Kumbukumbu: Soma la Kiswahili la Rais Ali Hassan Mwinyi

Chamoto

JF-Expert Member
Dec 7, 2007
8,339
17,586
Namkumbuka Rais Mwinyi kwa mengi, moja wapo ni pale alipoanzisha kipindi chake cha kiswahili RTD (Radio Tanzania Dar es salaam). Moja ya somo alilofundisha lilihusu tarakimu. Alisema, "katika tarakimu za kiswahili, kuna baadhi zina maneno yenye asili ya kibantu na nyingine kiarabu.

Tofauti na zile za asili ya kiarabu, zile za kibantu huwa zinaweza kutamkwa kwa uwingi". Mfano 1,2,3,4,5,8 ni tarakimu za kibantu, hivyo tunaweza sema watu wawili, watatu nakadhalika lakini hatuwezi kusema watu wasita au watisa, kwasabau hayo ni maneno yenye asili ya kiarabu".

RIP Rais Mwinyi.
 
Mimi nukuu yake niliyoipenda ni ile ya hivi karibuni " maisha ni hadithi, tujitahidi tuwe na hadithi nzuri" nitaitafuta ili niinukuu vizuri
 
Mimi nukuu yake niliyoipenda ni ile ya hivi karibuni " maisha ni hadithi, tujitahidi tuwe na hadithi nzuri" nitaitafuta ili niinukuu vizuri
Kweli hii hotuba ya hadithi huwa naipenda sana.
 
Back
Top Bottom