Mystery
JF-Expert Member
- Mar 8, 2012
- 15,484
- 30,160
Kwenye nchi yoyote duniani, inayoweza kusema inaendesha utawala bora, ni lazima iruhusu mfumo wa mihimili 3 mikuu ya nchi, ambayo ni Serikali, Bunge na Mahakama kujiendesha katika kutoingiliana katika uendeshaji wa shughuli zao, katika kile kinachoitwa "checks and balance"
Hali ni tofauti kubwa kwa hapa nchini, ambapo Mhimili wa Serikali, mkuu wake ambaye ni Rais, aliwahi nukuliwa akisema kuwa mhimili wake ndiyo uliojichimbia zaidi chini na kuifanya hiyo mihimili mingine miwili ya Bunge na Mahakama, kuwa si lolote wala chochote!
Nimekuwa nikijiuliza hivi kulikuwa na mantiki gani ya kupeleka muswada wa kuweka kinga ya kushitakiwa kwa wakuu wa hiyo mihimili miwlii. ikiwa wao ni watumishi wa Umma, ambao wanasitahili kuwajibika pale wanapokosea?
Jibu la swali hilo nimelipata baada ya kufuatilia mienendo ya hiyo mihimili miwili katika siku za karibuni.
Nianze na Bunge letu. Hivi hiki kiburi cha Spika wetu, Job Ndugai cha kuyapinga hadharani maamuzi ya Kamati Kuu ya CHADEMA kuhusu kuwavua uanachama wa chama chao angeyapata wapi kama siyo hiyo kinga aliyopata ya kushitakiwa na mahakama yoyote hapa nchini?
Hivi inakuwaje Spika wa Bunge Job Ndugai ayakatae hadharani maamuzi ya kikao cha Kamati Kuu ya chama kinachotambulika kihalali cha Chadema ya kuwavua uanachama kwa wale wabunge 19, ambao waliamua kujipeleka wenyewe kuapishwa, bila kufuata utaratibu wa kupitishwa na chama chao cha Chadema?
Hivi huyu Ndugai anataka kuuambia Umma wa watanzania kuwa ameamua kuisigina kwa makusudi Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977, ibara ya 71(1)(e) ambayo inaeleza wazi kuwa mbunge yeyote anapovuliwa uanachama wake na chama kilichomdhamini ubunge wake "automatically" na ubunge wake unakoma?
Mfano wa pili ni kwa huyu DPP wetu, Biswalo Mganga, ambaye naye ameamua kuisigina Katiba yetu ya nchi kwa kumtoa mahabusu, Nusrat Hanje, usiku wa tarehe 23/11/2020, tena bila "release order" yake kuidhinishwa na Hakimu aliyehusika na kumpeleka ndani mtuhumiwa huyo, kwa lengo moja tu la "kumwahisha" ili akale kiapo cha kuwa Mheshimiwa Mbunge kesho yake ya tarehe 24/11/2020?
Tulitegemea Mkuu wa Mhimili huo wa Mahakama ambaye ni Jaji Mkuu, ajitokeze hadharani na kukemea vikali kitendo hicho cha kuidhalilisha mahakama yake, lakini "ububu" wa Jaji Mkuu huyo ndiyo ninaoweza kuusema kuwa mhimili wake umewekwa "mfukoni" na mhimili wa serikali!
Kwa mifano hiyo miwili inatosha kuuthibitishia Umma wa watanzania kuwa muswada ule wa kuwawekea kinga ya kushitakiwa, uliopelekwa "chap chap" na utawala huu wa serikali ya awamu ya tano, mwaka huu kabla ya kulivunja Bunge, ulikuwa na lengo la kuwafanya hao wakuu wa mihimili hiyo miwili "waisalimishe" kwa mhimili mmoja ambao umejichimbia zaidi chini, mhimili wa serikali.
Hali ni tofauti kubwa kwa hapa nchini, ambapo Mhimili wa Serikali, mkuu wake ambaye ni Rais, aliwahi nukuliwa akisema kuwa mhimili wake ndiyo uliojichimbia zaidi chini na kuifanya hiyo mihimili mingine miwili ya Bunge na Mahakama, kuwa si lolote wala chochote!
Nimekuwa nikijiuliza hivi kulikuwa na mantiki gani ya kupeleka muswada wa kuweka kinga ya kushitakiwa kwa wakuu wa hiyo mihimili miwlii. ikiwa wao ni watumishi wa Umma, ambao wanasitahili kuwajibika pale wanapokosea?
Jibu la swali hilo nimelipata baada ya kufuatilia mienendo ya hiyo mihimili miwili katika siku za karibuni.
Nianze na Bunge letu. Hivi hiki kiburi cha Spika wetu, Job Ndugai cha kuyapinga hadharani maamuzi ya Kamati Kuu ya CHADEMA kuhusu kuwavua uanachama wa chama chao angeyapata wapi kama siyo hiyo kinga aliyopata ya kushitakiwa na mahakama yoyote hapa nchini?
Hivi inakuwaje Spika wa Bunge Job Ndugai ayakatae hadharani maamuzi ya kikao cha Kamati Kuu ya chama kinachotambulika kihalali cha Chadema ya kuwavua uanachama kwa wale wabunge 19, ambao waliamua kujipeleka wenyewe kuapishwa, bila kufuata utaratibu wa kupitishwa na chama chao cha Chadema?
Hivi huyu Ndugai anataka kuuambia Umma wa watanzania kuwa ameamua kuisigina kwa makusudi Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, 1977, ibara ya 71(1)(e) ambayo inaeleza wazi kuwa mbunge yeyote anapovuliwa uanachama wake na chama kilichomdhamini ubunge wake "automatically" na ubunge wake unakoma?
Mfano wa pili ni kwa huyu DPP wetu, Biswalo Mganga, ambaye naye ameamua kuisigina Katiba yetu ya nchi kwa kumtoa mahabusu, Nusrat Hanje, usiku wa tarehe 23/11/2020, tena bila "release order" yake kuidhinishwa na Hakimu aliyehusika na kumpeleka ndani mtuhumiwa huyo, kwa lengo moja tu la "kumwahisha" ili akale kiapo cha kuwa Mheshimiwa Mbunge kesho yake ya tarehe 24/11/2020?
Tulitegemea Mkuu wa Mhimili huo wa Mahakama ambaye ni Jaji Mkuu, ajitokeze hadharani na kukemea vikali kitendo hicho cha kuidhalilisha mahakama yake, lakini "ububu" wa Jaji Mkuu huyo ndiyo ninaoweza kuusema kuwa mhimili wake umewekwa "mfukoni" na mhimili wa serikali!
Kwa mifano hiyo miwili inatosha kuuthibitishia Umma wa watanzania kuwa muswada ule wa kuwawekea kinga ya kushitakiwa, uliopelekwa "chap chap" na utawala huu wa serikali ya awamu ya tano, mwaka huu kabla ya kulivunja Bunge, ulikuwa na lengo la kuwafanya hao wakuu wa mihimili hiyo miwili "waisalimishe" kwa mhimili mmoja ambao umejichimbia zaidi chini, mhimili wa serikali.