Kuibiwa kwenye Daladala

Kuibiwa kwenye Daladala

Watu wengi wanaoibiwa simu kwenye daladala mara nyingi huwa wameweka earphone.

Lilikua funzo lile, ila kosa langu siku hiyo nlikua nimebeba na hela katika mfuko Mwingine kwaiyo akili yangu nilizingatia hela zaidi ya simu
 
Haa ha...na alieibaa hukumuonaa

Kuna jamaa nilimuona nikamuhisi maana alikua kama ameishika kwa nyuma hivi, ila mimj Sasa ile akili ya haraka haraka kujua kua nimepigwa yaani Kama nilipagawa fulani hivi, ile nasema nimfatilie tayari kashapotea gizani vichochoroni zamanii
 
ha ha haah daah huu uzi nimecheka sana,nahisi utakuwa mrefu sana,sibanduki,ngoja nijibanze hapa nicheke niongeze siku za kuishi,ila huyo aliyeibiwa na kuwekewa mche wa sabuni katisha kuliko wote!
Sio Mche, kipande tu
 
kuna sehemu... mchana wahuni wanapiga tizi.. (mazoezi ya ngumi).. alaf usiku wanakaba.... mie nikawa nimewasoma... kuna siku natoka zangu Maeneo ya kujidai... nipo mwenyewe... mkononi nimeshika kibegi kina pc.. maana nilivyotoka chuo nikapitia maeneo.. sasa ile nakatisha vichochoro saa 6 usiku.. nikakutana na jamaa kama watatu hivi.. hawajashika silaha wala nini.. mie kama kawaida yangu uskiu huwa napasua katikati... ya watu (kama wamekaa kimstari)... sasa ile nakaribia kuwafikia wakasimama... mie sina habari hapo najua wahuni tu na mambo yao... nikashangaa mmoja ananiambia "oya.. unaziweza??? kama hautuwezi tuachie kila kitu ondoka... kama unatuchukulia kinyonge njoo tupambane.."

kucheki.. huku na huko.. kimyaa... sisi tu... nikasema kimoyomoyo leo afe kipa afe beki... kitaeleweka...

nikachukua kibegi changu nikakivaa.. fresh.. (mkono mmoja)... aisee zilipigika ngumi pale..... hahahahahaha narudi nyumbani suruali nimeipasua katikati... kiatu kimabanduka soli.. pc imeweka crack katika kioo.... hahaha daah nimekumbuka mbali..
Haaaaa vipi jamaa walikuwa wako njemaaa ? Vipi huku toa nakoz?
 
Mimi ilibaki kidogo teja anichomolee simu huku nagombania daladala maeneo ya mwenge. Machale yalinicheza kugeuka nyuma naona mtu kachomeka vidole kwenye mkoba nilimkata jicho alivyozuga nikabaki kucheka.
Muhindi unagombania daladala
 
Wanaume ndo mnaongoza kuibiwa sababu mnajiamini kupitiliza

Na ushamba wangu wa jiji lakini nilinusurika sikuibiwa kabisa, kwanini nyie wenyeji??????

Kuna siku kariakoo mida ya kumi na moja jioni tunasukumana kupanda daladala ebwana eh kuna jamaa anasisitiza tuwe makini na simu zetu kumbe ndo jizi nageuka hivi nakuta mkono wake kauzamisha katika pochi yangu nikasema we kaka umeniibia hapo gari ishaanza kuondoka sasa mi mguu mmoja upo garini mwingine unaning'inia chini kama nimedandia flani hivi

Wakati huo nimeshahamaki na kasimu kangu kapya kabisa kalikuwa na wiki tu nimekanunua laki nne

Nikafanikiwa kuzama ndani salamu ya kwanza kukagua kama imo .......nikaikuta huku abiria wengine wakinipongeza kuponea katika tundu la sindano

Ila nina uhakika kabisa nisingeikuta kingenikuta kama cha huyo paka hapo mi ningelia kabisa sio kuvunga na kamasi wangeziona wadau hahahahaha kibaka alinitukana siku hiyo.......wooooooooiii
 
kuna sehemu... mchana wahuni wanapiga tizi.. (mazoezi ya ngumi).. alaf usiku wanakaba.... mie nikawa nimewasoma... kuna siku natoka zangu Maeneo ya kujidai... nipo mwenyewe... mkononi nimeshika kibegi kina pc.. maana nilivyotoka chuo nikapitia maeneo.. sasa ile nakatisha vichochoro saa 6 usiku.. nikakutana na jamaa kama watatu hivi.. hawajashika silaha wala nini.. mie kama kawaida yangu uskiu huwa napasua katikati... ya watu (kama wamekaa kimstari)... sasa ile nakaribia kuwafikia wakasimama... mie sina habari hapo najua wahuni tu na mambo yao... nikashangaa mmoja ananiambia "oya.. unaziweza??? kama hautuwezi tuachie kila kitu ondoka... kama unatuchukulia kinyonge njoo tupambane.."

kucheki.. huku na huko.. kimyaa... sisi tu... nikasema kimoyomoyo leo afe kipa afe beki... kitaeleweka...

nikachukua kibegi changu nikakivaa.. fresh.. (mkono mmoja)... aisee zilipigika ngumi pale..... hahahahahaha narudi nyumbani suruali nimeipasua katikati... kiatu kimabanduka soli.. pc imeweka crack katika kioo.... hahaha daah nimekumbuka mbali..
Haa ha ha...Aaha mzee hawakuwa na silaha maana??
 
Dahh walinitoa laki 3 kweny wallet nimetoka kuchukua hesabu ya Jioni ofsn hakika walinibakishia buku niliyoweka kweny mfuko wa shati namshukuru Mungu hyo buku ilinisaidia kwenda nyumbn .

Toka siku hyo sijapanda hais tena kama usafir Wang unashida aheri nichukue Toyo.

Machalii arusha mnatabia mbaya sana ila nishawasamehe.
Machalii wakakuingiza mjini...duuh Ofisii ilikuelewaa kweli?!!
 
Washanikosa pale external kituoni wakati wa kupanda daladala la tabata segerea

Nimetoka chuga nikashukia ubungo mataa mida ya usiku nikachomoa wallet nikatoa pesa zote nikaacha ATM card na ID

Nimekaa kituoni daladala ikaja nikaanza kuparangana ili nipande Mara nasikia simu inachomolewa mfukoni

Nikazuia mkono ila kuzuia nasikia kwa nyuma wallet inachomolewa sikua na jinsi kwa sababu mkono mmoja nimeshikilia rasket mwingine nimezuia simu

Ikabidi nivumilie tu wallet ikaenda na wahuni ila pesa hawakupata
Ukaamua utoe sadakaa walet...haa ah
 
Wanaume ndo mnaongoza kuibiwa sababu mnajiamini kupitiliza

Na ushamba wangu wa jiji lakini nilinusurika sikuibiwa kabisa, kwanini nyie wenyeji??????

Kuna siku kariakoo mida ya kumi na moja jioni tunasukumana kupanda daladala ebwana eh kuna jamaa anasisitiza tuwe makini na simu zetu kumbe ndo jizi nageuka hivi nakuta mkono wake kauzamisha katika pochi yangu nikasema we kaka umeniibia hapo gari ishaanza kuondoka sasa mi mguu mmoja upo garini mwingine unaning'inia chini kama nimedandia flani hivi

Wakati huo nimeshahamaki na kasimu kangu kapya kabisa kalikuwa na wiki tu nimekanunua laki nne

Nikafanikiwa kuzama ndani salamu ya kwanza kukagua kama imo .......nikaikuta huku abiria wengine wakinipongeza kuponea katika tundu la sindano

Ila nina uhakika kabisa nisingeikuta kingenikuta kama cha huyo paka hapo mi ningelia kabisa sio kuvunga na kamasi wangeziona wadau hahahahaha kibaka alinitukana siku hiyo.......wooooooooiii
Laki NNE ingesepa kiutani utanii...
 
Mimi nilikua naskia simu kuwa sabuni,nilikua nawadharau wanaoibiwa.
Mwaka flani hivi nilipita pale kariakoo teja akanionesha simu kali ilikua Huawei.Nikajisemea moyoni ngoja nione hawa maboya huwa wanaiba vipi,nikamvuta pembeni.

Niliikagua simu zaidi ya mara 5,ipo fresh tukakubaliana nimpe 22,000/=.Nilizingatia hatua zote ili nisipigwe,simu nilikua nayo nikampa ela lakini alinilazimisha niiweke kwenye baasha yake sababu watu wataiona.
Nilihakikisha abadilishi kitu,mara tu alivyo nipa nilitoka nduki ghafla nikaanza kukimbizwa na watu wengine wawili lakini nikasikia sauti ya yule teja akisema muacheni.
Nilipanda daladala bila kujua linaelekea wapi huku nikijiona nimewakomesha.Gari ilivyofika muhimbili nikaona ngoja niiangalie simu yangu niliyojipatia bila jasho.

Duuuh,Sikuamini macho yangu....kukuta kipande cha sabuni.

Wale huwa wanatumia NDUMBA
Mie huo mchezo nlitaka kufanyiwa pale karikoo kwenye ghorofa la wachina, teja kaja na smartphone matata sana nikaitamani tukakubaliana nimpe elfu 40,lkn machale yakanicheza kwamba hapa huenda ana wenzake nikitoa tu hela naitiwa mwizi akafu nanyanganywa cm na hela nmetoa.

Mm nikamzidi ujanja nikamwambia twende nikakupie hela kule kwenye jengo la mwalimu nyerere kule ilala
Yani kutoka karikoo hadi ilala ili tukalipane kwamba kule hawezi kuzingua maana kama ana wenzie wamejibanza sehemu hawatupati. Kusikia hivyo akasema wewe huna nia nayo nikamwambia kwaheri bwana.
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom