Kufuru katika msiba wa bilionea Sambeke Arusha

Kufuru katika msiba wa bilionea Sambeke Arusha

alaf hii address ya u-bilionea, napata shida sana kuielewa

hata mimi inanisumbua sana, huyo jamaa sijamuona hata kwenye top 10 wa kibongo. AU kumiliki ndege ndiyo ubilionea?Hizi zhule za uandishi wa habari za mwezi mmoja wangezifuta.
 
rubbish. muiteni bilionea huko kwenu. tuwekeeni "net worth" yake hapa tumpime kwa standards zinazotambulika kote duniani. Alikuwa anafanya shughuli gan kwanza??? ametoa ajira ngapi??

Mkuu hilo ni jukumu lako kumpima kwa standard unazozijua wewe mwenyewe.Lakini kwa standard zetu amefuzu kuwa bilionea!
Nyinyi ndiyo mliokuja na tafsiri yenu ya umasikini kwamba mtu yeyote mwenye kipato chini ya U.S Dollar moja ni masikini,wakati huku bongo mtu anaweza kupata mahitaji yake yote ya msingi ilihali hana uwezo wa kuingiza U.S Dollar moja kwa siku!Tokeni na viwango vyenu sisi tunasonga mbele na viwango vyetu!
 
Then na mimi ni bilionea...
Cha ajabu ni nini kama na wewe pia unaassets zenye thamani isiyopungua shilingi bilioni moja za Kitanzania!au mbaka wawe wachache ndiyo utaheshimu ubilionia wa baadhi ya watu?
 
hata mimi inanisumbua sana, huyo jamaa sijamuona hata kwenye top 10 wa kibongo. AU kumiliki ndege ndiyo ubilionea?Hizi zhule za uandishi wa habari za mwezi mmoja wangezifuta.
Teh teh teh!kwani mbaka uwe kwenye kumi bora ndiyo uitwe bilionia?je hicho ndiyo kigezo?
 
tumefikia huku? Mungu aturehemu na huu utamaduni wetu mpya wa kuwananga marehemu woote wa kaskazini! Kufuru ni vinywaji na vyakula kwenye msiba! Yaani hizi chuki sijui zitatufikisha wapi?
mkuu hapa hakuna chuki,nazani hujaielewa vizuri hoja yangu!
 
watanzania lini tutaacha upuuzi wa kujadili upuuzi????
 
Watu wakienda msibani huku hula na kunywa. Watu ni wengi na chakula ni kingi pia. Hiyo kufuru ndio ipi? Huyu mwandishi sijui vipi. Ningemwelew kama angesema serikali yafanya kufuru kupotezea bilion 620 za mkopo..
 
Hahaha. Nyumbani kwenu hamna picha ya Yesu alipowaambia jamaa shusheni nyavu. Wakashusha wakapata mafishi hadi wakapata hasara ya neti kuchanika hahaha. Labda wanatumia hiyo aisee. Wachaga wa siku hizi kama wapare vile.
Hebu tuwekee picha

Ukute walikuwa wanakuwa ugali kwa samaki wa kuchora weeeeengi
 
Tatizo letu no ubwabwa kuwa mwingi kuliko kawaida kutegemeana na perception yako baba. Mi nilienda msiba musoma ule ugali wao niliona kama wamepika mwingi kama kufuru ila wakaula wote wakamaliza.

Marehemu hakuwa masikini. Na marafiki na wachangia msiba sio maskini. Mbona wachaga wa kimara misiba yao wanakunywa biya na huku kwa mtogole tunazima huzuni kwa gongo? Relax baba. Acha wafu wazike wagu wao kwa raha zao
Hata kama tunalima wenyewe,ukiwa mwingi zaidi ya kawaida ni kufuru mkuu!
 
Back
Top Bottom