Kumbe kubeba mimba si mchezo!

Kumbe kubeba mimba si mchezo!

Sijaexperience hilo ila penda sana kuperuzi a healthy baby jinsi yakumpata nini ule , kuepuka kutapikA ,kuwa na wewe na afya njema . Hadi mwisho uende kujifungua
 
Mnamtisha tu na kujiendekeza. Usister do na kujiendekeza ndio unawasumbua. Wengine huku vijijini wanajifungua leo kesho anaenda shamba. Mwaka 2014, mke wangu anaenda jifungua mtoto wa 4 pale Morogoro Hospital tumemsindikiza labour nikakuta binti mmoja anapiga kelele huku anamtukana mmewe. Yule binti kila anachoambiwa na wale wakunga/manesi hasikii yeye ni kujiliza tu mara ajipige selfie mara aangalie kama makope bandia yameanguka, mara alie mbona k yangu inatanuka mara inachanika na upuuzi kibao. Wale wasaidizi wakamwambia kama unaleta ujuaji, tutakuacha ufe.

Hii ndio inayowtesa wanawake wa kisasa ila hakuna uchungu wa kutisha hivyo. Mke wangu tulimpeleka saa 7, saa 9 kajifungua Glory wetu na saa 12 tumerudi kwetu yaani walimruhusu kuondoka.
Wanakuza mambo hawa wanawake
 
Ungekuwa Idete kule Dabaga Kilolo au ungekuwa Ilunde kule Inyonga Katavi umeolewa na msukuma hadi afanye vibarua vya kufyetua tofali ndio mpate pesa ya kula hayo yasingetokea. Ni kujiendekeza tu, mbona wengine wake zetu hawana hayo. Kwa watoto wote 4, sijawahi shuhudia hayo. Mungu awasaidie sana.
So wanajidekeza?? Dah.
 
Jamani kwema?
Ila wanawake ni wasiri jamani, mbona hata hamsemagi kwamba hizi "morning sickness" hilo ni neno tu ila inashinda siku nzima jamani?

Natamani hata mtu angeniambia kwamba ni vichefuchefu siku nzima. Mimi nilijua kama jina lilivyo basi ikifika mchana natakiwa niwe fresh.

Week 8 sasa ila food eversion na nausea muda wote. Kila chakula ninachokifikiria nahisi kichefuchefu.

Nahisi kuumwaumwa tu nikikaa sisikii raha nikilala sisikii raha bora hata kutembea tembea nje. Hiki kichefuchefu natamani hata nitapike ila ni kichefuchefu tu bila kutapika. Khaaa hadi natamani nipige mayowe.

Acha tu jamani watu waringe na watoto wao. Sasa nimeelewa.
Na hapo bado siku ya kujifungua utalia kama mbuzi Meeeeee
 
Jamani kwema?
Ila wanawake ni wasiri jamani, mbona hata hamsemagi kwamba hizi "morning sickness" hilo ni neno tu ila inashinda siku nzima jamani?

Natamani hata mtu angeniambia kwamba ni vichefuchefu siku nzima. Mimi nilijua kama jina lilivyo basi ikifika mchana natakiwa niwe fresh.

Week 8 sasa ila food eversion na nausea muda wote. Kila chakula ninachokifikiria nahisi kichefuchefu.

Nahisi kuumwaumwa tu nikikaa sisikii raha nikilala sisikii raha bora hata kutembea tembea nje. Hiki kichefuchefu natamani hata nitapike ila ni kichefuchefu tu bila kutapika. Khaaa hadi natamani nipige mayowe.

Acha tu jamani watu waringe na watoto wao. Sasa nimeelewa.
Ukisikia kichefuchefu tapika usijizuie kutapita ndio kidogo unapata ahueni. Na uombe Mungu sana hyo Hali ikate mapema kuliko ukakaa nayo miezi 9.
 
Mnadekezana sana wa mjini!

Anyway mazingira ndo chanzo cha huo ushauri,
Kijijini mimba uwe nayo usiwe nayo shughuli zinakusibiri na kituo cha ushauri sio hapo karibu!

Kuna mzee 1 nilionyeshwa pale mpakani Sirari yeye mkewe kila akizaa mtoto wa kike asubuhi yake ni shambani tu, Mungu mkuu mimba ya sita kazaa mtoto wa kiume unaambiwa mzee alifanya bonge la sherehe kwa mkewe!

Cha ajabu nikaambiwa kwa baadae mkewe ndo kamshauri aoe mke mwingine wasaidizane shughuli
 
Sijaexperience hilo ila penda sana kuperuzi a healthy baby jinsi yakumpata nini ule , kuepuka kutapikA ,kuwa na wewe na afya njema . Hadi mwisho uende kujifungua
Havina formula.yaani huwezi jipanga useme.sitaki morning sickness .so unaenda tu na biti
 
Mnadekezana sana wa mjini!

Anyway mazingira ndo chanzo cha huo ushauri,
Kijijini mimba uwe nayo usiwe nayo shughuli zinakusibiri na kituo cha ushauri sio hapo karibu!

Kuna mzee 1 nilionyeshwa pale mpakani Sirari yeye mkewe kila akizaa mtoto wa kike asubuhi yake ni shambani tu, Mungu mkuu mimba ya sita kazaa mtoto wa kiume unaambiwa mzee alifanya bonge la sherehe kwa mkewe!

Cha ajabu nikaambiwa kwa baadae mkewe ndo kamshauri aoe mke mwingine wasaidizane shughuli
Hayo ni ya huko kwenu
Huku mjini mwezi mzima tunaogeshwa kabisa.ni kula kunyonyesha tu.tena tunakamua unalala kimashine kinakukamua. mtoto anapewa maziwa huko .sisi ni kulala tu na kufanyiwa massage
Mwezi ukiisha bado hufanyi kazi labda uoge tu mwenyewe sasa ila kila kitu unafanyiwa.
 
Mnadekezana sana wa mjini!

Anyway mazingira ndo chanzo cha huo ushauri,
Kijijini mimba uwe nayo usiwe nayo shughuli zinakusibiri na kituo cha ushauri sio hapo karibu!

Kuna mzee 1 nilionyeshwa pale mpakani Sirari yeye mkewe kila akizaa mtoto wa kike asubuhi yake ni shambani tu, Mungu mkuu mimba ya sita kazaa mtoto wa kiume unaambiwa mzee alifanya bonge la sherehe kwa mkewe!

Cha ajabu nikaambiwa kwa baadae mkewe ndo kamshauri aoe mke mwingine wasaidizane shughuli

Hata huku mjini kuna watu wana mimba na haziwasumbui wanaendelea na shughuli zao kama kawaida.

Ila unapaswa kutambua kila mwili wa mtu ni tofauti. Hata huko unapopasifia sio wote wana uwezo wa kubeba mimba wakaendelea na heka heka zao.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom