Kula ugali usiku nacho ni kipimo cha umaskini

Kula ugali usiku nacho ni kipimo cha umaskini

The Businessman

JF-Expert Member
Joined
Jan 9, 2014
Posts
7,397
Reaction score
9,263
Ugali ni chakula kizito na digestion yake inafanyika taratibu hivyo matokeo yake digestion haiishi, chakula kinachacha na kuwa kigumu.

Ugumu wa chakula unafanya utumbo kukakamaa na hivyo kuongeza mgandamizo kwenye "diaphram' akili ita sence abnormality kutokana na huo mgandamizo.

Kwa kuwa umelala abnormality ndio hapa watu wanaanza kuota ndoto za ajabu na kuamka asubuhi wamechoka wakisingizia wachawi.

Usiku tunatakiwa tule chakula laini( tambi, wali, viazi, magimbi na ndizi) ila kwa sababu ya hali zetu za kimaskini wengine hatumudu hivyo vyakula hivyo ni mwendo wa ugali na maharage mbaya zaidi tunakula kiwango kile kile kama cha mchana.

Hii nayo ni aina ya umaskini kama umaskini mwingine! .
 
Si kweli,mtu ambaye hana shida anatakiwa ale chakula anachojisikia kula,na kula hakuna idadi,unaweza ukala hata mara nne usiku ni wewe tu kuweza kuamka.
 
Ugali ni chakula kizito na digestion yake inafanyika taratibu hivyo matokeo yake digestion haiishi, chakula kinachacha na kuwa kigumu.
Ugumu wa chakula unafanya utumbo kukakamaa na hivyo kuongeza mgandamizo kwenye "diaphram' akili ita sence abnormality kutokana na huo mgandamizo.

Kwa kuwa umelala abnormality ndio hapa watu wanaanza kuota ndoto za ajabu na kuamka asubuhi wamechoka wakisingizia wachawi.

Usiku tunatakiwa tule chakula laini( tambi, wali, viazi, magimbi na ndizi) ila kwa sababu ya hali zetu za kimaskini wengine hatumudu hivyo vyakula hivyo ni mwendo wa ugali na maharage mbaya zaidi tunakula kiwango kile kile kama cha mchana.

Hii nayo ni aina ya umaskini kama umaskini mwingine! .
Usomi mwiiingi na complications za ajabu lakini bado tunakufa sana tu. Wazee waligonga menyu hizo hizo na bado wakaishi miaka kibao tu ambayo leo hatufikishi licha ya elimu zenu uchwara hizo.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Msiwe wabishi na kumbishia mtoa mada.
Lkn nimrekebishe kidogo mtoa mada.
Sio kweli kwamba kula ugali usiku ni umasikini hilo napinga.
Wapo watu wenye pesa zao na usiku wanakamua ugali daily.
Kilichokosekana hapo ni elimu.
Wataalamu wanasema kuwa chakula kigumu kiliwe mwisho saa 11 jioni.
Yaani wakati unalala usiku tayari mmeng'enyo wa chakula hicho unakuwa umeshakwisha fanyika.
Lkn kama unakula zaidi ya huo muda basi kula vyakula laini kama vile wali,tambi,ndizi,viazi,mtoli nk.
Sasa kwa wale ambao uwezo wa kumudu gharama za vyakula hivyo laini hawana,basi wale huo ugali wao mapema kabla ya kulala.
Huo ndio utaratibu mzuri kasoro elimu ndio bado watu hawana.
 
Msiwe wabishi na kumbishia mtoa mada.
Lkn nimrekebishe kidogo mtoa mada.
Sio kweli kwamba kula ugali usiku ni umasikini hilo napinga.
Wapo watu wenye pesa zao na usiku wanakamua ugali daily.
Kilichokosekana hapo ni elimu.
Wataalamu wanasema kuwa chakula kigumu kiliwe mwisho saa 11 jioni.
Yaani wakati unalala usiku tayari mmeng'enyo wa chakula hicho unakuwa umeshakwisha fanyika.
Lkn kama unakula zaidi ya huo muda basi kula vyakula laini kama vile wali,tambi,ndizi,viazi,mtoli nk.
Sasa kwa wale ambao uwezo wa kumudu gharama za vyakula hivyo laini hawana,basi wale huo ugali wao mapema kabla ya kulala.
Huo ndio utaratibu mzuri kasoro elimu ndio bado watu hawana.
Ndio maana wanaokula vyakula vigumu usiku huota ndoto za ajabu na kuamka wachovu.
 
wabongo bwana mmedanganyana huko kijiweni unakuja kuanzisha thread.. ugali ukishautafuna mdomoni ukashuka tumboni unameng'enywa sawa na hivyo vyote ulivyotaja katika chemical digestion maana zote ni wanga

Sent from my iPhone6 using JamiiForums mobile app
 
Na makande je? maana sie huku kwetu upareni ndio menyu mchana na usiku daily?!
Ninapenda makande yawe na maharage mengi kuliko mahindi na yakolee nazi.

Makonde ya boarding yalikuwa na mahindi mengi mafuta ya kunyunyiza
 
Basi Mimi ni masikini sana, kwa mapenzi yangu na ugali saa yeyote ni ugali time
Nina kakaangu mkewe akipika chakula kingine tofauti na ugali lazima apikiwe ugali wake.

Wengine wanapenda tu ugali wala si kwa sababu ya umaskini. Halafu watafiti wa ugali wamekuwa wengi sana siku hizi kwani wazee wetu walikuwa wanakula nn enzi hizo!!!!
 
Na makande je? maana sie huku kwetu upareni ndio menyu mchana na usiku daily?!
ha ha haa!! mimi kwa kweli kama haujanianadalia/kuandaa ugali usiku siwezi kukuaelewa aisee!!

Hakuna kitu nakipenda kama ugali

Na vitu amabavyosipendi kula usiku ni ndizi, tambi na chips kwa kweli sijawahi kuwa mpenzi wa hivyo vitu.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom