Kutoka Bungeni-Star TV wamnyima coverage Mbunge Hines CHADEMA Ilemela

Utakuwa umechelewa sana kugundua hilo. Tangu bunge limeanza hajawahi kuonekana Star TV hata kwenye shughuli zinazofanyika Mwanza ama bungeni. Hilo ni agizo toka kwa bwana mkubwa DIALO mwenyewe kwa wafanyakazi wake na wameshaonywa kuwa akija kuonekana kwenye TV yake basi wewe uliyemuonyesha kibarua huna. Siasa na umiliki wa vyombo vya habari ndio matokeo yake haya
Du hii sasa kali imeniacha hoi. Mheshimiwa Highness Kiwia amesema hataacha maandamano kwani ndo yamemleta hapo Mjengoni- Kwahiyo kuacha maandamano ni sawa na mtu kumtukana baba na mama- Hinyo maandamano ni kama Baba na Mama kwa mh. Highness.
 
Huko ni kuvunja sheria za Tanzania chini ya kifungu cha kutoa na kupokea habari.
 
Hii ni hatari kwa taifa letu,sheria inabidi itungwe kuhusu mwana siasa asiruhusiwe kumiliki wala kuwa na hisa kwenye chombo chochote cha habari ili kuepuka migongano ya kimaslahi.
 
aaaaah diallo anapoteza mda wake tu..wananchi hawakumchagua kiwia ili aonekane star tv..alichaguliwa akiwa haonekani star tv so dialo anajaza maji kwenye gunia tena kwa kisoda...
 
Katika TV inayoibeba CDM hapa nchi ni STAR TV kila Jumapili tuongee asubuhi lazima wanachama wa CDM wale wanafunzi wa SAUT, wanapewa nafasi wanamwaga pumba zao! Hata Pro-CDM- JF, nawo pia huwa wanabebwa na STAR TV katika michango yao kupitia JF,&lt;br /&gt;<br />
Leo eti STAR TV wamekuwa wabaya, bora umfadhili mbuzi kuliko binadamu
Ningeomba kukuuliza tu, hivi wewe ni binadamu au Robbot (automatic mashine )? maana inawezekana ni mtambo tu uliosetiwa kuwa against kwa lolote litakaloletwa hapa jamvini.
Na kama wewe ni binadamu basi utakuwa una jicho moja kama la treni.
 
Ningeomba kukuuliza tu, hivi wewe ni binadamu au Robbot (automatic mashine )? maana inawezekana ni mtambo tu uliosetiwa kuwa against kwa lolote litakaloletwa hapa jamvini.<br />
Na kama wewe ni binadamu basi utakuwa una jicho moja kama la treni.
<br />
<br />
Mkuu, nimekuelewa!
 
kwa wanaotazama bunge,mbunge wa ilemela amechangia wizara ya mambo ya ndani kwa tarikani dk 8 hivi lakini star tv inayomilikiwa na dialo aliyengolewa na hines amenyimwa coverage kwa muda wote huo.

Walikuwa wakionesha tu picha za wabunge wegine huku ikisikika tu sauti yake pekee

je hili ni iagizo la dialo kwa wafanyakazi wake
watakoma kulinga! Umesahau wakati wa campaign, ilikuwa ni television ya chama.
 
Kama kuna mtu alitazama kipindi cha mjadala wa Bunge siku ya Ijumaa kati ya saa 5.15 hadi 5.45 wakati mbunge wa Ilemela ndg HIGHNES SAMSON KIWIA anachangangia atagundua kuwa Star Tv hawakutaka kumuonyesha kabisa huyu bwana badala yake camera zilielekezwa kwa mawaziri na watu wengine tu mpaka pale alipomaliza.

Ni kitendo ambacho kama unatumia akili utagundua kuwa ni kitendo ambacho kilikusudiwa. Hivi kuna Bifu lolote kati ya huyu mbunge na kituo hiki cha TV?
 
Japo mmiliki wa Star TV, Dr wa kuchonga Antony Diallo ndiye aliyekuwa mbunge wa Ilemela kupitia magamba, lakini siamini kama ndiye yeye aliyetoa amri hiyo kwa sababu, ukiondoa hiyo sarakasi ya Udakitari wake, huyu jamaa ni decent hawezi kufanya upuuzi wa kitoto kihivyo.

Nadhani ni director wa matangazo yale na wazimu wake kujipendekeza kwa bosi wake kama ishara ya kumpa pole kwa kipigo cha aibu cha kugalagazwa na kijana mdogo wa Peoples Power!.
 
Nadhani ni kujipendekeza kwa bosi wao hao waliokuwa wanasimamia matangazo.
 
Mkurugenzi star tv awaombe radhi watazamaji wa star tv na achukue hatua za nidhamu dhidi ya aliyesimamia matangazo siku hiyo kwani wengi tunaimani sana na kituo hiki.
 
Sawa sawa tu, hata mimi niko nymbani tv iko sitting room, ninachohitaji ni sauti tu sina haja na sura ya mtu. inaonekana wewe ni miongoni mwa wale waliompigia kura kura JK kwa kigenzo eti ni handsome! ujinga mtupu.
<br />
<br />
Matola nitake radhi haki ya nani. Kunisingizia nimepigia kura jah kaya ni tusi kubwa sana nitake radhi.
 
Matola plz plz nitake radhi. Ukigoma mod naomba msaada wako Matola aniombe radhi kwa kunisingizia na kunidhalilisha eti nilimpigia kula Jaa K. Amenivunjia sana imani kwa wanajamvi makini ambao wananiheshimu sana..
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom