Kuhusu Katiba Mpya, CHADEMA sio pekee wenye wananchi

Uncle Jei Jei

JF-Expert Member
Jan 7, 2011
1,684
2,157
Kwa namna Mambo yanavyoenda, viongozi wa CHADEMA wanazidi kukosa njia sahihi za kushughulika na maswala badala yake wanaendelea kuzidisha uanaharakati hata pale harakati zisipohitajika

Kwa watu makini wanafahamu kabisa jambo bora hutokana na fikra tulivu zisizo na purukushani wala marumbano

Kwa mazingira yaliyopo, hoja kuu ya CHADEMA wanataka katiba mpya ili wapate tume huru ya uchaguzi! (Japo yapo mengi lakini hili limeteka mijadala ya viongozi wao)

Sote tunafahamu kuwa katiba ndio msingi wa ujenzi wa Taifa bora! Fundi anapojenga msingi wa nyumba huku anapresha za hapa na pale kutoka kwa Boss wake, familia na njaa tumboni mwake hawezi kujenga msingi uliobora kubeba nyumba imara

CHADEMA wanatakiwa kutumia nafasi hii ya kudai katiba mpya bila vitisho kwa serikali ili waweze kupata faida ya kuwaunganisha wananchi wote bila kujali makundi yao ili wawe kitu kimoja

Mazingira ya Sasa sio yaliyokuwepo miezi kadhaa nyuma. Sasa hivi nchi ina utulivu na watu bado wanampima Rais aliyepo madarakani

Haiwezekani kwa miezi mitatu tu afute yale yooote yaliyoharibiwa na kiongozi aliyekuwepo! Angekuwa amejiuzulu au amepinduliwa hapo labda! Lakini kumbukeni aliyekuwepo amefariki! Anayeingia lazima atajaribu kulinda heshima ya marehemu kwa muda hata Kama alikuwa hakubaliana nae

CHADEMA wasitake kukurupuka katika hili halafu wakatuletea katiba mbovu kuliko iliyopo

Wanachotakiwa kufahamu, wananchi wote sio wanachama wa chama chao na wanapigania kitu kinachohusu wananchi wote. Jukumu lao kubwa ilitakiwa iwe kushawishi kwanza hasa hasa kidiplomasia kuliko kushurutisha

Baadhi ya wananchi wanaweza kuwaona CHADEMA kana kwamba wanapigania hiyo katiba zaidi kwa maslahi yao wenyewe kuliko maslahi ya nchi


Screenshot_20210701-174329~2.jpeg
 
Chadema wanataka chao mapema kweupeee kabla Mama hajaanza kuwa mkali. Wajue zile zama za USINIJARIBU zimekwisha na sasa ni zama za USINIZINGUWE. Wakitaka wanachotaka lazima aende kwa upole bila kumzinguwa mtu.
 
Kujenga uchumi bila demokrasia haiwezekani. Alijaribu Nyerere alipokataa Haki za Binadamu tangu mwaka 1961 mpaka mwaka 1984. Alijaribu Magufuli mwaka 2015 mpaka 2020.

Katiba sio ya Chadema wala CCM ni yetu sote yaweza kukusaidia familia yako huko mbeleni.
 
Kujenga uchumi bila demokrasia haiwezekani. Alijaribu Nyerere alipokataa Haki za Binadamu tangu mwaka 1961 mpaka mwaka 1984. Alijaribu Magufuli mwaka 2015 mpaka 2020.

Katiba sio ya Chadema wala CCM ni yetu sote yaweza kukusaidia familia yako huko mbeleni.
Mkuu katiba na familia wapi na wapi- kwanza familia ipi hizi za kishoga wanazotaka CHADEMA
 
Kwa namna Mambo yanavyoenda, viongozi wa CHADEMA wanazidi kukosa njia sahihi za kushughulika na maswala badala yake wanaendelea kuzidisha uanaharakati hata pale harakati zisipohitajika

Kwa watu makini wanafahamu kabisa jambo bora hutokana na fikra tulivu zisizo na purukushani wala marumbano

Kwa mazingira yaliyopo, hoja kuu ya CHADEMA wanataka katiba mpya ili wapate tume huru ya uchaguzi! (Japo yapo mengi lakini hili limeteka mijadala ya viongozi wao)

Sote tunafahamu kuwa katiba ndio msingi wa ujenzi wa Taifa bora! Fundi anapojenga msingi wa nyumba huku anapresha za hapa na pale kutoka kwa Boss wake, familia na njaa tumboni mwake hawezi kujenga msingi uliobora kubeba nyumba imara

CHADEMA wanatakiwa kutumia nafasi hii ya kudai katiba mpya bila vitisho kwa serikali ili waweze kupata faida ya kuwaunganisha wananchi wote bila kujali makundi yao ili wawe kitu kimoja

Mazingira ya Sasa sio yaliyokuwepo miezi kadhaa nyuma. Sasa hivi nchi ina utulivu na watu bado wanampima Rais aliyepo madarakani

Haiwezekani kwa miezi mitatu tu afute yale yooote yaliyoharibiwa na kiongozi aliyekuwepo! Angekuwa amejiuzulu au amepinduliwa hapo labda! Lakini kumbukeni aliyekuwepo amefariki! Anayeingia lazima atajaribu kulinda heshima ya marehemu kwa muda hata Kama alikuwa hakubaliana nae

CHADEMA wasitake kukurupuka katika hili halafu wakatuletea katiba mbovu kuliko iliyopo

Wanachotakiwa kufahamu, wananchi wote sio wanachama wa chama chao na wanapigania kitu kinachohusu wananchi wote. Jukumu lao kubwa ilitakiwa iwe kushawishi kwanza hasa hasa kidiplomasia kuliko kushurutisha

Baadhi ya wananchi wanaweza kuwaona CHADEMA kana kwamba wanapigania hiyo katiba zaidi kwa maslahi yao wenyewe kuliko maslahi ya nchi


View attachment 1836916

imeeleweka
 
Wewe unasemaje. Unahitaji katiba iliyobora ama unataka inayomruhusu kila mtu kufanya atakavyo, na hata akikosea asiulizwe milele?
Umewahi kuwaza kwamba dunia duara na ya kwamba kunasiku utakuwa upande wenye kivuli na kwamba itakuwaje kwako katika majira yale?
 
Wewe unasemaje. Unahitaji katiba iliyobora ama unataka inayomruhusu kila mtu kufanya atakavyo, na hata akikosea asiulizwe milele?
Umewahi kuwaza kwamba dunia duara ?
 
Kujenga uchumi bila demokrasia haiwezekani. Alijaribu Nyerere alipokataa Haki za Binadamu tangu mwaka 1961 mpaka mwaka 1984. Alijaribu Magufuli mwaka 2015 mpaka 2020.

Katiba sio ya Chadema wala CCM ni yetu sote yaweza kukusaidia familia yako huko mbeleni.
Ndiomaana wanatakiwa kwenda na wananchi wote. Hapa mtego ni mmoja tu, wao wanataka kohodhi hili jambo kwa shuruti! Sometimes convincing power ya kidiplomasia ni nzuri zaidi
 
Kujenga uchumi bila demokrasia haiwezekani. Alijaribu Nyerere alipokataa Haki za Binadamu tangu mwaka 1961 mpaka mwaka 1984. Alijaribu Magufuli mwaka 2015 mpaka 2020.

Katiba sio ya Chadema wala CCM ni yetu sote yaweza kukusaidia familia yako huko mbeleni.
Rwanda,Uganda,Ivory coast, Egypt nk kuna demokrasia gani huko? Mbona uchumi unakua vizuri?
 
Tunahitaji watuoneshe kwa mifano kwa kuwa na utaratibu wa kubadili Mwenyekiti wa chana maana tuliye naye sasa ni Mwenyekiti wa kudumu, sasa huyu akiwa Rais atang'atuka kweli?
 
Nilishangaa Mnyika aliposema wananchi wapo tayari kukatwa kodi kwa ajili ya katiba mpya sijui aliongea na wananchi wa wapi.
 
Mungu ibariki Chadema
Yani leo nimechoka Sana Yani Katiba tunayotumia ni sawa na kuchukua Katiba ya chama na chama ungaunganisha, alafu ukaweka mawazo ka kikundi ka watu sita, then unasema hii ndo Katiba ya kuongoza watu mil 60,

Na ccm bado wanaona sawa Yani ,
 
Kujenga uchumi bila demokrasia haiwezekani. Alijaribu Nyerere alipokataa Haki za Binadamu tangu mwaka 1961 mpaka mwaka 1984. Alijaribu Magufuli mwaka 2015 mpaka 2020.

Katiba sio ya Chadema wala CCM ni yetu sote yaweza kukusaidia familia yako huko mbeleni.
Baada ya katiba mpya agenda ya upinzani itakuwa nini? Tunadanganyana sana. Mama ameturuhusu kudemka sasa tunataka kumtia vidole machoni.
Katiba mpya asikimbilie kama ndio muarobani wa kuitibu Tanzania. Tanzania ina shida kubwa sana za kitamaduni na za kimaono, kuliko katiba mpya. Hivi hatuoni shida ya rushwa na wizi wa mali ya umma, na huu ujanja ujanja wa baadhi ya watu wenye dhamana kutumia nafasi na mali za nchi kuanzisha project kwa manufaa yao?
 
Sijui kwanini nikimuona kijana yupo CCM namuona tapeli
Hilo ndo tatizo la ushabiki wa vyama, kila anayekuwa tofauti na mawazo ya chama unachoamini unaamini yuko chama unachopingana nacho. Tunahitaji kubadili mitazamo ya vijana bila hivyo Taifa linapotea
 
Ndiomaana wanatakiwa kwenda na wananchi wote. Hapa mtego ni mmoja tu, wao wanataka kohodhi hili jambo kwa shuruti! Sometimes convincing power ya kidiplomasia ni nzuri zaidi
Kea Nini convincing power haina Nguvu hapa? Ccm wananufaika mmoja kwa moja na hii katiba wakati wasio ccm hawanufaiki. Kwa hiyo ni lazima chadema na raia watumie Nguvu ya ziada Ili kuruhusu hili lifanyike. Yani uende ccm halafu uwaambie tunataka katiba mpya unadhani watakubali?
 
Back
Top Bottom