Nyani Ngabu
Platinum Member
- May 15, 2006
- 98,008
- 142,667
Mods posts zangu zimefutwa kwa sababu gani?......
Ukihoji sana utakula ban kama kipindi kile. Unakumbuka ulivyokulaga ile ban?
Mods posts zangu zimefutwa kwa sababu gani?......
Huu ni mjadala wa kubadilishana mawazo kitaaluma. Hivyo kama unataka kumpa ongera Baraka Obama, nakushauri fanya hivyo kwenye thread nyingine.
Jana nilipokuwa naangalia matangazo kutoka katika Boston na Chicago niliona vitu viwili muhimu. Kitu cha kwanza kwenye kambi Romney waliokuwa wanasubiri matokeo wengi walikuwa wazee na wazungu. Kitu cha pili katika kambi iliyokuwepo Chicago, wengi walikuwa ni vijana na vilevile kutoka jamii mbalimbali.
Ukichunguza vitu hivi viwili kwa makini, unaweza kusema kuwa Obama amechaguliwa sio kwa sababu anamzidi Romney kiutendaji wa kazi. Amechaguliwa kwa sababu ya muundo wa jamii zilizopo Marekani. Hii ni sababu moja na zinaweza kuwepo zingine.
Ningeomba tuzichambue hizo sababu hili tujifunze.
Z10.......
Ukihoji sana utakula ban kama kipindi kile. Unakumbuka ulivyokulaga ile ban?
Typically CCM till 2015, after that utahamia CUF.
Nakubaliana na points zako nyingi. Naomba tuzungumze kuhusu kijiandaa. Romney amejiandaa kwa uchaguzi huu kwa zaidi ya miaka sita. Miaka miwili ya mwanzo alijiandaa kuwa mgombea wa uchaguzi wa 2008.
Na baada ya 2008 alianza kujiandaa na 2012. Hivyo kwa kujianzaa, alikuwa kamili. Je kuna kasoro yoyote katika maandalizi yake?
Z10, wanabodi wamechangia hoja nyingi za msingi zilizosababisha Romney ashindwe. Naomba kuongezea muonekano wa Obama na mkewe pia ulikuwa na mvuto kwa wapiga kura. Ile familia ina mvuto fulani ambao umeifanya kukubalika na Jamii apart from sera.Huu ni mjadala wa kubadilishana mawazo kitaaluma. Hivyo kama unataka kumpa ongera Baraka Obama, nakushauri fanya hivyo kwenye thread nyingine.
Jana nilipokuwa naangalia matangazo kutoka katika Boston na Chicago niliona vitu viwili muhimu. Kitu cha kwanza kwenye kambi Romney waliokuwa wanasubiri matokeo wengi walikuwa wazee na wazungu. Kitu cha pili katika kambi iliyokuwepo Chicago, wengi walikuwa ni vijana na vilevile kutoka jamii mbalimbali.
Ukichunguza vitu hivi viwili kwa makini, unaweza kusema kuwa Obama amechaguliwa sio kwa sababu anamzidi Romney kiutendaji wa kazi. Amechaguliwa kwa sababu ya muundo wa jamii zilizopo Marekani. Hii ni sababu moja na zinaweza kuwepo zingine.
Ningeomba tuzichambue hizo sababu hili tujifunze.
Z10
Huu ni uchambuzi au pumba? Anyway, Romney kashindwa kwa sababu nyingi tu, baadhi zikiwa ni:-Machozi ya Obama ndo ilikuwa zuga kubwa, wamarekani walidanganyika na vilio vya Obama kwenye campaign zake za mwisho..! Walidhani anawalilia wamarekani kumbe alikuwa anaulilia urais
Kambi ya Obama ilionekana kuungwa mkono na watu wa asili tofauti ukilinganisha na kambi ya Romney. Ni wazi kushindwa kwa Romney kumetokana na kuungwa mkono na wazungu wengi tena wazee ambao idadi yao katika ujenzi wa nchi ni mdogo. Sera zake za ndani hasa za uchumi was fine ila sera za nje hazikushawishi wapiga kura.
Ndugu yangu Zakumi, heshima yako sana bro! loong time!:
- Romney ameshindwa kwa sababu zile zile zinazomfanya Giuliani Popular Mayor wa zamani wa New York ashindwe kwua Rais kila anapogombea,
- Republicans hawachagui Rais aliyewahi kuwa Gavana au Mayor wa East Coast, mikoa ambayo inafahamika sana kwa ku-support Gay Marriages, Food Stamps, Abortions na Unions. Hizi ni sumu kwa Conservatives na ndio maana Mayor wa sasa wa New York pia anaogopa kugombea Urais.
- Huwezi kushinda Urais wa USA as Republican bila 100% Support ya Conservatives, including watangazaji wa Radio Rush Limbaugh, The Great One Mark Levine na Sean kutoka ABC RADIO, hawa wote hawakuwa wanaamuunga mkono Romney.
- Again ni vigumu sana kwa Republican asiyetokea South States kushinda Urais wa USA, Romney Republican kutokea Boston, alikuwa ameshashindwa hata kabla ya uchaguzi kuanza, kulichomfikisha hapo alipofikia ni mapesa yake mengi sana, halafu pia Dini yake Romney nayo ni tatizo kubwa sana Wamarekani hawachagui a Mormon ambayo ndio dini yake kuwa Rais wao.
Media ya USA ilikuwa inajua toka day one kwamba Romney hashindi, lakini kwa sababu they had to make money wakaanza uongo mwingi wa kuwa Race is tight, ndio maana ya Capitalism ni kutengeneza faida popote pale kwa kugeuza geuza habari ingawa ukweli unafahamika.
- The best Candidate Republicans had kumshinda Obama, alikuwa ni Christie Chrstie Gavana wa New Jersey, ambaye hata kambi ya Obama ilishaanza kumshambulia bila kutangaza kwamba anagombea, lakini akaogopa uwezo wake mdogo wa kuchangisha pesa za uchaguzi, hivyo akakataa kugombea and that was it!!
Le Mutuz!!
Every vote counts. Sasa wale wasiotaka "siasa" badala yake wanachagua mgombea kwa muonekano wake, lazima wafikiriwe kama Dr.Slaa anataka kura zao
*Sayansi ndio iliyosema kuwa wapo watu wanaochagua kwa muonekano, sio maneno yangu.
Usiwe na tabia ya hindi kila jino kukutafuna.
sababu kubwa ya Romney kushindwa ni kutokana na matamshi yake kuwa asilimia 47% ya wamarekani wanaishi kwa kutegemea ruzuku/msaada wa serikali.
Hivyo watu wengi walio maskini walikasirika na kumuona Romney kuwa akichaguliwa atawapendelea matajiri na kuwaacha maskini wakitaabika kwa kuwafutia posho za serikali kama ilivyotokea kwa chama cha sasa kinachotawala Uingereza. Hili ndilo pekee lililomwangusha.
Lakini laiti wamarekani wangechambua kwa umakini kauli yake wangejua alikuwa hapendezwi na umaskini wao katika taifa kubwa kama lile na angefanya bidiii kuwapa fursa ambazo zingepunguza kiwango cha umaskini wao na utegemezi wao kwa serikali.
Hili ndilo tatizo la wapiga kura wengi wanaofikiria kushiba leo bila kujali kesho yake itakuwaje?