Kuna nini kati ya Mwigulu na Zitto?

Kuna nini kati ya Mwigulu na Zitto?

Mi swali langu ni moja tu kwa nini ikiletwa hoja watetezi wa Zitto wanakuwa LB7,na ikiletwa hoja ya Dr.Slaa hata kama ya kujenga vipi.matusi mwanzo mwisho.ushahidi tosha ni siku Mwigulu aliposema Star Tv mbele ya Zitto kuwa ana mkanda wa cdm,ajabu naibu katibu mk8 ni kama hakusikia.Kwa nini nisiamini alimuunga mkono kwa kukaa kimya
 
Magamba wanajua walivyochakachuwa kura za Dr. Slaa wakiwatumia Usalama w Taifa.
Hata kwenye vikao vyao huwa wanajadili kwamba bila kazi kubwa ta kuchakachuwa CHADEMA wangechikuwa nchi.

MwanaHALISI waliandika kila kitu; nadhani ni mojawapo ya sababu kubwa ya kulifungia hilo gazeti makini.
 
Katika siasa za Tanzania kuna accomodative politician and isolationist politician.

Mh. Zitto Kabwe anaendesha siasa zake kwa misingi ya accomadative politics kwa maana kuwa, siasa zake zina nafasi ya masikilizano na pia makubaliano na makundi mengine yaliyoko ndani na nje ya chama chake.

Tatizo lililopo hapa ni baadhi ya wanaCHADEMA wamejengwa kisiasa katika misingi ya isolationist politics kiasi cha kujenga fikra na mitazamo ya kihasama kati ya wao kwa wao au kati yao na vyama vingine vya kisiasa. Sababu kuu ni hii fikra ya kudhani wao ni bora kuliko wengine, na ili ufanikiwe lazima uwe mmoja wao. Huu ni aina fulani ya ubinafsi wa kisiasa ambao unasababisha kutumia njia zozote zile katika kufanikisha malengo yake.

Hili kundi ndani ya CHADEMA ambalo siasa zake ndizo zinazofanywa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, ukichunguza kwa undani utagundua kuwa ndilo ambalo linamuona Mh. Zitto kama siyo active kwenye siasa zao.

Mh. Mwigulu yeye siasa zake niza mlengo wa isolationism kama lilivyo kundi ndani ya CHADEMA linalomuona Mh. Zitto siyo active kwenye siasa zao.

Kwa kawaida, kundi lenye mlengo wa siasa za isolationist huwa halipikiki kwenye chungu kimoja na kundi jingine lenye mlengo kama huo. Ndiyo maana Mh. Mwigulu ni sumu kwenye hili kundi ndani ya CHADEMA lakini kwa vile Mh. Zitto ni accomodative politician, siyo ajabu kumuona kwenye maelewano na makundi mengine pamoja na kwamba isolationist wanakuwa hawana imani naye 100%.

Accomodative politicians wengine ninaowaona kwenye uongozi wa juu ndani ya CHADEMA ni kama Mh. Mbowe, Mh. Mnyika, Said Arfi...
 
Nilipofika hapo kwenye red nimekuona wewe ni mzushi na mzandiki, na unaandika kitu ambacho huna data wala information. Zitto alikuwepo kwenye hicho kipindi, na video yake ilishakuwa uploaded humu JF mara kadhaa...

Unapata faida gani kuandika habari za uongo?...

jamaa kapotosha,Zitto alikuwepo ila tukumbushe alifanya nini dhidi ya propaganda chafu za Mwigulu,tena zikisemwa mbele yake?
 
zito na mwigulu wote ni wanasiasa wa hoja siyo porojo wewe unataka wakosoane hata kama hakuna sababu we vipi.

hizo siasa chafu za kuua watu,kujeruhi raia wasio na hatia nazo unaziita siasa? au una mahaba tu na huyo gaidi? kuhusu inshu ya zitto na mchembe hakuna lolote ila kwa akili za savimbi anadhani kuna siku watamtumia zitto ili kuidhofisha cdm,hivyo hawataki kumuudhi ili wajifanye wanamkubali kumbe wizi mtupu!.kuhusu kumwandama sana dr kwa kuzusha maneno ya kipuuz ni akili yake tu ndogo kudhani dr slaa ndo cdm,anasahau kuwa cdm kipo ndani ya watz mamilion tena wenye mapenz na misimamo thabiti isiyoweza kuyumbishwa na vijipropaganda vya kitoto wanavyofanya mchembe na wale LB7.
 
Katika siasa za Tanzania kuna accommodative politician and isolationist politician.
Hakuna cha accomodative wala isolationist kwangu nauita ni uhuni (umalaya sorry) wa kisiasa,

Ni ujinga au ujuha kuwa na rafiki anayekukosakosa kukuua kwa bomu eti kwa vile una siasa za accommodation.
 
uongo mwingine mtanyongwa slaa alikuwa wa tatu utasemaje alifanya vizuri.

unaweza kutueleza kinachoifanya ccm iogope kupatikana kwa tume huru ya uchaguzi ni nn? wanajua dr alichowafanya 2010,ni kweli bila kuchakachua ccm ingekuwa imeshazikwa muda mrefu,maana sidhani kama inaweza kuwepo baada ya kushindwa kwa sababu ni chama maslahi anzia kwa m/kt taifa hadi yule wa mtaa,na wengi wenu hata hapa jf bila LB7 project tunawapoteza
 
Lakini pia mleta mada ungejiuliza zaidi kwanini mh zitto kabwe anapendwa na watanzania wengi wakiwemo wabunge wa ccm na vyama vyengine na sio Mwigulu peke yake. Zitto ana ajenda za kitaifa na sio za kichama.
hilo swali nilikuachia wewe mkuu,kama una majibu yake pia tuwekee ila kwa pande zote mbili,kama zitto anapendwa na watanzania wengi wakiwemo wabunge wa ccm na vyama vingine je na mwigulu nae anapendwa na watanzani wengi wekimo wabunge wa upinzani na vyama vyao????
 
483509_211564288987396_922908494_n-333x330.jpg


hi hi hi hi hi, hebu nicheke leo mie - hilo swali mbona easy, Zitto ni Mwanadiplomasia na Yule mwingine ni Gaidi..
 
Katika siasa za Tanzania kuna accomodative politician and isolationist politician.

Mh. Zitto Kabwe anaendesha siasa zake kwa misingi ya accomadative politics kwa maana kuwa, siasa zake zina nafasi ya masikilizano na pia makubaliano na makundi mengine yaliyoko ndani na nje ya chama chake.

Tatizo lililopo hapa ni baadhi ya wanaCHADEMA wamejengwa kisiasa katika misingi ya isolationist politics kiasi cha kujenga fikra na mitazamo ya kihasama kati ya wao kwa wao au kati yao na vyama vingine vya kisiasa. Sababu kuu ni hii fikra ya kudhani wao ni bora kuliko wengine, na ili ufanikiwe lazima uwe mmoja wao. Huu ni aina fulani ya ubinafsi wa kisiasa ambao unasababisha kutumia njia zozote zile katika kufanikisha malengo yake.

Hili kundi ndani ya CHADEMA ambalo siasa zake ndizo zinazofanywa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, ukichunguza kwa undani utagundua kuwa ndilo ambalo linamuona Mh. Zitto kama siyo active kwenye siasa zao.

Mh. Mwigulu yeye siasa zake niza mlengo wa isolationism kama lilivyo kundi ndani ya CHADEMA linalomuona Mh. Zitto siyo active kwenye siasa zao.

Kwa kawaida, kundi lenye mlengo wa siasa za isolationist huwa halipikiki kwenye chungu kimoja na kundi jingine lenye mlengo kama huo. Ndiyo maana Mh. Mwigulu ni sumu kwenye hili kundi ndani ya CHADEMA lakini kwa vile Mh. Zitto ni accomodative politician, siyo ajabu kumuona kwenye maelewano na makundi mengine pamoja na kwamba isolationist wanakuwa hawana imani naye 100%.

Accomodative politicians wengine ninaowaona kwenye uongozi wa juu ndani ya CHADEMA ni kama Mh. Mbowe, Mh. Mnyika, Said Arfi...




"Tatizo lililopo hapa ni baadhi ya wanaCHADEMA wamejengwa kisiasa katika misingi ya isolationist politics kiasi cha kujenga fikra na mitazamo ya kihasama kati ya wao kwa wao au kati yao na vyama vingine vya kisiasa. Sababu kuu ni hii fikra ya kudhani wao ni bora kuliko wengine, na ili ufanikiwe lazima uwe mmoja wao. Huu ni aina fulani ya ubinafsi wa kisiasa ambao unasababisha kutumia njia zozote zile katika kufanikisha malengo yake"

"fikra ya kuzani wao ni bora kuliko wengine" katika andiko lako nimechukua nukuu hii moja ili nikuulize swali jepesi tu.

vyama vya upinzani vina miaka 20 t0 25 lakini Tanu badaye ccm ina miaka zaidi ya 51 madarakani na bado inataka kuendelea kutawala milele na milele,kwa misingi hii ni wapi wenye fikra ya kudhani wao ni bora kuliko wengine? chadema or ccm?
 
Hakuna cha accomodative wala isolationist kwangu nauita ni uhuni (umalaya sorry) wa kisiasa,

Ni ujinga au ujuha kuwa na rafiki anayekukosakosa kukuua kwa bomu eti kwa vile una siasa za accommodation.

Mkuu, waswahili wanasema, kupanga ni kuchagua na kikubwa kabisa, siasa huwa hazina 'perfect' formula.

Mh. Zitto na Mh. Mwigulu walichagua siasa za aina hii na ndizo zimewafikisha hapo alipo na kikubwa kabisa, hawawezi kuzibadili kwa sababu kufanya hivyo ni kujizika haraka sana kisiasa.
 
483509_211564288987396_922908494_n-333x330.jpg


hi hi hi hi hi, hebu nicheke leo mie - hilo swali mbona easy, Zitto ni Mwanadiplomasia na Yule mwingine ni Gaidi..

kwa nini na yule mwingine nae asiwe Mwanadiplomasia ili tutoke kwenye siasa chafu?
 
Wana janvi nichukue fursa hii kuwapongeza wote kwa kushiriki kwenye mjadala huu bila kutoa lugha chafu,leo mmekuwa wastaarabu sana,japo kuna changamoto za uccm na ucdm ila tumevuka siku bila kutukanana,ukipata mda soma kila alichochangia mwenzako kwenye uzi huu na jibu la swali langu kuu lipo ndani ya majibu ya watu walioshiriki kwenye topic hii:



cc:kwa mods niwekeeni shkrani zangu chii ya uzi huu,shkrn kwanu
 
Nadhani Zitto na Mwigulu walishaenda kwa yule mganga aliyewalisha viapo PM7.
....Ulishawahi kuwasikia akina Juliana Shonza na Mwampamba wakimsema vibaya Zitto hata siku moja? labda kama wanataka ukoo wao wote ufe.

Leo nimecheka sana .Duh!
 
"Tatizo lililopo hapa ni baadhi ya wanaCHADEMA wamejengwa kisiasa katika misingi ya isolationist politics kiasi cha kujenga fikra na mitazamo ya kihasama kati ya wao kwa wao au kati yao na vyama vingine vya kisiasa. Sababu kuu ni hii fikra ya kudhani wao ni bora kuliko wengine, na ili ufanikiwe lazima uwe mmoja wao. Huu ni aina fulani ya ubinafsi wa kisiasa ambao unasababisha kutumia njia zozote zile katika kufanikisha malengo yake"

"fikra ya kuzani wao ni bora kuliko wengine" katika andiko lako nimechukua nukuu hii moja ili nikuulize swali jepesi tu.

vyama vya upinzani vina miaka 20 t0 25 lakini Tanu badaye ccm ina miaka zaidi ya 51 madarakani na bado inataka kuendelea kutawala milele na milele,kwa misingi hii ni wapi wenye fikra ya kudhani wao ni bora kuliko wengine? chadema or ccm?

Mkuu, wewe ndiyo unaanza kuhama kutoka kwenye hoja yako ambayo ilikuwa inahusu viongozi wawili ndani ya vyama viwili katika mitazamo hasa ya wapenzi, wafuasi na wanachama katika vyama na hasa CHADEMA.

Hoja yangu nimeijenga katika mzunguko wa hawa viongozi ndani ya vyama vyao na siyo kati ya vyama na vyama.

Nimemwelezea Mh. Zitto na mtazamo wa siasa zake ndani ya CHADEMA na mtazamo wake kwa Mh. Mwigulu na pia nimemwelezea Mh. Mwigulu ndani ya mtazamo wa wanaCHADEMA.

Sitaki kutoka nje ya mada yako lakini nitakueleza hivi, CCM kiuhalisia hawakutaka siasa za vyama vingi lakini external pressure ziliwalazimisha kuyaoga maji ya siasa za vyama vingi, na kwa sababu hiyo, waliingia kwenye mapambano na siasa za isolationism wakidhani wao ndiyo 'number one'. Kama tunavyofahamu, hizi siasa mara nyingi huzaa ubinafsi na uhasama.

Hata pale vyama vingine vilipoingia kwenye ulingo wa kisiasa, ilibidi wakabiliane na hizi siasa za CCM, kitu ambacho kilisababisha uhasama mkubwa wa kisiasa nchini ambapo kwa kiwango fulani mpaka sasa bado unaendelea. Hizi siasa ni zaidi ya partisan politics.

Yes, CCM ndiyo waasisi nchini wa siasa za isolationism kwa kudhani kuwa wao ni bora zaidi.
 
Katika siasa za Tanzania kuna accomodative politician and isolationist politician.

Mh. Zitto Kabwe anaendesha siasa zake kwa misingi ya accomadative politics kwa maana kuwa, siasa zake zina nafasi ya masikilizano na pia makubaliano na makundi mengine yaliyoko ndani na nje ya chama chake.

Tatizo lililopo hapa ni baadhi ya wanaCHADEMA wamejengwa kisiasa katika misingi ya isolationist politics kiasi cha kujenga fikra na mitazamo ya kihasama kati ya wao kwa wao au kati yao na vyama vingine vya kisiasa. Sababu kuu ni hii fikra ya kudhani wao ni bora kuliko wengine, na ili ufanikiwe lazima uwe mmoja wao. Huu ni aina fulani ya ubinafsi wa kisiasa ambao unasababisha kutumia njia zozote zile katika kufanikisha malengo yake.

Hili kundi ndani ya CHADEMA ambalo siasa zake ndizo zinazofanywa na Katibu Mkuu wa CHADEMA, ukichunguza kwa undani utagundua kuwa ndilo ambalo linamuona Mh. Zitto kama siyo active kwenye siasa zao.

Mh. Mwigulu yeye siasa zake niza mlengo wa isolationism kama lilivyo kundi ndani ya CHADEMA linalomuona Mh. Zitto siyo active kwenye siasa zao.

Kwa kawaida, kundi lenye mlengo wa siasa za isolationist huwa halipikiki kwenye chungu kimoja na kundi jingine lenye mlengo kama huo. Ndiyo maana Mh. Mwigulu ni sumu kwenye hili kundi ndani ya CHADEMA lakini kwa vile Mh. Zitto ni accomodative politician, siyo ajabu kumuona kwenye maelewano na makundi mengine pamoja na kwamba isolationist wanakuwa hawana imani naye 100%.

Accomodative politicians wengine ninaowaona kwenye uongozi wa juu ndani ya CHADEMA ni kama Mh. Mbowe, Mh. Mnyika, Said Arfi...
masanjasb

Hii post ina jibu sahihi la swali lako kwa undani kabisa. Mkuu Ng´wamapalala Kwa post hii amefunga mjadala.

Nakuomba masanjasb uiweke hii post ya Ng´amapalala kama update au clarification hapo juu kwenye threa post tafadhali.

Asante sana.
 
Last edited by a moderator:
jamaa kapotosha,Zitto alikuwepo ila tukumbushe alifanya nini dhidi ya propaganda chafu za Mwigulu,tena zikisemwa mbele yake?

Kama nimepotosha umma naomba samahani sana,ila ili nafsi yangu itendewe haki wekini clip ya kipindi hicho,kwa yoyote mwenye access nayo yawezekana wakati mwigulu anatamka maneno ya ugaidi mie nilighabika nikasusa Tv,lakini niliangalia kipindi karibia chote na kuwaona mtatiro na mwigulu pekee,pia vipindi vya star tv kualika wanasiasa viko vingi yawezekana kipindi nachoongelea mie sicho unachoongelea wewe
 
Back
Top Bottom