Kuibiwa kwenye Daladala

Kuibiwa kwenye Daladala

M
mie nimetapeliwa mara moja na hela yenyewe ni ya nyanya tu.. tangia siku hiyo nipo makini vibaya mnoooo.... mie huwa napoteza vitu na sio kuibiwa
Mimi mara moja mara ya pili huyo mtu huwa akiniona ana badili njia nilimsaka miezi 3 nilipompata tulichomtendea Mungu atusamehe tu kisa laki tano ila aliijutia
 
Niliibiwa mkufu wa dhahabu wakati najiandaa kuteremka kutoka kwenye daladala nilihisi ni panga limekata shingo kumbe ni kofi lililonishtua na jamaa kuambaa na mkufu nikiwa namuona. Ni kitambo kdg miaka ya 90+
Pole sana dada.
Aisee kofi kama panga? Hawa watu hawa kiboko.
 
Mimi nilikua naskia simu kuwa sabuni,nilikua nawadharau wanaoibiwa.
Mwaka flani hivi nilipita pale kariakoo teja akanionesha simu kali ilikua Huawei.Nikajisemea moyoni ngoja nione hawa maboya huwa wanaiba vipi,nikamvuta pembeni.

Niliikagua simu zaidi ya mara 5,ipo fresh tukakubaliana nimpe 22,000/=.Nilizingatia hatua zote ili nisipigwe,simu nilikua nayo nikampa ela lakini alinilazimisha niiweke kwenye baasha yake sababu watu wataiona.
Nilihakikisha abadilishi kitu,mara tu alivyo nipa nilitoka nduki ghafla nikaanza kukimbizwa na watu wengine wawili lakini nikasikia sauti ya yule teja akisema muacheni.
Nilipanda daladala bila kujua linaelekea wapi huku nikijiona nimewakomesha.Gari ilivyofika muhimbili nikaona ngoja niiangalie simu yangu niliyojipatia bila jasho.

Duuuh,Sikuamini macho yangu....kukuta kipande cha sabuni.

Wale huwa wanatumia NDUMBA
Mkuu hawatumii dawa ni tekniki tu, ile ukishaishika mara moja weka mfukoni kwako usimrudishie tena wee lipa ela uone kama watakubali, ule mfuko anaoweka ile simu kuna sabuni imefanana vilevile kwa hiyo akitoa mfukoni unaona ndio ile kumbe tayari keshabadilisha.
 
Yaani wale wakati mnajibizana huku mkisukumana wengine wanafanya yao, alkua mpole maana aliona wenzie washamaliza kazi,
Mi walining'iniza mguu mmoja juu huku ananitingisha sana kwa sababu naujua mchezo nkawa nawangalia wale wa pembeni wanaosachi wakasepa na jamaa kaniachia
nililizwa kishamba sana, nimekomaa na mmoja kumbe kuna wenhine walinilia mingo ila ndio kujifunza pia.
 
Hii kitu iliwahi kunikuta, haki nilicheka hadi machozi.
Mimi nilikua naskia simu kuwa sabuni,nilikua nawadharau wanaoibiwa.
Mwaka flani hivi nilipita pale kariakoo teja akanionesha simu kali ilikua Huawei.Nikajisemea moyoni ngoja nione hawa maboya huwa wanaiba vipi,nikamvuta pembeni.

Niliikagua simu zaidi ya mara 5,ipo fresh tukakubaliana nimpe 22,000/=.Nilizingatia hatua zote ili nisipigwe,simu nilikua nayo nikampa ela lakini alinilazimisha niiweke kwenye baasha yake sababu watu wataiona.
Nilihakikisha abadilishi kitu,mara tu alivyo nipa nilitoka nduki ghafla nikaanza kukimbizwa na watu wengine wawili lakini nikasikia sauti ya yule teja akisema muacheni.
Nilipanda daladala bila kujua linaelekea wapi huku nikijiona nimewakomesha.Gari ilivyofika muhimbili nikaona ngoja niiangalie simu yangu niliyojipatia bila jasho.

Duuuh,Sikuamini macho yangu....kukuta kipande cha sabuni.

Wale huwa wanatumia NDUMBA
 
Washanikosa pale external kituoni wakati wa kupanda daladala la tabata segerea

Nimetoka chuga nikashukia ubungo mataa mida ya usiku nikachomoa wallet nikatoa pesa zote nikaacha ATM card na ID

Nimekaa kituoni daladala ikaja nikaanza kuparangana ili nipande Mara nasikia simu inachomolewa mfukoni

Nikazuia mkono ila kuzuia nasikia kwa nyuma wallet inachomolewa sikua na jinsi kwa sababu mkono mmoja nimeshikilia rasket mwingine nimezuia simu

Ikabidi nivumilie tu wallet ikaenda na wahuni ila pesa hawakupata
 
Dahh walinitoa laki 3 kweny wallet nimetoka kuchukua hesabu ya Jioni ofsn hakika walinibakishia buku niliyoweka kweny mfuko wa shati namshukuru Mungu hyo buku ilinisaidia kwenda nyumbn .

Toka siku hyo sijapanda hais tena kama usafir Wang unashida aheri nichukue Toyo.

Machalii arusha mnatabia mbaya sana ila nishawasamehe.
 
kuna sehemu... mchana wahuni wanapiga tizi.. (mazoezi ya ngumi).. alaf usiku wanakaba.... mie nikawa nimewasoma... kuna siku natoka zangu Maeneo ya kujidai... nipo mwenyewe... mkononi nimeshika kibegi kina pc.. maana nilivyotoka chuo nikapitia maeneo.. sasa ile nakatisha vichochoro saa 6 usiku.. nikakutana na jamaa kama watatu hivi.. hawajashika silaha wala nini.. mie kama kawaida yangu uskiu huwa napasua katikati... ya watu (kama wamekaa kimstari)... sasa ile nakaribia kuwafikia wakasimama... mie sina habari hapo najua wahuni tu na mambo yao... nikashangaa mmoja ananiambia "oya.. unaziweza??? kama hautuwezi tuachie kila kitu ondoka... kama unatuchukulia kinyonge njoo tupambane.."

kucheki.. huku na huko.. kimyaa... sisi tu... nikasema kimoyomoyo leo afe kipa afe beki... kitaeleweka...

nikachukua kibegi changu nikakivaa.. fresh.. (mkono mmoja)... aisee zilipigika ngumi pale..... hahahahahaha narudi nyumbani suruali nimeipasua katikati... kiatu kimabanduka soli.. pc imeweka crack katika kioo.... hahaha daah nimekumbuka mbali..
 
Nimewahi kuvunjiwa chumba ila wizi mwingine wote bado
 

Similar Discussions

Back
Top Bottom