Kumbe kubeba mimba si mchezo!

Kumbe kubeba mimba si mchezo!

Hahaha...........ila ni mateso sana Mkuu, yaani Mwanaume mzima nashinda nalamba limao ofisini kweli

Asubuhi kwenye gari lazima nibebe na kikopo cha kutema mate.

Kwa kweli siipendi hiyo hali basi tu
Ingekua ipo hivyo kwa wanaume wote basi kwa hakika wanaume wangewaheshimu sana wake zao na hata hao singo mamaz.
 
Mimba husumbua kwa baadhi ya watu kadri umri unavyosogea kuelekea kujifungua.

Kuna mimba humsumbua Mama, na baadhi akina Baba.

Mimi kila wife akibeba mimba basi ambaye anasumbuka huwa ni Mimi Baba.

Huwa nachagua vyakula, kichefuchefu lakini huwa sipendi mazingira machafu hata kama nitaenda ugenini.

Mbaya zaidi siku ya kujifunguza wife, basi dalili hunijia mimi.

Last time wife anakaribia kujifungua siku mbili mbele, basi nilishikwa na tumbo la kuendesha hadi alipojifungua ndiyo likakata.

Hivyo ni baadhi ya complications za mimba kwa akina Mama na akina Baba baadhi yetu.

Kwahiyo ukiwa Mzazi mtarajiwa, hivyo vitu ni vya kuzoea tu
Physics hyo magnetic forces
 
Namshukuru Mungu nina mume. Sipati picha kuyapitia haya ninayoyaona bila baba wa mtoto pembeni jamani.

Wanaume msiwe mnakataa mimba. Hiki kipindi ni kigumu sana halafu mtu aongeze na stress za kukataliwa kweli?
Shida ni kwamba ,, Mimba nyingine unashikishwa na unajua fika hapa tunapiga wengi🤨
 
Ingekua ipo hivyo kwa wanaume wote basi kwa hakika wanaume wangewaheshimu sana wake zao na hata hao singo mamaz.
Ni kweli usemacho Mkuu, kupitia hiyo hali nimejifunza kuwaheshimu sana Wanawake.

Hapa natamani Wife naye apate Mimba itakayomfanya ateseke kama Mimi. Maana zile mimba za mwanzo zote ni kama nilimsaidia tu.

Ila useme watoto ndiyo wote wamekuja kwangu, labda kwake wamefata rangi tu 🤗
 
Hiyo hali utakua nayo katika miezi mitatu ya mwanzo 'First Trimester' baada ya hapo utakua poa na kuenjoy ujauzito wako,

Mtoto akianza kucheza ni best experience ever, gusa gusa tumbo lako mara kwa mara ili mtoto afeel your love, zungumza na mtoto wako, muimbie nyimbo nzuri za watoto,msomee hadithi, kua happy muda wote epuka stress na hasira, wamatumbi wana msemo wao "happy mother, happy baby"

Zingatia mlo kamili kwani a healthy child anatokana na chakula bora cha mama, lakini pia uzingatie na diet yako pia usile kama fukufuku na kunenepeana hovyo,

Hongera sana Mama mtarajiwa, nakuombea kheir kwako na kwa mtoto mvuke salama,

NB: Hayo utayakuta kwenye second na third trimester ila kwa sasa msoto lazima.
Jamani nimesikia hadi raha, ubarikiwe. I cant wait kusikia mtoto anacheza tumboni.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom