Thecoder njoo kwenye huu uzi kaka
Andiko kubwa sana hilo mkuu😅😅 na kwakifupi kwa hizi akili zetu za past hatuwezi solve hiyo puzzle.
Akili yetu inaamini kwenye references zaidi so hii inafanya wasomi wengi washindwe kujifunza vitu vipya, kwamfano tafiti nyingi huwa zimekaa zaidi kwenye kurelate na past kisha kutoa conclusion so inapotokea kitu kipya hakuna ambae atakitolea conclusion badala yake wataendelea kukifuatilia huku wakiwa wanaendelea kurelate na tabia ya kitu au vitu fulani fulani ambavyo vilikuwepo hapo past.
Kwahiyo hata procedure ambazo hufanyika kwenye uchunguzi wa vitu vingi ni history ambayo ilikua proved kwa asilimia fulani katika kutoa matokeo chanya ya jambo hilo, so jambo likiwa ni jipya na halina historia yoyote ya kuwahi kuwepo duniani hakuna akili ya kawaida ya mtu yeyote duniani itakayoweza kulitolea ufumbuzi.
Kwahiyo ujanja wetu wote inategemea kale na pasipo na kale hakuna chochote ambacho kinaweza kufanyika na mwanadamu.
Kale hutumika ili kuitabiri future but universe ikibadili tabia zake kidogo watu wote duniani wataanza kulalamika... Chukulia mfano wakulima walivyokariri majira ya Kila mwaka, so wanaenda shamba kwa kufuata ratiba zile zile ila ikitokea universe ikabadilika kidogo au ikakataa kutabirika kwa angalau miaka mitano tu, wote mtakufa njaa😂😂😂.
Listen, kitendo cha kushindwa kuvuta na kutoa hewa wote tunaamini kwamba ni kifo kwakua historia tuliyoikuta imetuamunisha hivyo, na haujawahi kuwa na historia ya tofauti na hapo lakini what if hii historia iko wrong na haikufanyiwa utafiti wowote?...
Unajua wanyama wakali na ambao sio wakali kwa experience ya past ambayo kuna watu wameipata kwa maumivu makali na wakaamua kurithisha historia hiyo kizazi na kizazi.
Mtoto anavyokua huwa anajaribu kila kitu kwakua Hana experience na chochote na hapo watu wanasema bado Hana akili ndio maana anafanya hivyo, lakini kadri anavyokua anapata uzoefu kwa kujifunza kwa maumivu au kuhadithiwa na wale waliomtangulia nae ndio anatofautisha kipi ni kipi... So everything in your brain ni history and once ukaja na kitu kipya kabisa ambacho hakijawahi kuwepo duniani na ukashindwa kuprove basi wasomi wote watakuona wewe ni mwehu, so hakuna namna mnaweza kuyajua mambo hayo kwa akili hizi za past.
Na the bad thing ni kwamba ili universe ikucontrol vizuri ikakuwekea mipaka miwili sayansi na dini.
Sayansi inataka uamini kitu kwa kuthibitisha na kale while dini inakutaka ubaki kwenye upast wako na wala usianze kuacha ubongo wako uelee kwenye hoja nzito za future😅😅😅 mnajikuta mpo mpo tu na ulimwengu unaendelea kuwaamulia Kila kitu mnachotakiwa kufanya na hata mnavyotakiwa kuishi over and over again.