Wewe hulipi kodi au siyo?Mbona wewe unatapeliwa kila siku... maana hela zako unazolipa kodi sie tupo bize tunanunua wapinzani...
Wewe hulipi kodi au siyo?Mbona wewe unatapeliwa kila siku... maana hela zako unazolipa kodi sie tupo bize tunanunua wapinzani...
nalipa kodi kwa mujibu wa sheria.. ila kutapeliwa natapeliwa kwa style hiyo sasa cjui ww unakwepa vipi kutapeliwaWewe hulipi kodi au siyo?
Balaa...!Pole sana dada.
Aisee kofi kama panga? Hawa watu hawa kiboko.
Watu wengi wanaoibiwa simu kwenye daladala mara nyingi huwa wameweka earphone.
Haa ha...na alieibaa hukumuonaa
Sio Mche, kipande tuha ha haah daah huu uzi nimecheka sana,nahisi utakuwa mrefu sana,sibanduki,ngoja nijibanze hapa nicheke niongeze siku za kuishi,ila huyo aliyeibiwa na kuwekewa mche wa sabuni katisha kuliko wote!
Haaaaa vipi jamaa walikuwa wako njemaaa ? Vipi huku toa nakoz?kuna sehemu... mchana wahuni wanapiga tizi.. (mazoezi ya ngumi).. alaf usiku wanakaba.... mie nikawa nimewasoma... kuna siku natoka zangu Maeneo ya kujidai... nipo mwenyewe... mkononi nimeshika kibegi kina pc.. maana nilivyotoka chuo nikapitia maeneo.. sasa ile nakatisha vichochoro saa 6 usiku.. nikakutana na jamaa kama watatu hivi.. hawajashika silaha wala nini.. mie kama kawaida yangu uskiu huwa napasua katikati... ya watu (kama wamekaa kimstari)... sasa ile nakaribia kuwafikia wakasimama... mie sina habari hapo najua wahuni tu na mambo yao... nikashangaa mmoja ananiambia "oya.. unaziweza??? kama hautuwezi tuachie kila kitu ondoka... kama unatuchukulia kinyonge njoo tupambane.."
kucheki.. huku na huko.. kimyaa... sisi tu... nikasema kimoyomoyo leo afe kipa afe beki... kitaeleweka...
nikachukua kibegi changu nikakivaa.. fresh.. (mkono mmoja)... aisee zilipigika ngumi pale..... hahahahahaha narudi nyumbani suruali nimeipasua katikati... kiatu kimabanduka soli.. pc imeweka crack katika kioo.... hahaha daah nimekumbuka mbali..
Muhindi unagombania daladalaMimi ilibaki kidogo teja anichomolee simu huku nagombania daladala maeneo ya mwenge. Machale yalinicheza kugeuka nyuma naona mtu kachomeka vidole kwenye mkoba nilimkata jicho alivyozuga nikabaki kucheka.

Haa ha ha...Aaha mzee hawakuwa na silaha maana??kuna sehemu... mchana wahuni wanapiga tizi.. (mazoezi ya ngumi).. alaf usiku wanakaba.... mie nikawa nimewasoma... kuna siku natoka zangu Maeneo ya kujidai... nipo mwenyewe... mkononi nimeshika kibegi kina pc.. maana nilivyotoka chuo nikapitia maeneo.. sasa ile nakatisha vichochoro saa 6 usiku.. nikakutana na jamaa kama watatu hivi.. hawajashika silaha wala nini.. mie kama kawaida yangu uskiu huwa napasua katikati... ya watu (kama wamekaa kimstari)... sasa ile nakaribia kuwafikia wakasimama... mie sina habari hapo najua wahuni tu na mambo yao... nikashangaa mmoja ananiambia "oya.. unaziweza??? kama hautuwezi tuachie kila kitu ondoka... kama unatuchukulia kinyonge njoo tupambane.."
kucheki.. huku na huko.. kimyaa... sisi tu... nikasema kimoyomoyo leo afe kipa afe beki... kitaeleweka...
nikachukua kibegi changu nikakivaa.. fresh.. (mkono mmoja)... aisee zilipigika ngumi pale..... hahahahahaha narudi nyumbani suruali nimeipasua katikati... kiatu kimabanduka soli.. pc imeweka crack katika kioo.... hahaha daah nimekumbuka mbali..
Machalii wakakuingiza mjini...duuh Ofisii ilikuelewaa kweli?!!Dahh walinitoa laki 3 kweny wallet nimetoka kuchukua hesabu ya Jioni ofsn hakika walinibakishia buku niliyoweka kweny mfuko wa shati namshukuru Mungu hyo buku ilinisaidia kwenda nyumbn .
Toka siku hyo sijapanda hais tena kama usafir Wang unashida aheri nichukue Toyo.
Machalii arusha mnatabia mbaya sana ila nishawasamehe.
Ukaamua utoe sadakaa walet...haa ahWashanikosa pale external kituoni wakati wa kupanda daladala la tabata segerea
Nimetoka chuga nikashukia ubungo mataa mida ya usiku nikachomoa wallet nikatoa pesa zote nikaacha ATM card na ID
Nimekaa kituoni daladala ikaja nikaanza kuparangana ili nipande Mara nasikia simu inachomolewa mfukoni
Nikazuia mkono ila kuzuia nasikia kwa nyuma wallet inachomolewa sikua na jinsi kwa sababu mkono mmoja nimeshikilia rasket mwingine nimezuia simu
Ikabidi nivumilie tu wallet ikaenda na wahuni ila pesa hawakupata
Wanaume ndo mnaongoza kuibiwa sababu mnajiamini kupitiliza
Na ushamba wangu wa jiji lakini nilinusurika sikuibiwa kabisa, kwanini nyie wenyeji??????
Kuna siku kariakoo mida ya kumi na moja jioni tunasukumana kupanda daladala ebwana eh kuna jamaa anasisitiza tuwe makini na simu zetu kumbe ndo jizi nageuka hivi nakuta mkono wake kauzamisha katika pochi yangu nikasema we kaka umeniibia hapo gari ishaanza kuondoka sasa mi mguu mmoja upo garini mwingine unaning'inia chini kama nimedandia flani hivi
Wakati huo nimeshahamaki na kasimu kangu kapya kabisa kalikuwa na wiki tu nimekanunua laki nne
Nikafanikiwa kuzama ndani salamu ya kwanza kukagua kama imo .......nikaikuta huku abiria wengine wakinipongeza kuponea katika tundu la sindano
Ila nina uhakika kabisa nisingeikuta kingenikuta kama cha huyo paka hapo mi ningelia kabisa sio kuvunga na kamasi wangeziona wadau hahahahaha kibaka alinitukana siku hiyo.......wooooooooiii



Laki NNE ingesepa kiutani utanii...Wahuni wakishaamua kufanya mambo yao huwezi kuwazuiaUkaamua utoe sadakaa walet...haa ah
Bora uwe mpole ukijifanya mjanja utakwenda komboWengine wanakuwa na visuu kabisa
Acha tu ndugu yanguLaki NNE ingesepa kiutani utanii...
Mie huo mchezo nlitaka kufanyiwa pale karikoo kwenye ghorofa la wachina, teja kaja na smartphone matata sana nikaitamani tukakubaliana nimpe elfu 40,lkn machale yakanicheza kwamba hapa huenda ana wenzake nikitoa tu hela naitiwa mwizi akafu nanyanganywa cm na hela nmetoa.Mimi nilikua naskia simu kuwa sabuni,nilikua nawadharau wanaoibiwa.
Mwaka flani hivi nilipita pale kariakoo teja akanionesha simu kali ilikua Huawei.Nikajisemea moyoni ngoja nione hawa maboya huwa wanaiba vipi,nikamvuta pembeni.
Niliikagua simu zaidi ya mara 5,ipo fresh tukakubaliana nimpe 22,000/=.Nilizingatia hatua zote ili nisipigwe,simu nilikua nayo nikampa ela lakini alinilazimisha niiweke kwenye baasha yake sababu watu wataiona.
Nilihakikisha abadilishi kitu,mara tu alivyo nipa nilitoka nduki ghafla nikaanza kukimbizwa na watu wengine wawili lakini nikasikia sauti ya yule teja akisema muacheni.
Nilipanda daladala bila kujua linaelekea wapi huku nikijiona nimewakomesha.Gari ilivyofika muhimbili nikaona ngoja niiangalie simu yangu niliyojipatia bila jasho.
Duuuh,Sikuamini macho yangu....kukuta kipande cha sabuni.
Wale huwa wanatumia NDUMBA


