Kuishi Mbezi Kimara ni laana?

Kuishi Mbezi Kimara ni laana?

Baada ya kuona hali inakuwa ngumu kila kukicha nimeamua kutangaza kuuza nyumba. Na wakati huu nimehamia hapa mbezi tangi bovu.

Mbezi kimara sitaki tena hata unipe kiwanja bure sijengi. Nilikata tamaa siku nilipotoka mwenge saa 11 jioni nikafika nyumbani saa sita usiku!!!!

Wachaga endeleeni kukaa huko na mkiendelea kupambana na laana hiyo.


........aaah mazee acha masikhara!......hiyo ni balaa aisee....
 
Laana bado inaendelea. Nipo ova tangia 11. 30 alfajiri tumefungana hakuna anayeenda mjini wala mbezi. Tumezima magari tunaangaliana. Mvua zinazonyesha hatuwezi pita goba kwa wenye magari ya chini. Duh kweli tutafika kwa mtindo huu?
 
kuishi huko sio laana ila ufahamu wenyeww hawaishi huko....jipange
 
Laana bado inaendelea. Nipo ova tangia 11. 30 alfajiri tumefungana hakuna anayeenda mjini wala mbezi. Tumezima magari tunaangaliana. Mvua zinazonyesha hatuwezi pita goba kwa wenye magari ya chini. Duh kweli tutafika kwa mtindo huu?

Poleni sana. Hawa jamaa ni janga. Diversions zote wameziziba, kiasi kwamba kila mwenye gari analazimika kupita njia kuu ambako nako wamebana sana.
 
malori yasiingie jijini Dar hapo tu ndo tunaweza pata suluhisho.

wajengewe ICD huko chalinze makontena yapelekwe kwa treni hiyo itakuwa win win solution, maana wenye biashara ya malori wataendelea kupiga pesa na sie wakazi wa Dar foleni zitapungua.
Treni nayo itasababisha jam kwenye Railway Crossing
 
Laana bado inaendelea. Nipo ova tangia 11. 30 alfajiri tumefungana hakuna anayeenda mjini wala mbezi. Tumezima magari tunaangaliana. Mvua zinazonyesha hatuwezi pita goba kwa wenye magari ya chini. Duh kweli tutafika kwa mtindo huu?

hili nalo tatizo....sometime madereva mnaongeza foleni mara mbili kwa sababu ya 'ujanja wenu'...
 
Wadau wa jf jana nilikua naelekea mbez nilianzia safari yang mwenge saa kumi na nusu jion, baada ya kuvuka tu taa za ubungo nikakutana na jam ya ajabu gar haziend mbele wala nyuma. Nililala nikaamka ndan ya gar lakin ndo kwanza nipo rombo. Nilifika mbezi saa nne na robo usiku. Matukio haya ni ya kila mara sasa kwenye barabara hii. Mapungufu ni meng kuliko faida kwa sasa. Barabara ni nyembamba sana kupitisha gari mbili hasa ikitokea ajali,hata kama barabara ikikamilika hii kero sitegemei kwisha. Mpaka hapo wadau nataka kujua kuishi Mbezi kimara ni Laana?

Kigamboni ndio habari ya mujini sasa ivi.
 
Wanajenga daraja sasa hivi kwa hiyo baada ya daraja kuisha mambo yatakua mazuri. Tatizo kila kitu wamesiasisha ndio maana miundo mbinu itabaki kuwa janga la kitaifa .

Nasi uku foleni itaisha endapo wataboresha miundombinu...kuhama siyo suluhu....ila tunahitaji wahusika watatue hili janga....
 
Tangu saa mbili asubuh leo nipo hapa mbez kituon hamna daladala inayokuja kwenda mjin na ikija inapitia njia ya goba nauli sh.2000. Namuunga mkono mtoa mada Lorin kwamba kukaa mbezi kimara ni laana tena laana kumu.
Mbezi ukiwa kapuku kama mimi mji unazidi kuuona mchungu maanake licha ya kero ya usafir nilazima pia uwe na pesa isio ya mawazo,huku nauli za sh 2000 mbezi kwenda kariakoo au mwenge ni kawaida. Tumelalamika sana hakuna msaada.
Ndio maana mi nasema kuishi mbez kimara Ni LAANA KUMU.
 
Tangu saa mbili asubuh leo nipo hapa mbez kituon hamna daladala inayokuja kwenda mjin na ikija inapitia njia ya goba nauli sh.2000. Namuunga mkono mtoa mada Lorin kwamba kukaa mbezi kimara ni laana tena laana kumu.
Mbezi ukiwa kapuku kama mimi mji unazidi kuuona mchungu maanake licha ya kero ya usafir nilazima pia uwe na pesa isio ya mawazo,huku nauli za sh 2000 mbezi kwenda kariakoo au mwenge ni kawaida. Tumelalamika sana hakuna msaada.
Ndio maana mi nasema kuishi mbez kimara Ni LAANA KUMU.

Hahaaaa Rangoz umetisha. Pole sana na tushirikiane kuitoa hii serikali madarakani maana naona hawajali kabisa matatizo yanayoikabili nchi.
 
Stahmilini saana mbona hamna subira jamani.cc Wa Mbagala tuliteseka tokea zama za mwalimu.mpaka mkapa.kidogo ahuweni sasa.muwe na subira mbona Barbara imeshaanza kuchukua sura
 
Kupanga nyumba Kimara ni sh 100,000/- kwa mwezi kwa nyumba ya vyumba vinne. Utasemaje ni laana?
 
Hii barabara jaman. Hebu jiulize ni watu wangap wanapoteza maisha yao wakiwa kwenye magar kwenda hospital lakin sababu ya jam/ folen wanakosa huduma ya haraka wanafia njian.
 
Wadau wa jf jana nilikua naelekea mbezi nilianzia safari yangu Mwenge saa kumi na nusu jioni, baada ya kuvuka tu taa za Ubungo nikakutana na jam ya ajabu gar haziendi mbele wala nyuma.Nililala nikaamka ndan ya gari lakin ndo kwanza nipo Rombo.

Nilifika Mbezi saa nne na robo usiku.

Matukio haya ni ya kila mara sasa kwenye barabara hii. Mapungufu ni meng kuliko faida kwa sasa. Barabara ni nyembamba sana kupitisha gari mbili hasa ikitokea ajali,hata kama barabara ikikamilika hii kero sitegemei kwisha. Mpaka hapo wadau nataka kujua kuishi Mbezi kimara ni Laana?

kama vp jaribu kupitia barabara ya chuo cha ardhi upitie Goba afu uta evaluate alternative mwenyewe by weighted average time samahani kidhungu haha
 
Jana ilikuwa balaa tupu, nilikuwa kariakoo mida ya saa kumi jion natafuta gari ya kurud Mbezi, nilipata tabu sana kwanza kituo cha magari ya kwenda mbez hamna,mvua inanyesha ikabid nichape lapa mpaka jangwan ndio nikapata gari mbezi \muhimbili nigeuze nalo. Sinema haikuishia hapo kulikuwa na jam balaa gari haziendi. Mpaka kufika nyumbani mbezi ni saa tatu usiku hoi taaban. Kuishi huku kwetu shamba ujiandae na adha zote.
 
Jana ilikuwa balaa tupu, nilikuwa kariakoo mida ya saa kumi jion natafuta gari ya kurud Mbezi, nilipata tabu sana kwanza kituo cha magari ya kwenda mbez hamna,mvua inanyesha ikabid nichape lapa mpaka jangwan ndio nikapata gari mbezi \muhimbili nigeuze nalo. Sinema haikuishia hapo kulikuwa na jam balaa gari haziendi. Mpaka kufika nyumbani mbezi ni saa tatu usiku hoi taaban. Kuishi huku kwetu shamba ujiandae na adha zote.
Pole sana Mkuu, nikuhabarishe adha za namna hiyo zinapunguza uhai (umri wa mtu) !! yaani siku 365 x saa 6 kupoteza ktk misononeko inapelekesha kupata magonjwa kadhaa!!
Pole tena...
 
siyo sehemu ya kuishi huko bora ya Gongo LA mboto
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom