Hannah
JF-Expert Member
- Aug 28, 2015
- 10,146
- 41,401
Hii ndio inayowtesa wanawake wa kisasa ila hakuna uchungu wa kutisha hivyo. Mke wangu tulimpeleka saa 7, saa 9 kajifungua Glory wetu na saa 12 tumerudi kwetu yaani walimruhusu kuondoka.
Mshukuru Mungu kwa kumjalia neema mke wako ya kujifungua salama kwa wakati na bila usumbufu au matatizo yoyote ki afya ila hiyo neema aliyokupa Mungu isikupe kiburi ukamkufuru.
Unataka kuniambia wanaofia leba wakijifungua nao huwa wanaigiza kufa? Au wanaoshindikana kujifungua kawaida hadi wanaamua kumfanyia upasuaji ule ni uigizaji?
Kiburi cha uzima kinakusumbua . Mshukuru Mungu kwa ajili ya neema yake maishani mwenu ila usikufuru. Hiyo ni Neema tu wala haukustahili.
