Kujengea makaburi ya Waliotutangulia - Kuna umuhimu wowote?

Kujengea makaburi ya Waliotutangulia - Kuna umuhimu wowote?

charminglady Maandiko yanesamaje juu ya wafu na makaburu? Au Yesu anasemaje juu ya kupamba makaburu?

Muongozo mzuri dada Yangu ni Maandiko Lkn haya mengine yote ni mbwembwe za Dunia hii tu!
 
Last edited by a moderator:
Habari za asubuhi ya leo wapendwa wana Jamvi....

Kwanza niombe radhi kwa nitakaowakwaza kwa namna moja ama nyingine.

Kuna suala hili huwa linanitatiza naomba kuelewesha.

Kumezuka tabia ya kujengea makaburi kwa marumaru ya samani za aina tofauti tofauti tena zenye gharama kubwa, Utakuta mtu alikuwa anaumwa kwa muda mrefu lakini watu hawakujitokeza kumhudumia lakini baada ya mtu huyo kufariki dunia wanajitokeza ndugu, jamaa na marafiki wanapanga mipango ya kujengea kaburi lake na kuweka nakshi ya kila aina.

Je watu hawa walikuwa wapi wakati wa ugonjwa??

Je kujengea kaburi hilo kutamsaidia nini yule marehemu??

Kuna watu wanafariki ghafla aidha kwa ajali ama kifo cha aina yoyote ila kwa ghafla... Kuna ulazima gani wa kulinakshi kaburi???

Tena kuna wengine wamekwenda mbali wakaanza kutafuta makaburi haya ya mababu zao na kuanza kuyajengea na kuyaweka katika hali ya unadhifu kana kwamba kilichomo ndani yake kina thamani... Tena na kufanya sherehe sijui ya kujengea makaburi... Ni nini maana yake???

Kwa mtazamo wangu ujenzi huu wa kuweka nakshi ni kugharamika kusiko na faida...

N.B. Ni mtazamo tu naomba nisipondwe mawe....
Ukweli wa mambo kwanza kujengea kaburi ni kosa haifai ndio maana imani ya kiislamu inakataza kujengea makaburi. Hebu wav wajaribu kutafakari lau wanadamu wote waliokufa huku nyuma wangejengewa kwa masumenti kama baadh ya watu wanavyofanya leo tungekuwa twaishi wapi? Tungelimia wapi?
 
Siamini kama hii topic kweli inajadiliwa.. Seriously? Mtoa mada vipi??? Umenidisturb emotionally
 
Pole sana kwa kutojua thamani ya kaburi. Ila nakufundisha leo.1.ni kuweza kuunganisha ukoo kwa maana kizazi kinapoongezeka watu hutawanyika sehemu mbalimbali hivyo ili ndugu wajuane lazima pawe na aliyeunganisha ukoo je ni nani ni yule babu au bibi aliyekufa miaka mingi na kaburi lake ni hili.2.kuongeza ujasiri na kutoa maonyo kwa kizazi kijacho juu ya mawazo na maono na mafundisho ya mtu aliyefariki aliyoyafanya enzi ya uhai wake kama vile mwl nyerere,mkwawa, yesu na muhamad.3.
 
Mkuu unajua kujengea hakuna shida ila kuweka nakshi, mara marumaru, mara kuweka kivuli ndio shida! kwani ukijenga kawaida kumbukumbu haibaki???

huo ni uamuzi mkuu mi sioni shda hata ukajengea likiwa linameta meta
 
3.kumbuka pia kaburi hualalisha uwenyeji wako wa eneo husika hata ukitiliwa mashaka uraia wako unasema tu jamani mimi ni mzawa hapa mababu na mababu zangu wameishi hapa na nimewazika hapa ebu mkatazame.4. Makaburi ni historia ya kukuwezesha kujua mmetoka wapi mko wapi na mnakwenda wapi. Heshimu makaburi kwa kuyatunza na kuyahifadhi lakini ni vizuri kumjali mgonjwa siyo mpaka afe.
 
Pole sana kwa kutojua thamani ya kaburi. Ila nakufundisha leo.1.ni kuweza kuunganisha ukoo kwa maana kizazi kinapoongezeka watu hutawanyika sehemu mbalimbali hivyo ili ndugu wajuane lazima pawe na aliyeunganisha ukoo je ni nani ni yule babu au bibi aliyekufa miaka mingi na kaburi lake ni hili.2.kuongeza ujasiri na kutoa maonyo kwa kizazi kijacho juu ya mawazo na maono na mafundisho ya mtu aliyefariki aliyoyafanya enzi ya uhai wake kama vile mwl nyerere,mkwawa, yesu na muhamad.3.
 
Wewe ndin mjinga kabisa! Bila watu kutoa maiti zao zikafanyiwe majaribio na kujifunza hiyo technogy inayotumika kukutibu wewe ingeshushwa kutoka mbinguni? Hiyo CT-scan watu wangeoteshwa na malaika Ng'wana Mashiku?

Mimi pia nafuta mwanasheria wa kunisaidia ili nikifa mwili wapeleke maabara wanafunzi wajifunzie!

Sasa huyo mwanasheria ndo Mzazi wako,si unaweza ukawaambia ndg zako woote na waka i-mark kauli yako,nenda msikiti/kanisa unalo sal+ waeleze kile unachopenda kwisha habari! khs ct-scan hebu nambie miaka 2000b.c ct-scan ilihusikaje.?
Tusijazane ujinga bana! Sio kila unacho comment ndo nikifuate! Na neno lako sii sheria!
 
Yaani swali lako lina maidhi sana. Inawezekana wewe ni mbinafisi na hujali. Wenzio. Kujengea makabir ni utaratibu wa dunia nzima kama namna ya kuenzi wapendwa wao. Its culture which shapes the personality of an individual. So kuna umhimu wake tena sana. Sio tu katika kujifurahisha. Watu wengi wanaamini kuna neema fulani ukijali ndugu zako hivyo hata ulaya pia mwisho wa kila mwaka lazima waende wakajenge makuburi ya ndugu zao. So wewe huelewi tuache sis tujenge wewe kalewe na vijisent vyako
 
Suala la marumaru yaweza kuonekana anasa kwako ila kwa wengine ni kawaida kutokana na ukwasi.......,labda kwako CL ikoje kwa makaburi ya wapendwa wako (hasa hasa kama ni wazazi wako-samahani kama wapo hai )


Hauna haja ya kusema samahani, ni kweli nilimpoteza mzazi mmoja tayari na kaka yangu mkubwa.

But I have nothing to do with their graves.. Hainisaidii na wala haitonisaidia chochote katika.maisha yangu. Walisharudi mavumbini kama lilivyo agizo la Mwenyezi Mungu....
 
Dear CL, kuna issues 3 hapa zihusuzo kujengea makaburi!.

  1. Kuweka Alama- Hii ndio sababu kuu ya kujengea makaburi, ili tuu kuweka mark, nani alizikwa hapa, kaburi lisipotee. Ujenzi wa kuweka alama ni simple na wala hautumii gharama kubwa!.
  2. Kumplease Marehemu!. Watu wanajengea makaburi kwa gharama kubwa ili kujifariji nafsi zao kuwa ndio namna bora ya kumuenzi marehemu!, kwa kadri familia ilivyo na uwezo, ndivyo kaburi la thamani linavyojengwa hadi mengine kuwa kama minara, hivyo kuonyesha jeuri ya pesa.
  3. Kujengea makaburi kama sehemu ya kuabudia!. Hizi ni ibada za wafu!. Kuna makaburi yanajengwa kama shrines kwa watu wa ukoo ule kwenda hapo, kufanya misa, ibada, kumbukumbu hata kutoa makafara ya kiukoo!, hawa ndio wale utasikia hata akifia wapi, lazima akazikwe kwao ili wakafanye mambo yao!.
My take:
Mwili wa binadamu una sehemu kuu mbili, mwili na roho!. Mwili unakufa na kugeuka mavumbi, roho haifi, inadumu milele!. Mwili ukiishakufu, its nothing!, hata wafanyao ibada za wafu kwa kuombea dua miili, kupeleka nyumba za ibada, kusali misa za kumbukumbu za marehemu, kwenda kusali makaburini, kujengea makaburi, au anything to do with a dead body ni ubatili tuu, kwa watu kujifariji na kujifurahisha nafsi zao, a dead body is a dead body!.

Wako wengi wanaofanya ibada za wafu!, hawajijui kuwa hizo ni ibada za mashetani !. Bwana Wetu Yesu Kristu, alituasa
"Waacheni wafu wawazike wafu wao!".

Watu enlightened, wanakuwa wamefunuliwa kuijua kweli, ndio maana wengi wakifa, wanachomwa au kufanyiwa creamation kwa sababu the deadbody or lifeless body is nothing at all!. Kwenda kusali makaburini ni ibada za kishetani kwa kujua au kutojua!.

Mtu anayetoa mwili wake kufanywa cadaver is better of kuliko ule mwili, uliovishwa vito vya dhahabu na almasi, ukazikwa kwenye jeneza la kioo, alminium au la mbao lilitengenezwa vizuri na kupabwa sana hadi maua!, kisha kaburi likajengwa na marumaru, granite, tiles, etc ili lipendeze machoni, what befals that body huko ulimo, its the same!.

Pasco

Kaka Pasco nakushukuru sana kwa ufafanuzi wako maana nilikaribia kupondwa mawe hapa...

Hizo sehemu nilizoweka red ndio maana ya huu uzi...

Barikiwa sana.....
 
Last edited by a moderator:
charminglady Maandiko yanesamaje juu ya wafu na makaburu? Au Yesu anasemaje juu ya kupamba makaburu?

Muongozo mzuri dada Yangu ni Maandiko Lkn haya mengine yote ni mbwembwe za Dunia hii tu!

Mkuu Ntuzu nimesoma maandiko ndio maana nimekuja na hii mada... Hebu pitia vifungu hivi utaona ni nini kinasemwa hapa juu ya hili...

Imeandikwa Mhubiri 9:5-6, 10Kwa sababu walio hai wanjua ya kuwa watakufa lakini wafu hawajui neno lolote wala hawana ijara tena maana kumbukumbu lao limesahauliwa mapenzi yao namachukio yao na husuda yao imepotea yote pamoja wala hawana sehemu tena katika jambo lolote lililofanyika chini ya jua, lolote mkono wako utakapolipata kulifanya ulifanye kwa nguvu zako kwa kuwa hakuna kazi wala shauri wala maarifa wala hekima huko kuzimu uwendako wewe."
 
Last edited by a moderator:
Mkuu Ntuzu nimesoma maandiko ndio maana nimekuja na hii mada... Hebu pitia vifungu hivi utaona ni nini kinasemwa hapa juu ya hili...

Imeandikwa Mhubiri 9:5-6, 10Kwa sababu walio hai wanjua ya kuwa watakufa lakini wafu hawajui neno lolote wala hawana ijara tena maana kumbukumbu lao limesahauliwa mapenzi yao namachukio yao na husuda yao imepotea yote pamoja wala hawana sehemu tena katika jambo lolote lililofanyika chini ya jua, lolote mkono wako utakapolipata kulifanya ulifanye kwa nguvu zako kwa kuwa hakuna kazi wala shauri wala maarifa wala hekima huko kuzimu uwendako wewe."



Ata Yesu alisema mnapamba makaburu Lkn ndani kuna mizoga na mifupa tu!

Kwahiyo kupamba Kwa kuyajengea haifai! Muongozo Wa Maandiko unatosha kutuongoza ktk hili!
 
Last edited by a moderator:
Ni vizuri kujengea kwa ajili ya kumbukumbu. Fikiria mzazi aliyefariki akaacha watoto wadogo wakija kukua wataonyeshwa kuwa pale ndipo alizikwa mzazi wenu ukiliacha tu ule udongo utasambaratika na kaburi halitoonekana tena.
Nakshi kwenye ujenzi sasa inategemea na uwezo wa familia husika,wakati wewe unaona kuweka tiles ni gharama kuna wanaoona huo ndio ujenzi wa kawaida kabisa. Hata nyumba tunazoishi zinatofautiana thamani kutegemeana na uwezo wa wanafamilia.
 
Ata Yesu alisema mnapamba makaburu Lkn ndani kuna mizoga na mifupa tu!

Kwahiyo kupamba Kwa kuyajengea haifai! Muongozo Wa Maandiko unatosha kutuongoza ktk hili!

msisome maandiko machache mka generalize vitu watu wanajengea ukumbusho wa watu wao sioni kosa mi kwangu lazma yajengewe na ni msomaji mzuri wa biblia
 
Hauna haja ya kusema samahani, ni kweli nilimpoteza mzazi mmoja tayari na kaka yangu mkubwa.

But I have nothing to do with their graves.. Hainisaidii na wala haitonisaidia chochote katika.maisha yangu. Walisharudi mavumbini kama lilivyo agizo la Mwenyezi Mungu....

Haya mama..........umesema kweli yako.........na hiyo ni imani yako ni muhimu kuwa huru!
 
msisome maandiko machache mka generalize vitu watu wanajengea ukumbusho wa watu wao sioni kosa mi kwangu lazma yajengewe na ni msomaji mzuri wa biblia



Ukumbusho Wa nini? Ok tumetumia mstari mmoja wewe uko wapi Wa kwako uliouleta kutetea hoja yako?

Teh Teh Teh Teh
 
Ata Yesu alisema mnapamba makaburu Lkn ndani kuna mizoga na mifupa tu!

Kwahiyo kupamba Kwa kuyajengea haifai! Muongozo Wa Maandiko unatosha kutuongoza ktk hili!

Kidogo kidogo, unashangaa na wewe kupitia mstari huo unaanzisha kanisa.............mara linakuwa kubwa unakula vichwa, watu kibao wamefanikiwa kwa kutafsiri vifungu katika Biblia...................pambana mdogo wangu..........go......go............gooooooooo!
 
Hakuna haja ya kujengea kaburi. akifa amekufa, hana ijara tena chini ya jua. unajifunza nini ktk kaburi?. jiulize huyo mpendwa wako tangu afe alisha kusaidia nini?. kwa MKIRISTO huu ni upagani.
 
Back
Top Bottom