Kusema Rais anashauriwa vibaya ni kujaribu kueleza kuwa Rais hana akili; naona ni ukosoaji wa kinafiki

Robert Heriel Mtibeli

JF-Expert Member
Mar 24, 2018
21,340
51,900
Kwema Wakuu!

Hakuna Jambo ambalo linanikera kama kumsikia MTU akisema Rais anashauriwa vibaya na washauri wake. Watu wengi wanaosema hivyo ni Watu wasioweza kueleza mambo bayana. Ni Watu wakupindisha pindisha maneno. Wasioweza kutamka nyeusi ni nyeusi na nyeupe ni nyeupe.

Rais kama kakosea sema kakosea. Inatosha. Mambo ya kuanza kumtetea kuwa kashauriwa, sijui washauri wake ni wabaya ni kujaribu kumnasua na Matendo anayoyafanya. Ni kama unajaribu kueleza kuwa Rais Hakosei Jambo ambalo ni Uongo. Hakuna binadamu asiyekosea.

Kusema Rais anashauriwa vibaya kunatoa tafsiri na maana nyingi kama ifuatavyo;

1. Woga na unafiki
Unashindwa kuongea moja Kwa moja kuwa hapa Rais kakosea. Yaani kiufupi unashindwa kuwa mkweli. Watu Wanafiki wanatabia ya kutaka kuongea lakini wakiongea hushindwa kusema Ukweli. Wanakuwa na kiherehere na uchawa au upambe. Huo ni unafiki.
Wakweli wananamna mbili ya kufanya, ni aidha aseme ukweli wote pasipo kufichaficha au kunyamaza Kabisa. Sio kutoa mambo nusunusu.

2. Inamaanisha Rais Hana Akili ya kujua kibaya ni kipi na kizuri ni kipi

Rais sio Mtoto Mdogo, kusema Rais anashauriwa vibaya yaani anadanganywa ni kujaribu kueleza kuwa Rais hana Akili.

Kwamba yeye akipewa ushauri anaufanya pasipo kufikiri. Kiufupi ni matusi kusema Rais anashauriwa vibaya.
Mbali na hivyo ni kujaribu kusema wapo Watu wanaomdharau Rais na kutokumheshimu(kutokumuogopa) ndio maana wanauwezo WA kumshauri vibaya(kumdanganya). Hiyo sio tuu kumtukana Rais Bali kutukana Taasisi nzima ya Urais.

3. Inamaanisha Rais ni Mbaya na muovu
Yaani waje Watu wakushauri hapo twende tukaibe, au tupige dili alafu ukakubali alafu atokee mtu aseme umeshauriwa vibaya.

Kikawaida washauri hutoa ushauri kulingana na MTU alivyo. Ukiwa Mbaya utapewa ushauri Mbaya. Ukiwa mzuri ni ngumu sana washauri kukupa ushauri Mbaya Kwa sababu wanakujua fika. Tena Kwa nafasi ya Rais ni ngumu MTU akakushauri vibaya ilhali anajua wewe ni Mwema.

Haya unashauriwa vibaya alafu unatenda Ule ushauri Mbaya. Alafu wasingiziwe washauri. Huo ni Uongo.
Kikawaida mtu hujaribiwa Kwa tamaa, matamanio yake. Ubaya wa mtu upo ndani ya MTU na ndio unaojaribiwa. Ubaya siku zote hautoki nje kwenda ndani ya MTU. Bali unatoka ndani ya mtu kwenda nje.
Nazungumzia Kwa Watu wazima.

Uovu au uhalifu mara nyingi haunaga kisingizio. Kama ulivyo Wema nao hauna kisingizio.

Ukiona jitu ni jizi, fisadi, jambazi, Muuaji, mbakaji, na dhambi zingine jua Yale ayafanyayo yanatoka ndani yake na hakuna sababu ya nje inayoweza mfanya MTU kuwa Mtu Mbaya.

Ukiona MTU ni Malaya anafanya ukahaba ili ajipatie fedha, umaskini anaosema ndio Sababu, huo ni Uongo. Ila yeye ndani yake ndio Yuko hivyo. Narurudia, ubaya wa mtu upo ndani yake na kamwe ubaya hautoki nje. Vinavyotokaje ni vichocheo tuu.

Hata hivyo, Mtu huweza kudanganywa na kupotoshwa kuhusu Jambo Fulani. Lakini mpotoshaji, na anayepotoshwa wote wanakuwa katika nafasi Sawa pale watendapo Kosa Hilo. Tena mtendaji anakuwa ndiye mkosaji Square.

Chagua Watu waadilifu, Wema na wapenda HAKI.

Robert Heriel
Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
 
Ma Rais dunia nzima wanategemea ushauri....hakunaga kitu kama Rais mwenye akili...na Rais asie na akili..

Akili ya ma Rais wote hutegemea advisors ndo maana wenzetu wameenda mbali Sana na kuweka washauri rasmi wa Rais Kwa kila kitu...kuanzia siasa Hadi Uchumi...washauri wanatangazwa wanajulikana na CV zao zimeshiba

Wamarekani wameenda mbali zaidi
Mfano kuna mshauri wa uchumi anaelipwa wa Rais. Halafu kuna mshauri wa uchumi anaelipwa wa Makamu wa Rais ...halafu kuna waziri WA fedha na yeye ana mshauri wa uchumi anaelipwa wa waziri WA fedha...bado kuna washauri Tele wa wizara wanalipwa, the list goes on..


So Kwa Wamarekani likija suala la uchumi mezani Kwa Rais ...unakuta kuna PhD kama 10 hivi zimechangia Hilo wazo.....na mapendekezo.

You are only smart if you surround yourself with people who are more smarter than you
 
Ma Rais dunia nzima wanategemea ushauri....hakunaga kitu kama Rais mwenye akili...na Rais asie na akili..

Akili ya ma Rais wote hutegemea advisors....ndo maana wenzetu wameenda mbali Sana na kuweka washauri rasmi wa Rais Kwa kila kitu...kuanzia siasa Hadi Uchumi...washauri wanatangazwa wanajulikana na CV zao zimeshiba

Wamarekani wameenda mbali zaidi
Mfano kuna mshauri wa uchumi anaelipwa wa Rais. Halafu kuna mshauri wa uchumi anaelipwa wa Makamu wa Rais ...halafu kuna waziri WA fedha na yeye ana mshauri wa uchumi anaelipwa wa waziri WA fedha...bado kuna washauri Tele wa wizara wanalipwa....the list goes on..


So Kwa Wamarekani likija suala la uchumi mezani Kwa Rais ...unakuta kuna PhD kama 10 hivi zimechangia Hilo wazo.....na mapendekezo....

You are only smart if you surround yourself with people who are more smarter than you

Kuwa na Washauri ni kawaida. Lakini washauri wanaokupotosha na ukafanya hapo ndipo mada yangu ilipo.
 
What makes you so sure wanampotosha...
Mkapa alilaumiwa ana potoshwa kumbe alikuwa sahihi .

Matokeo ndio kipimo cha kukosea na kupatia.

Ninachojaribu kueleza ni kuwa, Ikiwa Rais tafanya Jambo Baya aliloshauriwa, basi naye ni mhusika namba moja ambaye lawama zote zitakuwa juu yake.
Kumnasua Rais kwenye kazi yake kisa alishauriwa hapo ndipo Mimi naona ni unafiki, woga au namna Fulani hivi ya kupindisha mambo.

Ndio maana nikasema wanaosema Rais anashauriwa vibaya wanakosea, kama MTU anakosea Sema amekosea. Kwani aliyewateua hao washauri ni Nani?
 
Matokeo ndio kipimo cha kukosea na kupatia.

Ninachojaribu kueleza ni kuwa, Ikiwa Rais tafanya Jambo Baya aliloshauriwa, basi naye ni mhusika namba moja ambaye lawama zote zitakuwa juu yake.
Kumnasua Rais kwenye kazi yake kisa alishauriwa hapo ndipo Mimi naona ni unafiki, woga au namna Fulani hivi ya kupindisha mambo.

Ndio maana nikasema wanaosema Rais anashauriwa vibaya wanakosea, kama MTU anakosea Sema amekosea. Kwani aliyewateua hao washauri ni Nani?
Mbona Nyerere alishauriwa vibaya kuhusu vijiji vya jamaa na watu wakafa na hatukusema Nyerere Hana akili??
 
