SAYVILLE
JF-Expert Member
- Mar 25, 2010
- 5,129
- 7,898
Kuna hili jambo niliwahi kuambiwa ila sikulitilia maanani siku za nyuma ila wiki hii nalishuhudia tena.
Pale timu mojawapo inapokuwa mwenyeji wa mechi hii ya "dabi", hiyo timu mwenyeji kwa kuwa inaenda kupata mapato yote ya mchezo ndiyo pekee inafanya hamasa. Timu ambayo ni mgeni "inauchuna" eti ili uwanja usijae kuathiri mapato ya mechi. Hili ni jambo la kushangaza sana.
Tafsiri ya haraka haraka unaweza ukadhani hili jambo linaleta mantiki yoyote kuepuka kumfaidisha timu pinzani ila embu tujiulize jambo lingine.
Hivi Yanga hawataki mashabiki wake waje uwanjani kwa wingi 16/04 kuipa sapoti timu yao? Je uwanja ukijaa mashabiki watupu wa Simba, Yanga hawadhani watakuwa kwenye disadvantage uwanja mzima ukiwa mwekundu na mweupe? Mbona tukiwa tunahamasisha katika mechi za CAF, huwa tunaongea mshabiki kama mchezaji wa 12, lakini kwenye "dabi" tunaangalia tu faida ya kifedha kwa timu pinzani? Kwa nini huwa tunalialia tukicheza ugenini huko mashindano ya CAF kuwa ni kugumu na sababu mojawapo huwa tunasema ni viwanja kujaa mashabiki wa timu tunazocheza nazo?
Nimegundua kuna matatizo mawili kwenye timu zetu hizi mbili.
Kwanza kuna maamuzi huwa yanafanywa kwa mihemko zaidi na ni ngumu sana kuyabadili maana watu wanaogopa kuonekana wasaliti. Matokeo yake tunaishia kufanya mambo kwa mazoea.
Pili, shangilia zetu viwanjani zaidi ni kupiga kelele, kwa hiyo hizi timu zinaona hata uwanja ukijaa Simba watupu (au Yanga watupu), ukiacha muonekano wa rangi za watazamaji, kelele za timu hizi mbili hazitofautiani.
Hizi timu hazina nyimbo ambazo zinaimbwa uwanja mzima wakati mechi inaendelea na hazina shangilia zinazotofautiana sana.
Sitaki tena kusikia kauli za "mshabiki ni mchezaji wa 12". Sitaki tena kusikia uhamasishaji wa kwenda nchi jirani na kutaka kulipisha watu 700,000/= maana huko tunapowapeleka mashabiki wetu mapato yote yatachukuliwa na mwenyeji.
Pale timu mojawapo inapokuwa mwenyeji wa mechi hii ya "dabi", hiyo timu mwenyeji kwa kuwa inaenda kupata mapato yote ya mchezo ndiyo pekee inafanya hamasa. Timu ambayo ni mgeni "inauchuna" eti ili uwanja usijae kuathiri mapato ya mechi. Hili ni jambo la kushangaza sana.
Tafsiri ya haraka haraka unaweza ukadhani hili jambo linaleta mantiki yoyote kuepuka kumfaidisha timu pinzani ila embu tujiulize jambo lingine.
Hivi Yanga hawataki mashabiki wake waje uwanjani kwa wingi 16/04 kuipa sapoti timu yao? Je uwanja ukijaa mashabiki watupu wa Simba, Yanga hawadhani watakuwa kwenye disadvantage uwanja mzima ukiwa mwekundu na mweupe? Mbona tukiwa tunahamasisha katika mechi za CAF, huwa tunaongea mshabiki kama mchezaji wa 12, lakini kwenye "dabi" tunaangalia tu faida ya kifedha kwa timu pinzani? Kwa nini huwa tunalialia tukicheza ugenini huko mashindano ya CAF kuwa ni kugumu na sababu mojawapo huwa tunasema ni viwanja kujaa mashabiki wa timu tunazocheza nazo?
Nimegundua kuna matatizo mawili kwenye timu zetu hizi mbili.
Kwanza kuna maamuzi huwa yanafanywa kwa mihemko zaidi na ni ngumu sana kuyabadili maana watu wanaogopa kuonekana wasaliti. Matokeo yake tunaishia kufanya mambo kwa mazoea.
Pili, shangilia zetu viwanjani zaidi ni kupiga kelele, kwa hiyo hizi timu zinaona hata uwanja ukijaa Simba watupu (au Yanga watupu), ukiacha muonekano wa rangi za watazamaji, kelele za timu hizi mbili hazitofautiani.
Hizi timu hazina nyimbo ambazo zinaimbwa uwanja mzima wakati mechi inaendelea na hazina shangilia zinazotofautiana sana.
Sitaki tena kusikia kauli za "mshabiki ni mchezaji wa 12". Sitaki tena kusikia uhamasishaji wa kwenda nchi jirani na kutaka kulipisha watu 700,000/= maana huko tunapowapeleka mashabiki wetu mapato yote yatachukuliwa na mwenyeji.