Carina
Senior Member
- Jan 4, 2011
- 194
- 71
Wadau wa jf jana nilikua naelekea mbez nilianzia safari yang mwenge saa kumi na nusu jion, baada ya kuvuka tu taa za ubungo nikakutana na jam ya ajabu gar haziend mbele wala nyuma. Nililala nikaamka ndan ya gar lakin ndo kwanza nipo rombo. Nilifika mbezi saa nne na robo usiku. Matukio haya ni ya kila mara sasa kwenye barabara hii. Mapungufu ni meng kuliko faida kwa sasa. Barabara ni nyembamba sana kupitisha gari mbili hasa ikitokea ajali,hata kama barabara ikikamilika hii kero sitegemei kwisha. Mpaka hapo wadau nataka kujua kuishi Mbezi kimara ni Laana?
Kwa kweli hii barabara sasa hivi ni Kimeo! Magufuli na Mwakyembe pls ingieni kati! Wananchi tunateseka sana na hizi foleni! Nani mwenye namba za hao watu tuwaandikie hata kaSMS!
Inakera na kuchosha! Kama huna safari ya maana ni bora ukae nyumbani kwako tu balaa tupu hii!
Barabara zote za michepuko imefungwa kuanzia Kimara Mwisho, Korogwe, Bucha, Baruti, Kona, Rombo, yaan hakuna sehem za kuingilia. Mbaya zaidi kwa wakazi ambao wako upande wa juu ya barabara wanalazimika kupitia eidha chuo au jeshini huku ambako barabara ni mbaya sana hakuna routine maintenance, kwa sisi wenye vigari kama Corolla, Carina, Corona sijui MarkX, Mark II, GX100 au GX110 kwa kweli ni balaaa kupita huko. Na hizi mvua .................