Hilo mimi nimeshalisema siku nyingi sana.

Nimeshahoji kuwa kwani Rais yeye hana akili zake mwenyewe?

Rais hana discernment?

Rais haulizi maswali? Yote anayoshauriwa yeye anayakubali tu?

Kama tuna Rais wa hivyo basi huyo hafai kabisa.

Hatuhitaji kuwa na Rais zumbukuku asiye na akili.
 
Mbona Nyerere alishauriwa vibaya kuhusu vijiji vya jamaa na watu wakafa na hatukusema Nyerere Hana akili??

Kwa nini unamtaja Nyerere?
Nimesema Rais, anaweza kuwa yeyote tuu.

MTU yeyote anaweza asiwe na Akili katika Jambo Fulani.

Kuhusu kusema au kukaa kimya; kusema au kutokusema haibadilishi chochote kwenye Jambo lililokwisha kutokea. Kama alifanya ujinga haitabadilika hata Watu wakikaa kimya. Halikadhalika na upande wa pili
 
Kwa nini unamtaja Nyerere?
Nimesema Rais, anaweza kuwa yeyote tuu.

MTU yeyote anaweza asiwe na Akili katika Jambo Fulani.

Kuhusu kusema au kukaa kimya; kusema au kutokusema haibadilishi chochote kwenye Jambo lililokwisha kutokea. Kama alifanya ujinga haitabadilika hata Watu wakikaa kimya. Halikadhalika na upande wa pili
Hutaki Nyerere atajwe?🤣🤣🤣🤣
 
Hilo mimi nimeshalisema siku nyingi sana.

Nimeshahoji kuwa kwani Rais yeye hana akili zake mwenyewe?

Rais hana discernment?

Rais haulizi maswali? Yote anayoshauriwa yeye anayakubali tu?

Kama tuna Rais wa hivyo basi huyo hafai kabisa.

Hatuhitaji kuwa na Rais zumbukuku asiye na akili.

Tatizo la Sisi wabongo tunapenda kuwanasua Watu Fulani kinafiki nafiki kisa Cheo, Pesa au mamlaka.
Mfano, mchungaji akiwa anahubiri ukasema anachohubiri hakiendani na akifanyacho, wabongo watakuambia; fanya akisemacho na sio atendacho.
Lakini akifanya mwingine labda ni muumini inakuwa Zoho.
 
Kwema Wakuu!

Hakuna Jambo ambalo linanikera kama kumsikia MTU akisema Rais anashauriwa vibaya na washauri wake. Watu wengi wanaosema hivyo ni Watu wasioweza kueleza mambo bayana. Ni Watu wakupindisha pindisha maneno. Wasioweza kutamka nyeusi ni nyeusi na nyeupe ni nyeupe.

Taikon wa Fasihi
Kwa sasa Dar es salaam
Kama hautakubali kuwa rais anashauriwa vibaya, basi msimamo wako ni kwamba kwa yanayoendelea haya, ni moja kwa moja kuwa hana akili na ungependa ibaki na itamkwe hivyo.
 
Naunga mkono hoja kuna mambo yako sensitive sana ambayo hata ukishauriwa lazima na ww uchekeche...

Nafasi ya uraisi sio mchezo...huezi kushauriwa tu ukafanya tuu bila na ww kuweka akili yako hapo....

The boss soma kitabu cha trump kinaitwa vipers...uone jinsi trump alivyokua anasumbuana na washauri wake...yaani mwisho wa siku maamuzi yanakua yake
 
Kwema Wakuu!

Hakuna Jambo ambalo linanikera kama kumsikia MTU akisema Rais anashauriwa vibaya na washauri wake. Watu wengi wanaosema hivyo ni Watu wasioweza kueleza mambo bayana. Ni Watu wakupindisha pindisha maneno. Wasioweza kutamka nyeusi ni nyeusi na nyeupe ni nyeupe.


Kwa sasa Dar es salaam


Hata wewe ukiwa Engineer au na CPA kama mhasibu ukienda Hospital huwa unashauriwa na unakaa kimya.

Kila mtu ni Mpumbavu eneo ambalo hana specialization nalo, hakuna mwanadamu, hata Clinto asiyeshauriwa.
 
Back
Top Bottom