TUKUTUKU
JF-Expert Member
- Sep 14, 2010
- 11,763
- 4,046
Ni kweli mkuu,lakini lengo la mtoa mada ni kutujuza yaliyojili msibani!Msiba ni msiba tu ndugu yangu. Roho imeshatoka haya mengine ni kujiridhisha.
Ni kweli mkuu,lakini lengo la mtoa mada ni kutujuza yaliyojili msibani!Msiba ni msiba tu ndugu yangu. Roho imeshatoka haya mengine ni kujiridhisha.
Sasa kula na kunywa ndio kufuru? Roho yake iende inapostahili either sawasawa na matendo yake.
Teh teh teh!umenichekesha sana mkuu!Sasa kama hela ipo watu wasile??
Namna ya uandishi huu wa habari inaonesha namna mwandishi wa habari alivyo na fikra za kimaskini.
Mtu kafariki lakini pesa haijafariki...
Ngoja tusikilize majibu ya MziziMkavu kuhusiana na hili!mzizimkavu is losing is cool and direction
labda friimeson wameshamla kichwa na maimani yake meusi
Ni kwa sababu hukumjua au hukuwahi kuishi karibu na mtu huyo ndio maana unapata shaka.
Kwa tuliomjua kwa karibu tunajua jinsi mwanaume yule alivyokuwa na uwezo wa kutisha wa senti, ikiwa ni pamoja na vision za hali ya juu za maendeleo.
Yeye alikuwa akiongelea kuhusu kuanzisha Flying School, kitu ambacho hata serikali haijawahi kuwaza hilo.
Vipi mkuu,ulikuwa na ungomvi na marehemu?Kazi ipo...nyama ya udongo mwacheni aende zake
Huu ni utamaduni wa binadamu!Kweli watu wakishakufa wanageuka watakatifu.
Alikuwa tishio kivipi?kisiasa,kiusalama au kimazingira?Kumbukumbu yangu huyu jamaa alikuwa tishio ila kwa sababu ya U-bilionea basi anaonekana wa maana.Mwenyezi mungu ailaze roho ya mbabe huyo mahali pema peponi.AMEN
Duh!akutukanaye akuchagulii tusi!Mwandishi ameiandika habarihii kama ANAOGA NJE! au ilikuwa na MINOFU lakini Mhariri akaipunguza?
Kwani watu huwa wanaitwa bilionaires kwasababu gani?Kwa nini anaitwa bilionea.
Babu Sambeke ni mmoja wa wafanyabiashara wa kwanza katika kanda ya Kaskazini kumiliki ndege, na hadi anafariki alikuwa akitumia ndege mbili.Jina lake lilianza kuwa maarufu 1985 akionekana kama mtoto wa mjini `mission town na baadaye alijiimarisha kibiashara na kuwa na utajiri mkubwa.Kufuru katika msiba wa bilionea Sambeke Arusha - Kitaifa - mwananchi.co.tz
Kwani watu huwa wanaitwa bilionaires kwasababu gani?
Sasakufuru hapo ni ubwabwa jamani? Waandishi wa habari bwana!