Kuibiwa kwenye Daladala

Kuibiwa kwenye Daladala

Natoka zangu mkoa, nikaingia Ubungo Terminal SAA mbili usiku,fasta nikakimbilia daladala LA Kariakoo...nikaingia ndani ya gari

gari lilikuwa limejaa...nafasi ikawepo pale mlangoni,nyuma kidogo na dereva..na walikuwa wamesimama wanaume..

wale jamaa waka adjust kama kunipa nafasi nipate kusimama nao...nami nikajibanza nao

nilishukia Manzese,pale Bakhresa...kufika chini tu;nikajisachi mifuko yote hola.!! lakini hela nilikuwa nimeweka mfuko wa nyuma tena 60,000/= haipo

nikajua wale jamaa pale mlangoni pamoja na Konda lao ni moja,ni wezi..

yaani nilikuwa najionaga mjanja ila baada ya kuibiwa na wale jamaa:nilikuwa mdogooo,hata chakula sikuweza kula jioni ilee..
Pole sana
 
Mimi nilikua naskia simu kuwa sabuni,nilikua nawadharau wanaoibiwa.
Mwaka flani hivi nilipita pale kariakoo teja akanionesha simu kali ilikua Huawei.Nikajisemea moyoni ngoja nione hawa maboya huwa wanaiba vipi,nikamvuta pembeni.

Niliikagua simu zaidi ya mara 5,ipo fresh tukakubaliana nimpe 22,000/=.Nilizingatia hatua zote ili nisipigwe,simu nilikua nayo nikampa ela lakini alinilazimisha niiweke kwenye baasha yake sababu watu wataiona.
Nilihakikisha abadilishi kitu,mara tu alivyo nipa nilitoka nduki ghafla nikaanza kukimbizwa na watu wengine wawili lakini nikasikia sauti ya yule teja akisema muacheni.
Nilipanda daladala bila kujua linaelekea wapi huku nikijiona nimewakomesha.Gari ilivyofika muhimbili nikaona ngoja niiangalie simu yangu niliyojipatia bila jasho.

Duuuh,Sikuamini macho yangu....kukuta kipande cha sabuni.

Wale huwa wanatumia NDUMBA[/QU ukiibiwa mara moja unajifunza
 
kipindi hicho nasoma form two.. pale ubungo.. nilienda na bro wangu mmoja hivi kulikuwa na mishemishe.. sasa... wakaja wale wanaouza simu za wizi... ilikuwa ni NOKIA fulani kali kinoma.. nene.. hivi.. sasa kumbe wanazo mbili simu moja ni OG na nyingine ni fake... imetiwa mchanga mbichi katika housing.. sasa tukaingiwa na tamaa.... ilikuwa inauzwa elfu 15..

ishu ilikuwa hivi.. mkono wa kulia katika mfuko aliweka simu og alaf upande wa kushoto aliweka fake.. wakat tunampa hela (tulichanga) akabadilisha .. akatupa ya mkono wa kushoto maana wakati tunaikagua tukajihakikishia ni simu kweli akairudisha mfukoni.. (hapo hatuelewi)... daah tunakuja kushtuka tupo nyumbani... daah.. nilirud na bonge la sime....... mamaeee siku ile ningechinja mtu
 
Huwa wanazikodi izo simu
Haaahaaaa ....


Mi juzi kati teja pale pale round about msimbazi akanionesha samsung kali kinoma anauza 30 elfu....huwaga nasikiaga zile storee zao za sabuni!

Nami nikamvuta pembeni nikatoa hela nikamwambia nipe hiyo simu hela hii hapa ( huku namshikisha mkononi

Akagoma eti mbona na haraka sana nisubiri ainfungie kwenye bahasha ya kaki coz wameiba dukani, nikamwambia nipe hivo hivo mi na pochi naidumbukiza fasta! Duuh teja likagoma akaanza kutukana na kufoka mara akanirushia hela angu ....nikajua huyu boya ntakuwa nimemkamata pabaya! Nikaokota mshiko wangu huku mateja mengine yanacheka huyoo nikasepa!
 
kaka.. wale jamaa wanapiga ngumi sijapata kuona...... nilikuwa narinda uso.. wasiniharibu wakawa wanapiga (guard) mpaka nikawa naachia mikono zinapita puani... alaf walikuwa wanapokezana.. wanakuja wawili double... wanakupiga nyingi nyingi... alaf mmoja anarudi nyuma.. anakuja mwingine.. yule aliyerud nyuma anapumzika... naendelea na wawili... mmoja akichoka,, anarudi nyuma.. hivyo hivyo... na walikuwa wote wanapiga mapigo ya ajabu ajabu.. NINGEKUFA WALLAHI
Hahahahaha

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Wewe kama mimi mkuu, nilipandia ubungo nikashukia Tip Top nlikua nmevaa t shirt fupi kwaiyo simu ilikua inaonekana huku nimechomeka earphones kwa kujiamini kabisa, ile nashuka tu nikasikia Kama navutwa masikio alafu mziki umezima ghafla Sina hili Wala lile najishika mfuko nakutana na paja badala ya simu, asee iliniuma!!
Unavutwa masikio
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom