Kuishi Dar haimaanishi wewe mjanja

Kuishi Dar haimaanishi wewe mjanja

Jana nilikuwa kariakoo nyuma ya china plaza sijui inaitwaje ile mitaa ila ni karibu na Agrey.... ebwana mvua imenyesha kuna maji machafu yametwama barabarani yanatoa harufu kali kweli utafikiri watu wametapisha vyoo, nilikaa pale kwa muda wa saa moja ila nilipata mateso makali sana sio kwa harufu ile, nilijikuta nawahurumia wafanya biashara wa lile eneo, halafu cha kustaajabisha zaidi nikawaona wengine eti wanakula na chakula kabisa licha ya harufu kali iliyokuwepo pale.

Kiukweli huu mji ni mchafu sana unatia kinyaa, ukitaka kuona hilo subiri kipindi cha mvua.
🤣🤣🤣Pole sana Huwa wanatabia ya kutapisha machemba ya vyoo mvua inyeshapo huoni maji yalivyo na rangi nyeusi na harufu juu
Sasa jichanganye kipindi cha mvua uvae viatu vya wazi utarudi na fangasi zisizotibika
 
Dar mlituoshea sana zamani hizo miaka ya 97-98 😁😁 sasa hivi wala hamtushtui bro, nakumbuka mlikua mna kuja na zile game boys zenu, ili kuzishika tu mnatuambia tukaoge kwanza na kuvaa nguo mpya😁😁😁
hawa wajinga walituoshea sana miaka ya late 90s na early 2000s, yaani ilikuwa kuishi dar ni kama huko peponi..

Mimi nakumbuka wakati bado ni madogo kitaani kwetu ilikuwa mtu akienda Dar likizo, siku akirudi anawakusanya rafiki zake wote karibu mtaa mzima anaanza kuwapa mastori ya kuhusu jiji la dar jinsi alivyokutana na akina Dully Sykes, Professor Jay sijui Mr.Nice alivyoogelea baharini, anawaonesha na picha aliyopiga kwenye ile sanamu ya askari pale posta...!! Basi hapo kila mtu anapata shauku kweli ya kutaka kufika kwenye jiji la makamba.
 
🤣🤣🤣Pole sana Huwa wanatabia ya kutapisha machemba ya vyoo mvua inyeshapo huoni maji yalivyo na rangi nyeusi na harufu juu
Sasa jichanganye kipindi cha mvua uvae viatu vya wazi utarudi na fangasi zisizotibika
Kumbe ndio michezo yao? Mimi nikajua hiyo tabia iko uswahilini huko manzese na kwingineko, kumbe hadi kariakoo na yale magorofa yao?

Aisee na kweli maji ni meusi kweli mpaka unajiuliza, huu uchafu ni wa nini...!? Kweli hili jiji la waswahili.
 
👉Harufu za shombo ya supu ya pweza
👉Harufu za kondomu zilizotumika kila gesti yenye 😅dada poa
👉Harufu ya uduvi
👉Harufu za bhangi na shisha
👉Harufu ya jasho la kwenye daladala
👉Harufu ya makombo ya supu za mabaki ya makongoro
👉Harufu ya visamaki vya mbususu za kushare
👉Harufu za mashoga Kmmke mbona mtihani🥶🙌

Hii combo ya minuko=mnuko promax
Umesema vyema

Plus harufu ya mitaro ya maji machafu yaliyotuama mitaani

Mashimo ya choo yaliyojaa mpaka yanafurumia mavi

Chamber zinazovujisha mchuzi wa mavi barabarani

Dar ni dampo kmmmk
 
Kumbe ndio michezo yao? Mimi nikajua hiyo tabia iko uswahilini huko manzese na kwingineko, kumbe hadi kariakoo na yale magorofa yao?

Aisee na kweli maji ni meusi kweli mpaka unajiuliza, huu uchafu ni wa nini...!? Kweli hili jiji la waswahili.
Kukaa au kuishi kwenye maghorofa si kipimo cha ustaarabu
Sijui ndio kukwepa gharama huko wanaona bora wayafungulie yaende na maji
 
Hizi mentality za watu wa hovyo...Kumkandia au kuwa na chuki kisa ukanda...na ww si uende Dar mzee uache majungu.
NA huyo anayejiona mjanja kisa anakaa Dar nae ni mbumbumbu tu.
Hellow

Kuna watu wana jiaminisha kuwa hawewezi kutapeliwa wala hakuna asichokijua kwasababu tu anaishi dar ni uongo

Kuna watu wamezaliwa dar na wamekulia hapo ila wanatapeliwa kila siku na kuibiwa kijinga sana sasa wewe wa mkoa umeenda dar kwasababu tu ya kazi unajiona mjanja subiri wakuingize mjini

Na watu wa dar wengi wanajiamin kuwa wanajua kuvaa yaan wanaenda na wakati uongo sio wote ukitembea utakutana na vituko vingi sana kiasi hukutegemea kabisa

Kuishi kwako dar haimaanishi unajiweza uongo wengi dar wanaishi maisha ya kawaida sana tena kama mgeni usikimbilie kununua gar itakutesa mkuu

Kuishi kwako dar sio kwamba dar yote unaijua no kuna njia zingine uzijui kuwa mpole punguza ujuaji utashindwa saidiwa
 
Back
Top Bottom