Kumbe kubeba mimba si mchezo!

Kumbe kubeba mimba si mchezo!

Sikia miezi mitatu minne ya mwanzo yaani hakuna rangi utaacha kuona.mimi nilikuwa natamani kutapika dunia yote.yaani chakula unachagua nilikuwa najipikia mwenyewe maana mtu akipika asipopika kama navotaka na yeye namchukia vibaya mno sitaki hata kumuona tena nikija kumuona natapika tu
Ila nikuombe usiache kutumia folic japo zinachangia kuchefua ila usiache
Ukimaliza miezi ya mwanzo mwezi wa nne kati hapo hadi saba unakuwa sawa ila kuchoka sana maana mtumbo unakuwa ushaanza kujaa na unatakiw ulale kushoto sana.so unachoka na uzito unakuwa umeongezeka hata kilo 10 hivi
Miezi ya mwisho nayo ni kuchooka maana mtoto anakuwa kawa mkubwa zaidi ila hujiskii vibaya kiivo jikaze
Ila hakikisha una folic na mavitamins ili uzae katoto kazuri
Asante dear kwa huu mwongozo.
Natumia pregnacare ya UK na ina folic ndani ila sasa ina chefua ila ndio nimeamua siachi kumeza angalao hii miezi mitatu ya mwanzo iishe kwanza.
 
Jamani nimesikia hadi raha, ubarikiwe. I cant wait kusikia mtoto anacheza tumboni.
Kuanzia week ya 20 utaanza kusikia movements japo wengine huanza kuhisi hata week ya 16.... hua inafurahisha sana ukikagusa na kenyewe kama respond kwa kukick kataanza kukick usiku wa manane na wewe usingizi ndio umekolea patamu hapo, hapo weka mkono wako tumboni au wa baba ake amshike amshike hadi atulie.
 
Kuna wengine hawapati shida hata moja kila mtu na bahati yake asikutishe shoga
Hii kweli namuona hata wife akibeba mimba anacheka cheka tu siku ikifika mwenyewe anajisalimisha mchezo unaisha hajawahi zingua wala kugoma kula zaidi akiwa na mimba vitunguu weka mbali kabisa.
 
Namshukuru Mungu nina mume. Sipati picha kuyapitia haya ninayoyaona bila baba wa mtoto pembeni jamani.

Wanaume msiwe mnakataa mimba. Hiki kipindi ni kigumu sana halafu mtu aongeze na stress za kukataliwa kweli?
Hapo sawa! Jikaze yatapita tu
 
Kuna wengine hawapati shida hata moja kila mtu na bahati yake asikutishe shoga
Ni sahihi pia anatakiwa ashukuru. Kuna watu hadi kufa kwao hawajawahi pitia hiko anachopitia.

Nakumbuka mke wangu alikuwa na rafiki mama mtu mzima mmoja hajawahi kubeba mimba wala kujifungua akawa anamuuliza hivi uchungu unaumaje. Yule Mama hadi kufa kwake hakuwahi kupata mtoto.
 
Hiyo hali utakua nayo katika miezi mitatu ya mwanzo 'First Trimester' baada ya hapo utakua poa na kuenjoy ujauzito wako,

Mtoto akianza kucheza ni best experience ever, gusa gusa tumbo lako mara kwa mara ili mtoto afeel your love, zungumza na mtoto wako, muimbie nyimbo nzuri za watoto,msomee hadithi, kua happy muda wote epuka stress na hasira, wamatumbi wana msemo wao "happy mother, happy baby"

Zingatia mlo kamili kwani a healthy child anatokana na chakula bora cha mama, lakini pia uzingatie na diet yako pia usile kama fukufuku na kunenepeana hovyo,

Hongera sana Mama mtarajiwa, nakuombea kheir kwako na kwa mtoto mvuke salama,

NB: Hayo utayakuta kwenye second na third trimester ila kwa sasa msoto lazima.
HOHEHAHE nikionaga mchango wako tu lazima kiroho kiniende mbio na udenda unitoke.

Nahodha mjeuri/mgumu ambaye nimenogewa na kipande cha mua... tartiiiiiibu M.V wasakatonge naizamisha kwa utamu wako mrembo 😋🤤
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom