Kulikuwa na wazee wa hizi kazi wawili tu. Saddam Hussein na Osama Bin Laden, Viongozi wa Iran wanachojua ni kupiga domo na kutegemea proxy wars,

Kulikuwa na wazee wa hizi kazi wawili tu. Saddam Hussein na Osama Bin Laden, Viongozi wa Iran wanachojua ni kupiga domo na kutegemea proxy wars,

mkata uzi

JF-Expert Member
Joined
Aug 3, 2025
Posts
1,910
Reaction score
5,451
1772656853833.png


1772656952894.png


Marekani walipoenda Iraq kwa Saddam Hussein hawakuweza kufikia hata kwa theluthi walichokiweza Iran, yani Iran wameigeuza kama sebule yao, wanajipigia tu.

Osama alikuwa mwiba sana, hadi Marekani wanamkamata ilikuwa shughuli nzito.

Iran alitegemea zaidi kufanya mashambulizi kwa Proxies kama Hamas, Hezbolah, Houthi, Vikundi vya Iraq na Syria.

Iran kupigana Direct ni mchovu sana, Israel na Marekani zinaingia Iran kama vile sebuleni. walitumia SEKUNDE 60 tu kuwafyeka Ayatollah na viongozi wengine wakubwa wa jeshi. SEKUNDE 60.

Yani Israel na Marekani watautumia sana huu mfano kila muda wakielezea uwezo wa majeshi yao.

Hadi sasa wiki bado haijaisha ila mifumo ya ulinzi wa Iran ipo nyanga nyanga si rada wala meli, leo hii ndege ya kivita ya Iran iliyotaka kujaribu kupigana na F 35 za Israel imepigwa angani punde tu ilipopaa.

Na vita inazidi kuwa nyepesi kwasababu wananchi wengi wapo upande wa Marekani na Israel, wanaona wanakombolewa sio vita hii.
 
Huyo Sadam alipigana na nchi ngapi kwa miaka mingapi?

Hizo nchi za ulaya kipindi kile uchumi wao ulikuwaje na sasa upoje?

Iraq na Libya walikuwa na technology za kijeshi zinazo karibiana na Iran?

Vita sio Sindimba hii vita ngumu, mataifa mawili tu ya NATO (France na UK), wanasema wao watamsaidia US ,kambi zao zilizo karibu na middle east na meli vita,ila hawaingizi wanajeshi wao vitani,wengine wamekula bati, Spain kamfukuza US na ndege yake ya mizigo baada ya kutaka kutumia viwanja vyake.
 
Osama alikua CIA agent, thanks to Edward Snowden aliyenifunulia ukweli huu na kwasasa yupo visiwa vya Bahamasi. Kuhusu sadam hussein hakua na jeshi lenye uwezo mkubwa kama wa irani ndioo maana alipgwa sanction akatepeta na kushughulikiwa kwa kusingiziwa kuwa na WMD(Weapon of Mass Destruction).

Wote hao osama na saddam ni takataka kwa irani ambayo imepigwa sanction zaidi ya miaka 40 na bado imefanya mapindizi makubwa kwenye sayansi na teknolojia. Na bado ndio nchi inayoida Taifa lako la Tanzania hela kubwa. Kwahyo ukichoandika ni mahaba nasio hoja zenye akili.
 
Huyo Sadam alipigana na nchi ngapi kwa miaka mingapi?

Hizo nchi za ulaya kipindi kile uchumi wao ulikuwaje na sasa upoje?

Iraq na Libya walikuwa na technology za kijeshi zinazo karibiana na Iran?

Vita sio Sindimba hii vita ngumu, mataifa mawili tu ya NATO (France na UK), wanasema wao watamsaidia US ,kambi zao zilizo karibu na middle east na meli vita,ila hawaingizi wanajeshi wao vitani.
Usiangalie wingi angalia uzito, mfano Iran kazipiga Bahrain, Qatar, Kuwait, Saudi kisa tu zina kambi za Marekani wala hakujali kambi hizo wanajeshi waliondoshwa na vifaa vingi vilitolewa kabla vita haijaanza.

Vita sio vifaa tu bali hata uchungu wa wananchi kwa taifa lao, vita hii ni nyepesi sana kwasababu wananchi wengi hawaipendi serikali yao, kwao ni ukombozi wala sio vita na ndio sababu shangwe zimetawala nchi nzima kasoro kwa ndugu, jamaa, marafiki na machawa wachache wa viongozi
 
Osama alikua CIA agent, thanks to Edward Snowden aliyenifunulia ukweli huu na kwasasa yupo visiwa vya Bahamasi. Kuhusu sadam hussein hakua na jeshi lenye uwezo mkubwa kama wa irani ndioo maana alipgwa sanction akatepeta na kushughulikiwa kwa kusingiziwa kuwa na WMD(Weapon of Mass Destruction).

Wote hao osama na saddam ni takataka kwa irani ambayo imepigwa sanction zaidi ya miaka 40 na bado imefanya mapindizi makubwa kwenye sayansi na teknolojia. Na bado ndio nchi inayoida Taifa lako la Tanzania hela kubwa. Kwahyo ukichoandika ni mahaba nasio hoja zenye akili.
Madai ya kwamba Osama Bin Ladeen alikuwa CIA ni story za vijiweni wala hakuna ushahidi wa kuaminika.

Edward Snowden hajawahi kutoa ushahidi rasmi kuthibitish hayo, ila alitoa ripoti ya Marekani kutumia teknolojia ya hali ya juu sana kumtrack Osama mpaka wakampata.

Edward Snowden hayupo Bahamas, yupo Urusi.

Kusema Iran imefanya mapinduzi kisayansi na Kiteknolojia ni kuwakuza sana, kwanza wanategemea zaidi silaha za China na Urusi ambazo zimewadhalilisha, Israel imepita na Ayatollah ndani ya sekunde 60 tu, Hizo teknolojia hazijasaidia chochote.
 
Usiangalie wingi angalia uzito, mfano Iran kazipiga Bahrain, Qatar, Kuwait, Saudi kisa tu zina kambi za Marekani wala hakujali kambi hizo wanajeshi waliondoshwa na vifaa vingi vilitolewa kabla vita haijaanza.

Vita sio vifaa tu bali hata uchungu wa wananchi kwa taifa lao, vita hii ni nyepesi sana kwasababu wananchi wengi hawaipendi serikali yao, kwao ni ukombozi wala sio vita na ndio sababu shangwe zimetawala nchi nzima kasoro kwa ndugu, jamaa, marafiki na machawa wachache wa viongozi
Unaongelea suala la serikali kupendwa na wananchi au Taifa lenye nguvu kati ya Iraq na Iran?
 
Unaongelea suala la serikali kupendwa na wananchi au Taifa lenye nguvu kati ya Iraq na Iran?
Acha kumfananisha Saddam huseein na kiongozi ambae kwa dakika ya kwanza tu ya mashambulizi waliondoka naye pamoja na jopo lake wakiwemo waziri wa ulinzi na viongozi wengne zaidi ya 40 . kuwa na adabu 😁

Marekani walipoenda Iraq kwa Saddam hawakuweza kufikia hata kwa asilimia 1 walichokiweza Iran.

Iran walitegemea zaidi proxy wars kufadhili vikundi
 
Usiangalie wingi angalia uzito, mfano Iran kazipiga Bahrain, Qatar, Kuwait, Saudi kisa tu zina kambi za Marekani wala hakujali kambi hizo wanajeshi waliondoshwa na vifaa vingi vilitolewa kabla vita haijaanza.

Vita sio vifaa tu bali hata uchungu wa wananchi kwa taifa lao, vita hii ni nyepesi sana kwasababu wananchi wengi hawaipendi serikali yao, kwao ni ukombozi wala sio vita na ndio sababu shangwe zimetawala nchi nzima kasoro kwa ndugu, jamaa, marafiki na machawa wachache wa viongozi
Kuzipiga hizo ni lazima ,bila kufanya hivyo ndege za US zingekuwa na uhakika wa kupata maeneo ya ndege zao kutua na kujaza mafuta, kwa sasa hayo maeneo mengi yameripuliwa na uzuri Iran aliziambia mapema hizo nchi za middle east. Ndio maana nchi za middle east zimeanza kuangalia upya uhusiano wao na US. Mpaka sasa US katimuliwa Spain na India wamempiga marufuku kutumia bandari.

Vita gharama wewe US Iraq pale zimekatika USD 3T ,yani fedha ndio kitu cha kwanza.Hizo za kusema wananchi hawawapendi viongozi wa hizo propaganda, kama kipindi kile waliposema Sadam ana Nuclear, baadae Tony Blair anakubali walipokea wrong Intel kuhusiana na Iraq.

Hivi vita atapigana Myahudi na US, Iraq US na nchi zote za NATO iliwachukua miaka nane, kumpiga Iraq,sasa hivi nchi za NATO zina hali mbaya za kiuchumi sababu ya Corona na vita ya Ukraine. Wakiangalia capability ya Iran na resources walizokuwa nazo wanaona bora wakae pembeni.
 
Acha kumfananisha Saddam huseein na kiongozi ambae kwa dakika ya kwanza tu ya mashambulizi waliondoka naye pamoja na kiongozii mkuu,waziri wa ulinzi na viongozi wengne zaidi ya 40 . kuwa na adabu 😁

Iran walitegemea zaidi proxy wars kufadhili vikundi
Unakumbukumbu juu ya vita ya Iran na Iraq?
Nani alitandikwa?
 
Bado upo mweupe na unaongozwa na mahaba na hisia pia hutumii akili kufikilia. Alafu aliye Bahamas ni huyo gaidi alitengenezwa na CIA. Irani silaha zake ni 90% uzalishaji wa ndani hio 10% ndio anaagiza nje tena ni kujua teknolojia iliyopo na kuzitumia as strategic tu nasio tegemezi kwa ulinzi.

Alafu kumua ayatollah sio kigezo cha kushinda vita na kubadilisha mfumo wa uongozi hivyo bado nakuambia upo mweupe kwenye siasa za mashariki ya kati. Wew hata nikikuliza ni kwanini Zimbabwe na umasikini wao wote kwanini serikali yao imekataa msaada wa afya wa Dola za Marekani milioni 367 kutoka Washington. Lazima utanijibu kwa hoja za kitoto na nikikuambia the reason behind utasema hizo ni story za vijiweni zisizo na ushahidi.
 
View attachment 3552589

View attachment 3552591

Marekani walipoenda Iraq kwa Saddam Hussein hawakuweza kufikia hata kwa theluthi walichokiweza Iran, yani Iran wameigeuza kama sebule yao, wanajipigia tu.

Osama alikuwa mwiba sana, hadi Marekani wanamkamata ilikuwa shughuli nzito.

Iran alitegemea zaidi kufanya mashambulizi kwa Proxies kama Hamas, Hezbolah, Houthi, Vikundi vya Iraq na Syria.

Iran kupigana Direct ni mchovu sana, Iliwachukua Israel na Marekani SEKUNDE 60 tu kuwafyeka Ayatollah na viongozi wengine wakubwa wa jeshi.

Hadi sasa wiki bado haijaisha ila mifumo ya ulinzi wa Iran ipo nyanga nyanga si rada wala meli, leo hii ndege ya kivita ya Iran iliyotaka kujaribu kupigana na F 35 za Israel imepigwa angani punde tu ilipopaa.

Na vita inazidi kuwa nyepesi kwasababu wananchi wengi wapo upande wa Marekani na Israel, wanaona wanakombolewa sio vita hii.
Jidanganye.
 
Bado upo mweupe na unaongozwa na mahaba na hisia pia hutumii akili kufikilia. Alafu aliye Bahamas ni huyo gaidi alitengenezwa na CIA. Irani silaha zake ni 90% uzalishaji wa ndani hio 10% ndio anaagiza nje tena ni kujua teknolojia iliyopo na kuzitumia as strategic tu nasio tegemezi kwa ulinzi.

Alafu kumua ayatollah sio kigezo cha kushinda vita na kubadilisha mfumo wa uongozi hivyo bado nakuambia upo mweupe kwenye siasa za mashariki ya kati. Wew hata nikikuliza ni kwanini Zimbabwe na umasikini wao wote kwanini serikali yao imekataa msaada wa afya wa Dola za Marekani milioni 367 kutoka Washington. Lazima utanijibu kwa hoja za kitoto na nikikuambia the reason behind utasema hizo ni story za vijiweni zisizo na ushahidi.
Wewe ndio mweupe, hata hujui Edward Snowden yupo Urusi, hayupo Bahamas.

Edward Snowden has been living in Russia since 2013, where he was granted permanent residency in 2020 and Russian citizenship in 2022
 
Jidanganye.
Hivi unajua hata yai haliivi ndani ya sekunde 60 zilizotumika kumbamiza Ayatollah na mawaziri wa ulinzi ?

Ndo utamlinganisha na Saddam Hussein, acheni dharau aisee

Yani Marekani na Israel kama kuna sehemu wanatafuta ya kujisifu uwezo wake wa kivita basi ni walichofanya ndani ya SEKUNDE 60
 
Back
Top Bottom