Tabia za Kuwatahiri watoto wadogo na kuwatoboa masikio na pua mabinti wadogo zinapaswa kulaaniwa na kukomeshwa

Wamuyaya

Member
Apr 4, 2021
72
68
Ndugu zangu, nimesimama mbele yenu ili kuwashirikisha ukatili wanaofanyiwa watoto wadogo (wa kiume na kike) na wazazi/walezi wao. Wazazi na walezi wa watoto hawa naamini wanawafanyia ukatilii huu watoto wao kwa sababu ya ujinga tu.

Kwa mfano, utakuta binti mdogo anatobolewa masikio tena wakati mwingine bila ganzi kwa kisingizio kuwa wanamfanya awe mrembo. Hii naona haipo sawa, ni ukiukwaji wa haki ya mtoto. Wewe mzazi/mlezi nani amekwambia kuwa mtoto huyo anahitaji urembo huo? Kwa nini msimwache hadi atakapokuwa mtu mzima aamue yeye mwenyewe kuutafuta urembo huo? Acheni mambo ya kishamba! Binafsi nimekataa katakata kuwatoboa masikio mabinti zangu...mama yao ananilaumu na kuniona mimi ni mshamba, nimemwambia acha nibaki na ushamba wangu.

Vivyo hivyo, tupo wazazi/walezi tunaowatahiri watoto wetu wa kiume ili kudumisha mila zetu. Hebu fikiria mtoto mdogo wa miaka 12 au 15 anapelekwa porini/jando anatahiriwa bila ganzi. Huu ni ukatili na ukiukwaji wa haki ya mtoto. Kuna wazazi wengine pia tuna kawaidi ya kuwapeleka hispitali watoto wadogo kwa lengo la kuwatahiri, tukisingizia sababu za kiafya. Sina uhakika kama sababu hiyo ina mantiki yoyote...Mbona zamani hatukuwa tunatahiriwa kwa umri huo na afya zetu zilikuwa imara tu? Tuache mambo ya kishamba! Tuwape wototo haki zao, watakapokuwa watu wazima wataamua wenyewe kutahiri au kubaki na govi.

Ni jukumu la kila mtu kuhakikisha haki za watoto zinalindwa. Mashirika ya kutetea haki za binadamu pia yanapaswa kuangalia ukatili huu kwa jicho la tatu. Pia wataalam wa sheria wanaweza kukusaidia juu ya hili...Nawasilisha!
 
...Mbona zamani hatukuwa tunatahiriwa kwa umri huo na afya zetu zilikuwa imara tu? Tuache mambo ya kishamba! Tuwape wototo haki zao, watakapokuwa watu wazima wataamua wenyewe kutahiri au kubaki na govi.
Zamani ni miaka ipi mkuu?
Sasa ngoja uambiwe kijana wako anatakiwa atahiriwe kwa sababu za kiafya halafu ugome utaleta mrejesho.
 
Zamani ni miaka ipi mkuu?
Sasa ngoja uambiwe kijana wako anatakiwa atahiriwe kwa sababu za kiafya halafu ugome utaleta mrejesho.
Vipi kuhusu wanaowapeleka porini/jando na kuwatahiri bila ganzi...wewe kama mzazi unalionaje hili? Naomba useme neno pia hapo kwenye kuwatoboa masikio mabinti wadogo, ikiwezekana tupatie na uzoefu wako ili tuokoe kizazi.
 
kama JF wanaruhusu bandiko kama hili, sijui yale waliyo yazuia yatakuwaje...

hoja yako ilipaswa ielekezwe kwenye njia zitumikazo kwenye kuwatahiri watoto au kuwatoboa masikio na sio kuzuia kwa ujumla🚮
 
Kuhusu kutahiriwa umepuyanga mkuu unasema kwamba wakikuta ndo wachague kutahiriwa ama kubaki na govi?
Ama na wewe haujatahiriwa nini acha bangi zina kuharibu
 
Vipi kuhusu wanaowapeleka porini/jando na kuwatahiri bila ganzi...wewe kama mzazi unalionaje hili? Naomba useme neno pia hapo kwenye kuwatoboa masikio mabinti wadogo, ikiwezekana tupatie na uzoefu wako ili tuokoe kizazi.
Kuhusu kuwapeleka porini kuwatahiri bila ganzi siwezi kuzungumzia mila za watu mkuu. Ila mimi binafsi siwezi kutahiri wanangu namna hiyo hata kama mila inanilazimu.

Hapo kwenye kutoboa masikio sasa, no comment 😂
 
Kuhusu kutahiriwa umepuyanga mkuu unasema kwamba wakikuta ndo wachague kutahiriwa ama kubaki na govi?
Ama na wewe haujatahiriwa nini acha bangi zina kuharibu
Sijatahiri mkuu, na utafiti unaonesha mashine isiyokatwa ndio inapiga kazi vzr.
 
Back
Top Bottom