Kwa CHADEMA kuanza kupokea ruzuku, akina Halima Mdee wanasameheka

Petro E. Mselewa

JF-Expert Member
Dec 27, 2012
10,197
25,516
Nawasalimu waungwana wote wa JF,

Nimesoma mahali kuwa CHADEMA wameanza kupokea ruzuku za kila mwezi zinazotokana na uchaguzi mkuu wa mwaka 2020. Ulikuwa ni msimamo wa CHADEMA kuwa uchaguzi mkuu wa 2020 haukuwa halali na ulikuwa uchafuzi na si uchaguzi. Kutokana na kutokuwa halali, ulikuwa ni msimamo wa CHADEMA kuwa mazao yote ya uchaguzi huo: Wabunge wa kuchaguliwa na wale wa viti maalum pamoja na ruzuku yalikosa uhalali.

Rais Samia Suluhu Hassan na Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe 'wamefanikisha na kuasisi' maridhiano ya kitaifa ya kisiasa ambayo yapo kwenye utekelezaji unaotia matumaini na nguvu ya kusonga mbele tukiwa wamoja kama taifa. Pamoja na kubatilishwa katazo la mikutano ya hadhara ya kisiasa, Rais Samia anaonyesha kwa vitendo utekelezaji wa maridhiano hayo. CHADEMA nao hawako nyuma. Wameanza mikutano yao ya hadhara na kupokea ruzuku.

Leo hii, Rais Samia ni Mgeni Rasmi kwenye Kongamano la Baraza la Wanawake CHADEMA (BAWACHA) (katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani) huko Moshi, mkoani Kilimanjaro. Sasa ni dhahiri kuwa maridhiano yanaleta mapatano; amani; utulivu; ustahimilivu wa kisiasa; msamaha na ustawi wa kidemokrasia. Ni wakati sahihi wa akina Halima Mdee kusamehewa na kurejeshwa kundini CHADEMA, kama wako tayari kwa jambo hilo.

Akina-Halima Mdee ambao walifukuzwa uanachama wa CHADEMA na sasa wako Mahakama Kuu ya Tanzania kusaka haki yao, hata kama walikuwa na makosa na ukakasi wa kuteuliwa kwao kuwa Wabunge wa Viti Maalum wanasameheka. Ni wakati wa zama mpya. Ni wakati wa kuwa pamoja. Binafsi, mbele ya Rais Samia huko Moshi, naitarajia kauli ya CHADEMA kupitia Mbowe au mwingine kuwa akina Halima Mdee wamerudishwa kundini. Kesi yao nayo yapaswa kuondolewa mahakamani. Halafu, heshima;kufuata utaratibu; nidhamu na adabu zinapaswa kutembea nao popote.

Kila la heri Wanawake wote wa Tanzania katika kuadhimisha siku yao!
 
Kitendo cha CDM kuwasamehe hao wahuni kutaharibu haiba yao na kitaigharimu sana cdm. Mtaji wa CDM ni watu, hao viongozi wenye tamaa ya fedha ni sehemu ndogo sana ya ubora wa CDM. Tuko sisi wafuasi wa CDM ambao hatutakuwa nao pindi wakichukua hatua hizo. Tulivumilia kwa shingo upande ujio wa Lowassa, ila sio hili.
 
Kitendo cha CDM kuwasamehe hao wahuni kutaharibu haiba yao na kitaigharimu sana cdm. Mtaji wa CDM ni watu, hao viongozi wenye tamaa ya fedha ni sehemu ndogo sana ya ubora wa CDM. Tuko sisi wafuasi wa CDM ambao hatutakuwa nao pindi wakichukua hatua hizo. Tulivumilia kwa shingo upande ujio wa Lowassa, ila sio hili.
Unamsamehe vipi mtu ambae hajaomba msamaha? Na mbaya zaidi amekupeleka mahakamani kwa sababu anaamini ulimuonea? Kitu kimoja kizuri ambacho wamekifanya ni kutokipakazia chama chao cha zamani kama walivyofanya wakina Lijualikali, Silinde, Mollel na hata Slaa. Kama kweli wanataka kurudi Chadema inabidi wajiuzuru ubunge wao na wakiri kuwa walikosea bila masharti yeyote.

Chadema wakiamua kuwarudisha arbitrarily kutawafanya wanachama na mashabiki wao wengi wakose imani nao. Hii ni kwa sababu kitendo kilichofanywa na wakina Halima kiliwaumiza mno hasa kutokana na mapenzi na imani kubwa waliyokuwa nayo juu yao.

Amandla....
 
Ila ruzuku inayotokana na ubunge wao mnaitaka😅😅😅njaa mbaya
Again huu ndio upumbavu mwingine, why hujisomei kupata facts?,ubunge wao umetokana na KURA walizopata CDM kwenye uchafunzi ule, shirikisha ubongo wako pls na usiwe mvivu wa kutafuta facts
 
Kitendo cha CDM kuwasamehe hao wahuni kutaharibu haiba yao na kitaigharimu sana cdm. Mtaji wa CDM ni watu, hao viongozi wenye tamaa ya fedha ni sehemu ndogo sana ya ubora wa CDM. Tuko sisi wafuasi wa CDM ambao hatutakuwa nao pindi wakichukua hatua hizo. Tulivumilia kwa shingo upande ujio wa Lowassa, ila sio hili.
Hahahha... Utafanya nini?

Kama leo wanapokea ruzuku waliyoikataa mbele ya hadhara kwamba hawawezi kuchukua hela iliyotokana na uchaguzi uliojaa damu, na nyie wafuasi mmekaa kimya mtafanya nini kina Mdee wakisamehewa?

Ni hivi, anachoamua Mbowe nyie vidagaa hamuwezi kupinga zaidi ya kuumia kimoyomoyo tu
 
Again huu ndio upumbavu mwingine, why hujisomei kupata facts?,ubunge wao umetokana na KURA walizopata CDM kwenye uchafunzi ule, shirikisha ubongo wako pls na usiwe mvivu wa kutafuta facts
Fact gani mlisema ruzuku hamtaki,imekuwaje?😅😅
 
Nawasalimu waungwana wote wa JF,

Nimesoma mahali kuwa CHADEMA wameanza kupokea ruzuku za kila mwezi zinazotokana na uchaguzi mkuu wa mwaka 2020. Ulikuwa ni msimamo wa CHADEMA kuwa uchaguzi mkuu wa 2020 haukuwa halali na ulikuwa uchafuzi na si uchaguzi. Kutokana na kutokuwa halali, ulikuwa ni msimamo wa CHADEMA kuwa mazao yote ya uchaguzi huo: Wabunge wa kuchaguliwa na wale wa viti maalum pamoja na ruzuku yalikosa uhalali.

Rais Samia Suluhu Hassan na Mwenyekiti wa CHADEMA Freeman Mbowe 'wamefanikisha na kuasisi' maridhiano ya kitaifa ya kisiasa ambayo yapo kwenye utekelezaji unaotia matumaini na nguvu ya kusonga mbele tukiwa wamoja kama taifa. Pamoja na kubatilishwa katazo la mikutano ya hadhara ya kisiasa, Rais Samia anaonyesha kwa vitendo utekelezaji wa maridhiano hayo. CHADEMA nao hawako nyuma. Wameanza mikutano yao ya hadhara na kupokea ruzuku.

Leo hii, Rais Samia ni Mgeni Rasmi kwenye Kongamano la Baraza la Wanawake CHADEMA (BAWACHA) (katika Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani) huko Moshi, mkoani Kilimanjaro. Sasa ni dhahiri kuwa maridhiano yanaleta mapatano; amani; utulivu; ustahimilivu wa kisiasa; msamaha na ustawi wa kidemokrasia. Ni wakati sahihi wa akina Halima Mdee kusamehewa na kurejeshwa kundini CHADEMA, kama wako tayari kwa jambo hilo.

Akina-Halima Mdee ambao walifukuzwa uanachama wa CHADEMA na sasa wako Mahakama Kuu ya Tanzania kusaka haki yao, hata kama walikuwa na makosa na ukakasi wa kuteuliwa kwao kuwa Wabunge wa Viti Maalum wanasameheka. Ni wakati wa zama mpya. Ni wakati wa kuwa pamoja. Binafsi, mbele ya Rais Samia huko Moshi, naitarajia kauli ya CHADEMA kupitia Mbowe au mwingine kuwa akina Halima Mdee wamerudishwa kundini. Kesi yao nayo yapaswa kuondolewa mahakamani. Halafu, heshima;kufuata utaratibu; nidhamu na adabu zinapaswa kutembea nao popote.

Kila la heri Wanawake wote wa Tanzania katika kuadhimisha siku yao!
1. Kama imethibitika kuwa, Mwendazake John P. Magufuli na kundi lake liliwatishia uhai wao na kuwalazimisha kuuopkea huo ubunge haramu kwa nguvu, basi hilo linaeleweka na (labda) inazungumzika Kwa muktadha wa kusameheana..

2. Hata hivyo, ruzuku ya CHADEMA haina uhusiano na ubunge wa viti maalumu wa kina Halima Mdee na wenzake. Nina maana kuwa, hata kama kina Mdee watafukuzwa ubunge Leo Kwa kukosa uhalali wa kisheria, bado CHADEMA ruzuku yao itaendelea kuwepo.
 
Kitendo chochote cha kuwasamehe wahuni waliojaa viburi walivyojazwa na mwendazake na Ndugai wale ambao waliwatesa viongozi wa Chadema usiku na mchana ni ujuha.

Chadema wakithubutu kufanya hivyo itawalazimu waache kumsema vibaya Magufuli, kwasababu watakuwa wamepigia mstari yale yote waliyofanyiwa wakati wa awamu ile.
 
Back
Top Bottom