KARLO MWILAPWA
JF-Expert Member
- Apr 10, 2019
- 2,590
- 4,603
Ni muda muafaka wa kumpongeza Rais Samia kwa kuwahamisha Wamasai na wakazi wengine ndani ya hifadhi ya Ngorongoro kulingana na maamuzi kama hayo yaliyowahi kufanyika Canada na Marekani.
Tarehe 20 ya mwezi wa 7 kila mwaka nchini Canada wanasherehea ' National Park Day" sherehe ambayo Wacanada wanapewa ruhusa ya kutembelea hifadhi za Taifa bure.
Inasemwa kwamba furaha ya uwepo wa siku hii unachagizwa na maamuzi magumu na mazito yaliyochukuliwa miaka ya 1880 na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Taifa hilo la kuwahamisha wazawa na wakazi kwenye hifadhi za Taifa.
Mwaka 1887 hifadhi ya kwanza Canada na ya Tatu duniani inayoitwa "Banff National Park" ilianzishwa Kwa wazawa kuhamishwa tena kwa kutumia nguvu kubwa. Maamuzi hayo leo ndio yamesadia kukuza utalii ndani ya Canada na utalii unachangia pakubwa sana katika Pato la Taifa la pili kwa ukubwa Marekani ya Kaskazini.
Mchakato wa kuwahamisha wazawa kwenye hifadhi haukuishia hapo bali uliendelea kwenye hifadhi nyingine ndani ya Canada na Marekani.
Faida zilizopatikana/zinazopatika a maeneo husika Kwa kuwahamisha wakazi kwenye hifadhi:
Kwanza, kukuza utalii wa ndani na wa nje. Utalii kama chanzo kikubwa Cha mapato na fedha za kigeni kwa mataifa mengi, mataifa mengi yameangalia suala la kukuza utalii Kwa namna hii. Kama ilivyokuwa kwa hifadhi ya 'Banff' nchini Canada na hapa Tanzania utalii Ngorongoro utakua sana.
Pili, kulingana na mtazamo wa wahifadhi, Moja ya njia ya uhifadhi ni kuwatenganisha binadamu na viumbe wengine. Kwenye hifadhi Kuna viumbe vingi ambavyo ni urithi wa dunia, viumbe hivyo kuwa karibu na binadamu ni kuhatarisha uwepo wao. Ndio maana yanafanyika maamuzi ya kuwahamisha.
Hasara za kuwahamisha wazawa kwenye maeneo ya hifadhi:
Kwanza, kupotea kwa utamaduni wa wazawa na asili yao.
Pili, kama itatumika nguvu inawezekana wakapanga kurudi tena baadae Kwa hoja za kurejesha utamaduni na asili yao.
The way forward: Wazawa kama wahifadhi:
Ili kuepukana hasara za hapo juu nchini Canada walifanya makubaliano mbalimbali na wazawa na wazawa wakawa ni wahifadhi namba moja na haya ni baadhi ya makubaliano hayo:
Mwaka 1984 kulifanyika "Inuvialuit Final Agreement" ya kuruhusu wazawa kuwepo hifadhini Kwa kutengenewa eneo dogo ndani ya hifadhi ili waweze kudumisha mila, desturi na tamaduni zao.
Vivyo hivyo mwaka 1993 kulifanyika "Gwaii Haanas Agreement" kati ya Haida Nation na nchi ya Canada juu ya uhifadhi wa maliasili na utamaduni katika " Gwaii National Park Reserve"
Makubaliano kama hayo yanaendelea kwenye nchi nyingine nyingi mpaka Leo katika hoja kwamba WAZAWA NI WAHIFADHI.
The way forward: Hoja ya wazawa ni wahifadhi na suala la Ngorongoro:
Nadhani nasi pia tunaweza kwenda na hoja hiyo ya wazawa ni wahifadhi kwenye suala la Ngorongoro na Wamasai lakini iendane na mazingira ya kwetu.
Pawepo na makubaliano maalumu na wazee wa kabila la kimasai na Serikali, watengewe eneo kidogo ndani ya hifadhi ambalo watakuwa wanaishi humo. Hoja ya msingi ya kutengewa eneo hilo ni kuendeleza na kudumisha utamaduni wao na sio vinginevyo
Hitimisho,
Kama kichwa Cha mada kinavyosema uamuzi wa kuwahamisha Wamasai Ngorongoro ni sahihi na Rais Samia apongezwe Kwa hilo.
Kwa uelewa Zaidi, pitia mada hii website ya straight: Charlotte Dawe: Canadian parks-a dark history and a way forward
Tarehe 20 ya mwezi wa 7 kila mwaka nchini Canada wanasherehea ' National Park Day" sherehe ambayo Wacanada wanapewa ruhusa ya kutembelea hifadhi za Taifa bure.
Inasemwa kwamba furaha ya uwepo wa siku hii unachagizwa na maamuzi magumu na mazito yaliyochukuliwa miaka ya 1880 na aliyekuwa Waziri Mkuu wa Taifa hilo la kuwahamisha wazawa na wakazi kwenye hifadhi za Taifa.
Mwaka 1887 hifadhi ya kwanza Canada na ya Tatu duniani inayoitwa "Banff National Park" ilianzishwa Kwa wazawa kuhamishwa tena kwa kutumia nguvu kubwa. Maamuzi hayo leo ndio yamesadia kukuza utalii ndani ya Canada na utalii unachangia pakubwa sana katika Pato la Taifa la pili kwa ukubwa Marekani ya Kaskazini.
Mchakato wa kuwahamisha wazawa kwenye hifadhi haukuishia hapo bali uliendelea kwenye hifadhi nyingine ndani ya Canada na Marekani.
Faida zilizopatikana/zinazopatika a maeneo husika Kwa kuwahamisha wakazi kwenye hifadhi:
Kwanza, kukuza utalii wa ndani na wa nje. Utalii kama chanzo kikubwa Cha mapato na fedha za kigeni kwa mataifa mengi, mataifa mengi yameangalia suala la kukuza utalii Kwa namna hii. Kama ilivyokuwa kwa hifadhi ya 'Banff' nchini Canada na hapa Tanzania utalii Ngorongoro utakua sana.
Pili, kulingana na mtazamo wa wahifadhi, Moja ya njia ya uhifadhi ni kuwatenganisha binadamu na viumbe wengine. Kwenye hifadhi Kuna viumbe vingi ambavyo ni urithi wa dunia, viumbe hivyo kuwa karibu na binadamu ni kuhatarisha uwepo wao. Ndio maana yanafanyika maamuzi ya kuwahamisha.
Hasara za kuwahamisha wazawa kwenye maeneo ya hifadhi:
Kwanza, kupotea kwa utamaduni wa wazawa na asili yao.
Pili, kama itatumika nguvu inawezekana wakapanga kurudi tena baadae Kwa hoja za kurejesha utamaduni na asili yao.
The way forward: Wazawa kama wahifadhi:
Ili kuepukana hasara za hapo juu nchini Canada walifanya makubaliano mbalimbali na wazawa na wazawa wakawa ni wahifadhi namba moja na haya ni baadhi ya makubaliano hayo:
Mwaka 1984 kulifanyika "Inuvialuit Final Agreement" ya kuruhusu wazawa kuwepo hifadhini Kwa kutengenewa eneo dogo ndani ya hifadhi ili waweze kudumisha mila, desturi na tamaduni zao.
Vivyo hivyo mwaka 1993 kulifanyika "Gwaii Haanas Agreement" kati ya Haida Nation na nchi ya Canada juu ya uhifadhi wa maliasili na utamaduni katika " Gwaii National Park Reserve"
Makubaliano kama hayo yanaendelea kwenye nchi nyingine nyingi mpaka Leo katika hoja kwamba WAZAWA NI WAHIFADHI.
The way forward: Hoja ya wazawa ni wahifadhi na suala la Ngorongoro:
Nadhani nasi pia tunaweza kwenda na hoja hiyo ya wazawa ni wahifadhi kwenye suala la Ngorongoro na Wamasai lakini iendane na mazingira ya kwetu.
Pawepo na makubaliano maalumu na wazee wa kabila la kimasai na Serikali, watengewe eneo kidogo ndani ya hifadhi ambalo watakuwa wanaishi humo. Hoja ya msingi ya kutengewa eneo hilo ni kuendeleza na kudumisha utamaduni wao na sio vinginevyo
Hitimisho,
Kama kichwa Cha mada kinavyosema uamuzi wa kuwahamisha Wamasai Ngorongoro ni sahihi na Rais Samia apongezwe Kwa hilo.
Kwa uelewa Zaidi, pitia mada hii website ya straight: Charlotte Dawe: Canadian parks-a dark history and a way forward