Kuna nini kati ya Mwigulu na Zitto?

Kuna nini kati ya Mwigulu na Zitto?

Leo nimecheka sana .Duh!

Sehemu na namna ambavyo huwa unatokea kwenye uzi zinazomtaja Zitto, zinatia shaka sana broo wangu!

Usiangaike na HISIA zetu maana kesho zinaweza kukugeuka, hangaika na AKILI zetu maana humo ndimo msingi bora wa Ukombozi unapopaswa kusimikwa! Tusiiache Tz na Wanawaafrika wake ikatopea katika tope la giza!
Anaita sasa!
 
Katibu Mkuu wa magwanda Dr.W.Slaa aka babu, hampati Zitto kwa lolote, Zitto ni kijana, mwerevu, mchapa kazi, msomi, kwa juhudi zake pekee aliinyanyua chadema aka kadima na kuifikisha hapo ilipo.

Zitto hatujamuona wala kumsikia akifanya kazi za unaibu katibu mkuu wa chadema, sio saizi yake, huyo ni zaidi ya Katibu Mkuu na Mwenyekiti wa chadema kwa pamoja.

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.
Wewe tatizo lako mdini
 
Mkuu, wewe ndiyo unaanza kuhama kutoka kwenye hoja yako ambayo ilikuwa inahusu viongozi wawili ndani ya vyama viwili katika mitazamo hasa ya wapenzi, wafuasi na wanachama katika vyama na hasa CHADEMA.

Hoja yangu nimeijenga katika mzunguko wa hawa viongozi ndani ya vyama vyao na siyo kati ya vyama na vyama.

Nimemwelezea Mh. Zitto na mtazamo wa siasa zake ndani ya CHADEMA na mtazamo wake kwa Mh. Mwigulu na pia nimemwelezea Mh. Mwigulu ndani ya mtazamo wa wanaCHADEMA.

Sitaki kutoka nje ya mada yako lakini nitakueleza hivi, CCM kiuhalisia hawakutaka siasa za vyama vingi lakini external pressure ziliwalazimisha kuyaoga maji ya siasa za vyama vingi, na kwa sababu hiyo, waliingia kwenye mapambano na siasa za isolationism wakidhani wao ndiyo 'number one'. Kama tunavyofahamu, hizi siasa mara nyingi huzaa ubinafsi na uhasama.

Hata pale vyama vingine vilipoingia kwenye ulingo wa kisiasa, ilibidi wakabiliane na hizi siasa za CCM, kitu ambacho kilisababisha uhasama mkubwa wa kisiasa nchini ambapo kwa kiwango fulani mpaka sasa bado unaendelea. Hizi siasa ni zaidi ya partisan politics.

Yes, CCM ndiyo waasisi nchini wa siasa za isolationism kwa kudhani kuwa wao ni bora zaidi.

Mkuu mda hii nimeianzisha mwenye,na wala siwezi kutoka nje ya mada hata kidogo na ndiyo maana kuna wale walijaribu kunitoa nje ya mda nimeenda nao sawa...

jibu la swali langu ushanipa,naona tuishie hapo tu "Yes, CCM ndiyo waasisi nchini wa siasa za isolationism kwa kudhani kuwa wao ni bora zaidi"
 
masanjasb

Hii post ina jibu sahihi la swali lako kwa undani kabisa. Mkuu Ng´wamapalala Kwa post hii amefunga mjadala.

Nakuomba masanjasb uiweke hii post ya Ng´amapalala kama update au clarification hapo juu kwenye threa post tafadhali.

Asante sana.

mkuu ZeMarcopolo kwa hyo tuzuie watu wasiendelee kuchangia uzi kwa vile msukuma huyu Ng'wamapalala kakuridhisha na majibu yake?
 
Katika siasa za Tanzania kuna accomodative politician and isolationist politician.

Mh. Zitto Kabwe anaendesha siasa zake kwa misingi ya accomadative politics kwa maana kuwa, siasa zake zina nafasi ya masikilizano na pia makubaliano na makundi mengine yaliyoko ndani na nje ya chama chake.

Tatizo lililopo hapa ni baadhi ya wanaCHADEMA wamejengwa kisiasa katika misingi ya isolationist politics kiasi cha kujenga fikra na mitazamo ya kihasama kati ya wao kwa wao au kati yao na vyama vingine vya kisiasa. Sababu kuu ni hii fikra ya kudhani wao ni bora kuliko wengine, na ili ufanikiwe lazima uwe mmoja wao. Huu ni aina fulani ya ubinafsi wa kisiasa ambao unasababisha kutumia njia zozote zile katika kufanikisha malengo yake.

Hili kundi ndani ya CHADEMA ambalo siasa zake ndizo zinazofanywa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, ukichunguza kwa undani utagundua kuwa ndilo ambalo linamuona Mh. Zitto kama siyo active kwenye siasa zao.

Mh. Mwigulu yeye siasa zake niza mlengo wa isolationism kama lilivyo kundi ndani ya CHADEMA linalomuona Mh. Zitto siyo active kwenye siasa zao.

Kwa kawaida, kundi lenye mlengo wa siasa za isolationist huwa halipikiki kwenye chungu kimoja na kundi jingine lenye mlengo kama huo. Ndiyo maana Mh. Mwigulu ni sumu kwenye hili kundi ndani ya CHADEMA lakini kwa vile Mh. Zitto ni accomodative politician, siyo ajabu kumuona kwenye maelewano na makundi mengine pamoja na kwamba isolationist wanakuwa hawana imani naye 100%.

Accomodative politicians wengine ninaowaona kwenye uongozi wa juu ndani ya CHADEMA ni kama Mh. Mbowe, Mh. Mnyika, Said Arfi...
Ng'wamapalala

Naamini wewe si mgeni au mtoto kiasi kutokujua ya kwamba:-

1. Siasa za accomadative politics zilishashindwa na NCCR, TLP, CUF na daima kwa Siasa za MACCM zilivyo haitakaa kamwe hii style kufanikiw akuiondoa CCM madarakani.

2. Hili la kusema kuna chuki zidi ya Zitto ni prppaganda zilezile za siku zote na hata yeye mwenyewe zitto amekuwa akisema kila siku haya kuwa wanapandikizwa chuki bila sababu na ni kuwachonganisha tu wana-CHADEMA ili wafarakane na MACCM yaendelee kupeta.

Na hata hizi porojo za leo zimeanzia kwenye ziara inayoendelea huko kanda ya Magharibi ambayo kiukwlei ni kitu kilichotangazwa siku nyingi sana na kimeandaliw asiku nyingi na sio kitu cha kuzuka, watuw ankuja wanahoji kw anini ZITTO yupo peke yake, mnajibiw akuwa sababu ni kuwa hiyo ni mikutano ya KIKANDA haitaji viongozi w akitaifa kuwepo na hata Kanda zingine zinaendesha hiyo mikutano kila siku.

Pia kama ingekuw ani kuhoji watu wangehoji wapi ARFI ambaye ni mbunge wa Kanda hiyo lakini mleta mada hawezi hoji hilo kw akuwa alisha panga mambo yake pamoja na kutengwa pia atumie KETE ya UDINI sasa nashindwa kwa kuwa ARFI na ZITTO ni DINI moja anakosa hoja za kulalamika.

Pia ilizuka hoja ya kuwa mbona ZITTO hana ELIKOPTA wakati ipo wazi kuw ahiyo ni mikutano ya Kanda na nilion aPicha FB akiwa na GARI la M4C na sio gari lake binafsi, sasa sijuhi walikuwa wanataka nini.

CONCLUSION:
narudia tena 2015 WAISLAM wenzangu mataaumbuka pale MACCM watakapo msimamisha MKATOLIKO LOWASSA na CHADEMA watakapo Msimamisha ZITTO from now where na hili Pasco alisha lizungumzia sana hapa
kuwa TURUFU ya CHADEMA ni ZITTO na naaminio CHADEMA ni wenye akili na kujingamua na siku ya siku ZITTO atapeperusha bendera ya CHADEMA ya URAISI sijuhi BAKWATA watakuw aupande gani.
1383296_516132815137913_1226329488_n.jpg
1383293_516132798471248_579254229_n.jpg
1383173_516132811804580_928914905_n.jpg
1385136_516132725137922_26454949_n.jpg
 
Last edited by a moderator:
Katibu Mkuu wa magwanda Dr.W.Slaa aka babu, hampati Zitto kwa lolote, Zitto ni kijana, mwerevu, mchapa kazi, msomi, kwa juhudi zake pekee aliinyanyua chadema aka kadima na kuifikisha hapo ilipo.

Zitto hatujamuona wala kumsikia akifanya kazi za unaibu katibu mkuu wa chadema, sio saizi yake, huyo ni zaidi ya Katibu Mkuu na Mwenyekiti wa chadema kwa pamoja.

Mnyonge mnyongeni haki yake mpeni.

Mpaka kumwita Dr. Slaa babu bila shaka ni baba wa mama au baba yako. Sasa ni kwa nini unamdhamdhalilisha mzazi wa wazazi wako? Ina mana Nape akiwaambia mchojoe hadharani mtafanya hivyo? Acha uzandiki, uzushi, unafiki na uongo. Kama unamtaka Zitto mweleze acha kubwabwaja.
 
uongo mwingine mtanyongwa slaa alikuwa wa tatu utasemaje alifanya vizuri.

Join Date : 8th October 2013
Posts : 19
Rep Power : 304
Likes Received0
Likes Given1



Hilo ni tatizo la kuvamia jukwaa nafikiri ungejijenga kwanza kusoma wanavyo andika wenzio ndio na wewe uanze kuchangia. hiyo Takwimu ya Kuwa Dr. Slaa alikuwa wa 3 umeipata wapi au ni Kura mlizopiga wewe na familia yako?
 
Sehemu na namna ambavyo huwa unatokea kwenye uzi zinazomtaja Zitto, zinatia shaka sana broo wangu!

Usiangaike na HISIA zetu maana kesho zinaweza kukugeuka, hangaika na AKILI zetu maana humo ndimo msingi bora wa Ukombozi unapopaswa kusimikwa! Tusiiache Tz na Wanawaafrika wake ikatopea katika tope la giza!
Anaita sasa!

Nimekosea wapi?Ninatokeaje?
 
Hivi kofia imeandikwa nini?

attachment.php

Uzinduzi wa Kanda na M4C kipi kilianza? Kwa nini ZITTO Kabwe anafanya mikutano peke yake tofauti na desturi ya M4C ya makamanda wengi kuongozana? Kwenye picha mikutano ya ZITTO sioni nembo za M4C.
 
Ng'wamapalala

Naamini wewe si mgeni au mtoto kiasi kutokujua ya kwamba:-

1. Siasa za accomadative politics zilishashindwa na NCCR, TLP, CUF na daima kwa Siasa za MACCM zilivyo haitakaa kamwe hii style kufanikiw akuiondoa CCM madarakani.

2. Hili la kusema kuna chuki zidi ya Zitto ni prppaganda zilezile za siku zote na hata yeye mwenyewe zitto amekuwa akisema kila siku haya kuwa wanapandikizwa chuki bila sababu na ni kuwachonganisha tu wana-CHADEMA ili wafarakane na MACCM yaendelee kupeta.

Na hata hizi porojo za leo zimeanzia kwenye ziara inayoendelea huko kanda ya Magharibi ambayo kiukwlei ni kitu kilichotangazwa siku nyingi sana na kimeandaliw asiku nyingi na sio kitu cha kuzuka, watuw ankuja wanahoji kw anini ZITTO yupo peke yake, mnajibiw akuwa sababu ni kuwa hiyo ni mikutano ya KIKANDA haitaji viongozi w akitaifa kuwepo na hata Kanda zingine zinaendesha hiyo mikutano kila siku.

Pia kama ingekuw ani kuhoji watu wangehoji wapi ARFI ambaye ni mbunge wa Kanda hiyo lakini mleta mada hawezi hoji hilo kw akuwa alisha panga mambo yake pamoja na kutengwa pia atumie KETE ya UDINI sasa nashindwa kwa kuwa ARFI na ZITTO ni DINI moja anakosa hoja za kulalamika.

Pia ilizuka hoja ya kuwa mbona ZITTO hana ELIKOPTA wakati ipo wazi kuw ahiyo ni mikutano ya Kanda na nilion aPicha FB akiwa na GARI la M4C na sio gari lake binafsi, sasa sijuhi walikuwa wanataka nini.

CONCLUSION:
narudia tena 2015 WAISLAM wenzangu mataaumbuka pale MACCM watakapo msimamisha MKATOLIKO LOWASSA na CHADEMA watakapo Msimamisha ZITTO from now where na hili Pasco alisha lizungumzia sana hapa
kuwa TURUFU ya CHADEMA ni ZITTO na naaminio CHADEMA ni wenye akili na kujingamua na siku ya siku ZITTO atapeperusha bendera ya CHADEMA ya URAISI sijuhi BAKWATA watakuw aupande gani.
1383296_516132815137913_1226329488_n.jpg
1383293_516132798471248_579254229_n.jpg
1383173_516132811804580_928914905_n.jpg
1385136_516132725137922_26454949_n.jpg
"Pia kama ingekuw ani kuhoji watu wangehoji wapi ARFI ambaye ni mbunge wa Kanda hiyo lakini mleta mada hawezi hoji hilo kw akuwa alisha panga mambo yake pamoja na kutengwa pia atumie KETE ya UDINI sasa nashindwa kwa kuwa ARFI na ZITTO ni DINI moja anakosa hoja za kulalamika"

Lengo la uzi huu haikuwa kuhoji zito yu wapi nanafanya nini wala kulalamikia zira zake? ulitakiwa usome Uzi unaongelea nini sio kusema tu eti tungehoji ARFI aliko?

kuna mtu humu aliuza why zito yupo tabora na sio arusha or kilimanjaro,na mie nikajibu kuwa aliko zito ni kanda yake kwa hyo lazima mda wote awe active kuhakikisha kuna uhai wa chama kwenye kanda hyo,nways jiridhishe tena kwa kusoma mada ili uje uchangie mda sasa
 
Huwezi kujifunza siasa nzuri bila kumwangalia zito z kabwe na pia vijana wa ccm nao siasa zao zina mkono mkubwa wa mh mwigulu, kufikia hatua yakuandika uzi kama huu nimefatilia mda sana siasa za hawa watu, na kwa nini zito awe kimya wakati chama kinaumizwa au viongozi wake wanashambuliwa?
Tatizo lipo and we need to fix it kabla ya 2015

Uzuri ni kwamba ndugu Zitto na Mwiguru wote wamo humu,usijali watatoa ufafanuzi,
 
Last edited by a moderator:
Zito na Mwiguru WANa hoja nzito za nchi wabishanie nini lengo ni kuona nchi ikisonga mbele
 
Siku zote zitto huwananga viongozi wa serikali na sio wa vyama! Anapomnanga mtu huwa analenga direct utendaji wake na athari yake moja kwa moja kwa wananchi! Ukinangana na mwigulu wote mnakuwa hamna malengo zaidi mtadhalilishana tu. Zitto yuko makini

Nakubaliana nawe kabisa. Mwigulu ni kama kichaa aliyeiba nguo za mtu anayeoga. Ukimkimbiza watu watakuita kichaa kumbe kichaa mwenyewe ndiye aliyeiba nguo.

Zito yuko makini na katika hilo sina wasiwasi naye. Ni kweli kuwa zito hugusa mtu anayejulikana na yale yanayofanyika yanaonekana wazi. Mwigulu hana chochote anachokifanya kinachoweza kuonekana kwa wananchi wa kawaida. Kumtunishia misuli Mwigulu ni sawa na kupoteza nguvu zako kwenye upepo unaopita tu.
 
Hivi Mwigulu naye ni mwanasiasa wakulinganishwa na wanasiasa nchini? Yani kwenye hii thread mmekosa mtu wakumlinganisha na Zitto? Wanasiasa wa ccm vijana ni hasara kabisa kwa taifa, afadhalia wale wazee kina Sumaye, Lowassa, Kikwete nk, wakiongea kitu i can take my time to listen, siyo Mwigulu, Nape, nani huyu mwingine anaitwa Kingwagalla. They are just rubbish, wanaongega tu from heresay!

Zitto anajulikana, bado utoto unamsumbuwa, kadiri siku zinavyokwenda anazidi kuwa mwanaharakati zaidi kuliko mwanasiasa, inabidi ajiunge na jumuiya ya wafanyakazi kudai haki, kama wanasiasa wakijapan.
 
Ukiona unashambuliwa na Timu ya Lumumba ujue wewe ndiye unayefaa kuongoza harakati za kweli za kuwang'oa.

Kamwe CCM wasitarajie CHADEMA kita-loose focus.

Adui wa CCM ni rafiki yetu na tutasimama nae hadi tone la mwisho tukiendelea kuimarisha misingi ya kitaasisi itakayozalisha maadui wengi zaidi wa CCM na mfumo wa kidhalimu
Kumbeeee hii ni kwa cdm pekee au hata ccm ?
 
Wana janvi nichukue fursa hii kuwapongeza wote kwa kushiriki kwenye mjadala huu bila kutoa lugha chafu,leo mmekuwa wastaarabu sana,japo kuna changamoto za uccm na ucdm ila tumevuka siku bila kutukanana,ukipata mda soma kila alichochangia mwenzako kwenye uzi huu na jibu la swali langu kuu lipo ndani ya majibu ya watu wSalioshiriki kwenye topic hii:
..
Kuna ukweli kidogo, ingawa tumewaona pro CCM wakimjumuisha na wakimdhih
aki Dr
Slaa ili kufunua chuki zao kwake.
 
hilo swali nilikuachia wewe mkuu,kama una majibu yake pia tuwekee ila kwa pande zote mbili,kama zitto anapendwa na watanzania wengi wakiwemo wabunge wa ccm na vyama vingine je na mwigulu nae anapendwa na watanzani wengi wekimo wabunge wa upinzani na vyama vyao????

Zitto anafanya siasa za zinazoruhusu akili yake kukaa hata na yule adui wakakubaliana na kupingana katika baadhi(agree to disagree) ila viongozi wengine wa chadema siasa kwao ni vita.
 
Back
Top Bottom