongozwi na roho mtakatifu.

Kwa laana ile ya kiapo na nadhiri akajikuta anaangukia kwenye Ulimwengu wa mapepo na roho za kutangatanga.. Na tangu hapo ameendelea kutangatanga kuanzia kwenye mahusiano mpaka kwenye maisha.

Hakuna ambacho ameweza kufanya kikakamilika, amekosa ndoa takatifu amekosa maisha ya kudumu Kwenye siasa amekosa Kuacha Heshima na historia ya kutukuka kwenye lolote alilolifanya.

Kila alipoanza alianza vizuri kwa mafanikio na kupendwa sana lakini mwishoni kila kitu kikaenda kombo na kugeuka ubatili.... Kiapo kinamtesa.. Na haya ndio atakuwa maisha yake mpaka kaburini .

Viapo ni vibaya hakikisha unatengua kama hutaki kuendelea nacho viapo vina roho na roho haifi, mengi mabaya yatamtokea Dr na hii ni kanuni ya kidunia katika Ulimwengu wa roho.
 
Ni kweli alikwenda hija. Lakini Mwenyezi Mungu anautaratibu wake wa kuyajibu maombi yetu na hutenda kwa majira/wakati wake. Huu ndio wakati wake wa kudhihirisha kuwa bado hakupata msamaha na yampasa kuirudia familia yake ili apate kuikiri imani ya kanisa alimokuwa mtendaji mkuu wa TEC,kumbuka huyu Dr. ni wazi nadhiri mbili za kidunia ambazo hufungwa duniani na mbinguni zote kwa imani ya kikristu amezikiuka. Inatupasa tumpe Mungu sifa kwa kutuonesha aina ya viongozi tuliokuwa nao na pia ametuokoa kwenye mikono yake inayoteswa na uovu aliomtendea muumba wake,tumwombe mungu amhurumie na kumsamehe Makosa yake.

Ni Afadhali kutokuweka NADHIRI kabisa.
 
Ni Afadhali kutokuweka NADHIRI kabisa.


Kwa imani ya kikristo nadhiri ni mkataba kati yako na Mungu,kwani hata kuna baadhi ya watawa hujaribu kuolewa na kutafuta kuzaa lkn kwa vile tayari ameweka nadhiri kupata mtoto kwake hugeuka kuwa ndoto. Hii haiwahusu wale ambao bado hawaweka nadhiri ya maisha
 
Lawkeys asante, nimesoma bandiko lako kwa utulivu na nimekuelewa sana tu. Hakika sikujua kuwa Dr ni jesuit na kwa viapo ulivyoviweka nikikonekti doti naungana na wewe kuwa si wa kupuuza! Kwanza moja ya jibu lake alipoulizwa kuhusu gharama za press aliyofanya alisema alidhaminiwa na waliokuwa wakidhamini safari zake za nje wakati chama kikimpa laki tano! :nono:
 
Last edited by a moderator:
Lawkeys asante, nimesoma bandiko lako kwa utulivu na nimekuelewa sana tu. Hakika sikujua kuwa Dr ni jesuit na kwa viapo ulivyoviweka nikikonekti doti naungana na wewe kuwa si wa kupuuza! Kwanza moja ya jibu lake alipoulizwa kuhusu gharama za press aliyofanya alisema alidhaminiwa na waliokuwa wakidhamini safari zake za nje wakati chama kikimpa laki tano! :nono:

Najaribu kutafuta cha kuongeza nakosa na si mimi pekeyangu hata wale wapinzani wa hii post nao wamekuwa kimya kabisa... reply ya Lawkeys ni yenye ufunuo na imekuja katika wakati sahihi
 
Last edited by a moderator:
Zipo nadhiri za upadirisho na hufanyika kwenye ibada maalum na nadhiri hizi huambatana na viapo vya kumkataa shetani na hila zake zote na kazi zake zote.. Nadhiri ni kiapo na kiapo ni maagano kati yako wewe na Mungu, shetani, mwanadamu nk, maagano ni maapizo yanayokazia nadhiri zako
Mimi naapa kwamba Slaa akipita anga hizi lazima akosoe uelewa wako wa nadhiri na kiapo.
 
Tanzania hivi SASA hakuna upinzani Woote fedha NA dhiki vinawasumbua
 
Siku zote uongo hupanda lifti na ukweli hupanda ngazi , Nasubiri siku ya kudhihirika maovu ya Mbowe.!

Siku za kudhihirika kwa unafiki na maovu ya mhe Aikael Mbowe zinasogea
 
kwanza tufahamu kuwa yaliyotokea na yanayotokea hayana budi kutokea na hakuna mwenye uwezo wa kuyazuia yasitokee.

Pili yote anayoyafanya kwasasa slaa hana hiari nayo si kwa maana ya ccm au wale wanaomfadhili kwa sasa bali ni laana ya kiapo na nadhiri zake...hawa wanaomfadhili ni kiambishi tu cha nguvu iliyo nje ya uwezo wa kibinadamu .

Slaa anateswa na haiba na kiapo, nadhiri na ahadi ya kutumikia kiapo.. Nimekutana na viapo nimeishi maisha ya viapo lakini sikuapa. Viapo ni vibaya na viapo havifi na kuviuwa kunahitaji mlolongo mrefu na wenye mambo mengi.

Slaa aliitwa kwa wito kuonyesha na kutumia vipawa vyake kwa njia ya upadri akakubali na kupokea mpaka daraja la upadirisho mbele ya mimbari takatifu...aliingia mkataba na mungu na kukamilisha wito.

Bahati mbaya sana akakengeuka nakuanguka moja kwa moja na tangu hapo viapo nadhiri na laana vikaanza kumuandama.

Siasa sio dini siasa ni propaganda siasa ni unafiki siasa haina kweli na siasa haiongozwi na roho mtakatifu.

Kwa laana ile ya kiapo na nadhiri akajikuta anaangukia kwenye ulimwengu wa mapepo na roho za kutangatanga.. Na tangu hapo ameendelea kutangatanga kuanzia kwenye mahusiano mpaka kwenye maisha.

Hakuna ambacho ameweza kufanya kikakamilika, amekosa ndoa takatifu amekosa maisha ya kudumu kwenye siasa amekosa kuacha heshima na historia ya kutukuka kwenye lolote alilolifanya.

Kila alipoanza alianza vizuri kwa mafanikio na kupendwa sana lakini mwishoni kila kitu kikaenda kombo na kugeuka ubatili.... Kiapo kinamtesa.. Na haya ndio atakuwa maisha yake mpaka kaburini .

Viapo ni vibaya hakikisha unatengua kama hutaki kuendelea nacho viapo vina roho na roho haifi, mengi mabaya yatamtokea dr na hii ni kanuni ya kidunia katika ulimwengu wa roho.

mtumishi umenena, ubarikiwe, bora kuomba kubatilisha kiapo vinginevyo mapigo yatakufuata popote uendapo maana kiapo ni agano
 
Back
Top Bottom