Hii kada ndio ilikuwa chaguo No.1 kwa mwanangu nyuma ya TPA na Jeshi la Wananchi kwa pass ya Grade 2 ya Point 19, Intake ya mwaka 2023
Ila kwa hali ya nchi inakoelekea sihitaji mwanangu atengwe na ndugu zake kisa kusomea hii kozi.
Majibu yametoka na kafaulu kwenda chuo cha Upolisi (CCP Moshi), ila naghahiri kumpeleka mara moja.
Serikali, naomba pia hili mliangalie kwani huko tunakoelekea sidhani kama kuna mzazi mwenye akili timamu atakubali mwanae achekwe au kudharaulika hadharani kisa hii kazi.
Mwanangu anaonekana kukosa amani tangu aone yanayoendelea nchini huku yeye mwenyewe akiwa mstari wa mbele katika kutimiza malengo yake.
Heri aende kozi ya Jeshi tu japo dirisha lishafungwa na Intake mpya imeveshwa gwanda pale Juzi Monduli ila atapeleka maombi hata mwakani.
Mimi mzazi wake ni kada kindakindaki wa Chama cha Mapinduzi (CCM), ila kwa hili hapana.
Wabillahi Tawfiq 🙏
Niwatakie Alhamis Njema.