Habari ya uzima wanajamii forum Kwanza natanguliza shukrani kwa ushauri wowote ntakaopata kutoka kwenu naomba niulize ukinunua nyumba au kiwanja Cha mirathi ni documents gani za msingi za kupatiwa Kama mnunuaji wa nyumba/kiwanja Cha mirathi hiyo.
Nimetanguliza swali hili kutokana na story yangu nilinunua nyumba Kama miezi 6 nyuma nikaandikisha mauziano serikali za mitaa na muuzaji akaniambia yeye ndio msimamizi wa mirathi akanipatia fomu namba nne ya mahakamà na mukhtasari wa kikao cha wanafamilia kumchagua yeye ndio msimamizi wa mirathi.
Nikauliza kwa majirani pamoja na serikali za mitaa wakaniambia kweli hapo niliponunua ni kwa baba yake na yeye ndio mrithi halali na msimamizi wa mirathi. Baada ya kununua nyumba tu miezi kupita wakaja baadhi ya ndugu nakusema kwamba msimamizi wa mirathi hawakuhusishwa kwenye mauziano hayo.
Nikajaribu kumtafuta Yule aloniuzia akaniambia hao sio ndugu zake hawausiki na nyumba hiyo Mimi nikajaribu kurudi Tena kwa majirani kuuliza waloniambia hapo mahala hapana shuda wanasema kuwa wale watoto walokuja kuwepo kwenye mauziano yako walikua ni wa mama mwengine ambao wanashare mama na muuzaji lakini Hawa walokuja ni wa baba moja pamoja na muuzaji sema wanugomvi wa familia. Ndio maana wakauza na sehemu hiyo watoto walokuja kulalamika na wao wanausika na mirathi.
Mbaya zaidi ukipata shida ndio majirani wanaibuka wakaniambia na hapo ulipouziwa kwa mbele Kuna Barabara inapita na watu walishalipwa ikiwemo na nyumba yangu nilionunua nusu ya nyumba inamegwa na kiwanja chote Cha mbele ya nyumba.
Naomba msaada wenu ni hatua gani za kisheria nichukue na documents gani ambazo niwenazo au nizidai kwa muuzaji wa nyumba nashukuru.
Nimetanguliza swali hili kutokana na story yangu nilinunua nyumba Kama miezi 6 nyuma nikaandikisha mauziano serikali za mitaa na muuzaji akaniambia yeye ndio msimamizi wa mirathi akanipatia fomu namba nne ya mahakamà na mukhtasari wa kikao cha wanafamilia kumchagua yeye ndio msimamizi wa mirathi.
Nikauliza kwa majirani pamoja na serikali za mitaa wakaniambia kweli hapo niliponunua ni kwa baba yake na yeye ndio mrithi halali na msimamizi wa mirathi. Baada ya kununua nyumba tu miezi kupita wakaja baadhi ya ndugu nakusema kwamba msimamizi wa mirathi hawakuhusishwa kwenye mauziano hayo.
Nikajaribu kumtafuta Yule aloniuzia akaniambia hao sio ndugu zake hawausiki na nyumba hiyo Mimi nikajaribu kurudi Tena kwa majirani kuuliza waloniambia hapo mahala hapana shuda wanasema kuwa wale watoto walokuja kuwepo kwenye mauziano yako walikua ni wa mama mwengine ambao wanashare mama na muuzaji lakini Hawa walokuja ni wa baba moja pamoja na muuzaji sema wanugomvi wa familia. Ndio maana wakauza na sehemu hiyo watoto walokuja kulalamika na wao wanausika na mirathi.
Mbaya zaidi ukipata shida ndio majirani wanaibuka wakaniambia na hapo ulipouziwa kwa mbele Kuna Barabara inapita na watu walishalipwa ikiwemo na nyumba yangu nilionunua nusu ya nyumba inamegwa na kiwanja chote Cha mbele ya nyumba.
Naomba msaada wenu ni hatua gani za kisheria nichukue na documents gani ambazo niwenazo au nizidai kwa muuzaji wa nyumba nashukuru.