Kutoka Ikulu: Baraza la Mawaziri kutangazwa J'tano (kesho)

Status
Not open for further replies.
Baraza la mawaziri litatangazwa muda wa saa tisa mchana leo hii( kwa saa za Tanzania)..Kawaida huwa linatangazwa muda huo
kwani imekuwaje asitangaze saa nne kama tulivyo taarifiwa awali au kajangwani?
 
Huwa najiuliza kila siku hii ofisi iliyotoa hii taarifa ni:

a. Ofisi ya Mawasiliano ya Rais - Presidential Communication Office - private and public????
b. Ofisi ya Mawasiliano ya Ikulu - Statehouse Office of Communication
c. Ofisi ya Habari ya Ikulu - Statehouse Public Information Office
d. Ofisi ya Habari za Rais - Office of Presidential News


Kwa ufupi ni ofisi ya mawasiliano au ya habari?
 
kutokana na tatizo la umeme ktk maeneo mengi jijini dar, naomba wadau mpost hapa jf mara baraza litakapotangazwa, maana hapa nilipo umeme toka jana saa 4 hadi sasa saa 5 asubuhi bado haujarudi, sasa wadau mtujulishe hilo baraza litakapokuwa limetangazwa, naomba kuwasilisha kwenu.

subirini mpaka tutakapoagiza mitambo kutoka richard monduli kama ilivyokuwa mara tu baada ya serikali ya jk kuingia madarakani 2005. Huyo sitta wenu tushapiga chini na mzito wenu tunaye kiroho. Hivyo mkitaka kurejesha amani yenu katika hili joto kubalini tuingize mitambo ya richard monduli.
 
Na hicho kiswahili kilotumiwa .....mmmh hapana kwa kweli. Hakivutii.
 
kutokana na tatizo la umeme ktk maeneo mengi jijini dar, naomba wadau mpost hapa jf mara baraza litakapotangazwa, maana hapa nilipo umeme toka jana saa 4 hadi sasa saa 5 asubuhi bado haujarudi, sasa wadau mtujulishe hilo baraza litakapokuwa limetangazwa, naomba kuwasilisha kwenu.

Mhhh ndugu yangu yaonekana haupo Tanzania, maana saa yako iko mbele dakika 23 nzima. Hivi sasa ni saa nne na dakika 38.
 
Mkuu Invisible, hii ni ndoto kwa CCM kuruhusu foreign impurities kuingia kwenye mtandao wao!!! Hakuna jipya, sana sana ataongeza idadi ya wanawake na kujisifia.

Anyways, tusubiri.
Kwani CUF nao ni impurity.......??? Upinzani si CDM pekee, kuna TLP vile vile
 
Huwa najiuliza kila siku hii ofisi iliyotoa hii taarifa ni:

a. Ofisi ya Mawasiliano ya Rais - Presidential Communication Office - private and public????
b. Ofisi ya Mawasiliano ya Ikulu - Statehouse Office of Communication
c. Ofisi ya Habari ya Ikulu - Statehouse Public Information Office
d. Ofisi ya Habari za Rais - Office of Presidential News


Kwa ufupi ni ofisi ya mawasiliano au ya habari?

MM Naona hapo kuna ofisi za Habari mbili (moja ya Rais nyingine Ikulu) na Ofisi za Mawasiliano mbili (moja ya Rais nyingine Ikulu)
 
Duuu mwaka 2005 alitangaza saa 3 asubuhi....leo vipi au anapiga ramli kwanza??aibu nchi mwz mzima haina full cabinet...kwani wabunge si alikuwa anawajua in 3 days baada uchaguzi???one man show ......kudumaza uchunmi vitu vingi vimesimama...malipo kibaooo yamesiamamaa
 
Naona mna matumbo joto.
Tuendelee kukata ishu za kujenga chi yetu. tumwachie mkwere na cabinet yake watangazane wagawane urithi
 
Hakuna jipya hapa kama sikosei kumbukumbu zangu zinaonyesha alishawahi kuishika hiyo Wizara.

Kaka hapo unakosea watu hubadirika Sitta sasa ktk CCM ndiye tunamwona wadilifu na anafuata nyayo za baba wa Taifa hivyo ni bora tuombe mungu tetesi hizi ziwe za kweli kwakuwa Sitta anauwezo wa kujenga hoja ya kubadili katiba na mambo mengi yaliyopitwa na wakati kurekebishwa ila sidhani kama CCM inaweza fanya kosa hilo la kumpa sitta wizara hiyo kwakuwa hata NEC anaweza kuiboresha

Sitta ni mwadilifu na mpenda maendeleo ya nchi yetu na watu wake pia ni mjamaa wa kweli mimi nampenda sitta kuendelea kuwa kiongozi wa kitaifa bila kujali anapitia chama gani kwakuwa Sitta ni Mzalendo na mawazo na matakwa yake yako juu ya hila za chama chake chenye mlengo wa kizandiki
 
Ni kwamba Rais jana alilala kijijini kwao Msoga, ndio yupo njiani anarudi Ikulu sasa
 
Baada ya kukataa kwa muda sasa kutokana na ushauri aliyokuwa anapewa na rafiki zake wakiongonzwa na Seleli aliyesafiri toka Dar kwenda Dodoma kumwambia Sitta asikubali kupewa uwaziri, sasa dhamana ameikubali na kupuuza maneno ya marafiki. Ndiye Waziri wa SHERIA NA KATIBA. Nakutakia kila la kheri na uongoze kwa haki na si majungu.


kama litakuwa kweli ninakuwa wakwanza kumpongeza Rais kwa hekima na busara zake; kwa maana nyingine anamwambia fanya kweli ili demokrasia yetu ikue. Sasa tutashuhudia ukweli wa mambo je baada ya mzalendo kupewa jembe na nyundo atatumia kujenga nyumba yetu ya Tanzania au atakuwa mchagua jembe si mkulima? Just crossing my fingers for the tetesi to be breaking news!
 
Kufuatia mambo mengi aliyo nayo JK, ameahirisha utangazaji wa baraza la mawaziri mpka hapo kesho saa 4 asubuhi.
 
Status
Not open for further replies.
Back
Top Bottom