Teslarati
JF-Expert Member
- Nov 21, 2019
- 1,873
- 7,318
Maxence namuomba huyu jamaa kituoni aje kutoa ushahidi... over.Heri ya mwaka mpya.
Hii kitu nilishawahi kuambiwa na mtu flani nikapinga, nikasema maybe huyu jamaa ana chuki na wivu na jitihada za vijana wajasirimali.
But baada ya kufikiria zaidi, it made so much sense, but sikuwa na uhakika 100%
Sasa kuna siku nilikuwa nimekaa na washkaji tunapiga story tunabadilishana mawazo, sasa hawa wanangu nawajua ni watumiaji wa bangi, sasa wakataka niwape lift wakachukue mzigo, fresh tukaingia kwenye gari tukaanza safari, sasa tulivofika (sinza) wakanielekeza nipaki mbele ya duka flani ivi la iPhone, washkaji wakatoka wakaingia kwenye hilo duka, mimi nilibaki kwenye gari.
Baada ya dakika 20 wakarudi bhana, nikawauliza "vipi mmepata" jamaa wakanijibu "uhakika kaka" nikajisemea kimoyomoyo "kumbe jamaa alienambia hivi viduka vya iPhone vina push hakukosea".
My take;
Vijana wenzangu tuweni makini, kupendapenda shortcut utaishia kujisaidia kwenye ndoo.
Punguza mdomo utafia jela.