Kuna haja ya kuanza kuwafundisha watoto ujuzi mapema wakiwa bado wadogo?

Red Giant

JF-Expert Member
Mar 9, 2012
15,658
20,903
Zamani suala la kumpatia mtoto ujuzi utakao mfaa maishani lilikuwa ni jukumu la mzazi. Mzazi mvuvi alimfundisha mtoto uvuvi. Mfua chuma, mganga, mkulima, mfinyanga vyungu, mrina asali, mfugaji, mfanyabiadhara nk. Ujuzi ulitoka kwa mzazi kwenda kwa mtoto.

Ikaja hii elimu rasmi. Jukumu la kumfundisha mtoto ujuzi likawa la shule na waalimu huko. Na mbaya huu ujuzi wa shuleni mzazi ni ngumu kumrithisha mtoto. Na kibaya hata zaidi, ujuzi huu wa shuleni umeanza kutokuwa na msaada kwa alioupata. Kuajiriwa ni kazi na wala hawezi kujiajiri.

Mi naona kuna haja kubwa ya kurudi utaratibu wa kufundisha watoto ujuzi. kwa sababu wazazi wenyewe haeana ujuzi wowote wa maana, badi Badala ya mtoto kwenda twisheni ya hesabu, basi aende twisheni ya computer programming, umeme, upishi, ufundi bomba, magari, ujenzi nk nk nk.

Kwenye likizo mwezi mwezi wa sita apate kozi mbalimbali za ujuzi. Kwanza watoto wa tz ni moja ya wanaotumia muda mchache sana shuleni kwa mwaka. Wana muda mwingi nje ya shule wa kujifunza ujuzi unaoweza kuwafaa maishani.

Jambo hili linawezekana? Linafaa?
 
Idea nzuri...

Kitu kingine, unaweza ukamwandikisha mtoto wa kati ya miaka 3 hadi 12 hapo kwenye madarasa mbali mbali ya lugha za kigeni, huwa wanaelewa chap...
 
Idea nzuri...

Kitu kingine, unaweza ukamwandikisha mtoto wa kati ya miaka 3 hadi 12 hapo kwenye madarasa mbali mbali ya lugha za kigeni, huwa wanaelewa chap...
Hii ni skill nyingine nzuri ya kumfaa maishani.
 
Ni kweli mzazi ka una biashara Anza kumfundisha mwanao mapema, ka una kampuni Anza kumfundisha mtoto jinsi ya kufanya kazi, ku network even lobbying hapo utakuwa umetoa msaada mkubwa kuliko kukazania tu mtoto kupata A, Mimi binafsi wanangu nitawafundisha extra curriculum activities za kusaka hela na opportunities kuliko kumeza madesa na kupata A zote with nothing in hands rather than A.
 
Ni kweli mzazi ka una biashara Anza kumfundisha mwanao mapema, ka una kampuni Anza kumfundisha mtoto jinsi ya kufanya kazi, ku network even lobbying hapo utakuwa umetoa msaada mkubwa kuliko kukazania tu mtoto kupata A, Mimi binafsi wanangu nitawafundisha extra curriculum activities za kusaka hela na opportunities kuliko kumeza madesa na kupata A zote with nothing in hands rather than A.

Unataka mtoto mwenye akili, serious..! Fanya fanya uzae na Ncha Kali, the genius.!!
 
Zamani suala la kumpatia mtoto ujuzi utakao mfaa maishani lilikuwa ni jukumu la mzazi. Mzazi mvuvi alimfundisha mtoto uvuvi. Mfua chuma, mganga, mkulima, mfinyanga vyungu, mrina asali, mfugaji, mfanyabiadhara nk. Ujuzi ulitoka kwa mzazi kwenda kwa mtoto.

Ikaja hii elimu rasmi. Jukumu la kumfundisha mtoto ujuzi likawa la shule na waalimu huko. Na mbaya huu ujuzi wa shuleni mzazi ni ngumu kumrithisha mtoto. Na kibaya hata zaidi, ujuzi huu wa shuleni umeanza kutokuwa na msaada kwa alioupata. Kuajiriwa ni kazi na wala hawezi kujiajiri.

Mi naona kuna haja kubwa ya kurudi utaratibu wa kufundisha watoto ujuzi. kwa sababu wazazi wenyewe haeana ujuzi wowote wa maana, badi Badala ya mtoto kwenda twisheni ya hesabu, basi aende twisheni ya computer programming, umeme, upishi, ufundi bomba, magari, ujenzi nk nk nk.

Kwenye likizo mwezi mwezi wa sita apate kozi mbalimbali za ujuzi. Kwanza watoto wa tz ni moja ya wanaotumia muda mchache sana shuleni kwa mwaka. Wana muda mwingi nje ya shule wa kujifunza ujuzi unaoweza kuwafaa maishani.

Jambo hili linawezekana? Linafaa?
Mkuu una akili Sana. Mie nawaza namna wanangu watakavyotumia muda mwingi Sana katika crafting of their art.
Yaani nawaza nimpige mwalimu hela awe anaenda shule kwa siku mbili tu. Shule nyingine iwe labda veta ama anakomalia sport anayoipenda.
Mana wasomi soko limeisha na hawalipwi like wanamichezo.
Shule ya vitendo inahitajika Sana Tena Sana. China ndo wako huko kwa Mana ya kuwa Engineer from Veta University analipwa zaidi like twice kuliko aliyetokea hivi vyuo vya kiakademic aka theory oriented like udsm and like.
Yaani sipendi akariri mfano table Mana iko kwenye daftari nyuma ama kwa kalkuleta Kuna haha gani ya kumeza konstanti na huku zipo kisa tu eti aonekane mtabe awe wa kwanza na malipo yake ni sifa tu.

Yaani nawaza mfano mtt Kama ni mechanics anainza mapema.anaenda shule kule ili apate basics halafu anakomalia Kama ni umeme.
Pia nawaza ni jinsi gani primary atumie miaka minne tu.yaani naumiza akili Sana Ila mbele ya pesa najua hakuna kinachoshindikana. Ni aheri asome fomu three hata miaka miwili ama mitatu kuliko huku primary kumsoma sijui mirambo
 
Back
Top Bottom