Kuelekea Uchaguzi 2024 na 2025: Umesikia kauli gani kutoka kwa viongozi ukaona zinahatarisha Ustawi wa Demokrasia?

Papaa Mobimba

JF-Expert Member
Jan 27, 2018
754
3,097
Wakati wa chaguzi mbalimbali duniani huwa viongozi na wanasiasa wanatoa kauli mbalimbali katika kunadi sera zao na vyama vyao kwa ujumla. Kauli zinazotolewa huweza kuwa nzuri za kujenga au zikawa kauli za chuki zenye lengo la kugawa na kubagua kundi fulani.

Hayati Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa wagombea wakishindwa kujinadi kwa sera zilizo saaafi ili wakubalike, basi wanaweza kutumia njia mbadala ambazo zinaweza kuwa za chuki na kugawa jamii, hivyo viongozi hao hawapaswi kabisa kuchaguliwa.

Pia, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonia Guterres alitoa hadhari kuwa hotuba za chuki zinapaswa kuchukuliwa kama tunavyochukulia vitendo vyovyote vibaya, kwa kuzilaani, kutoziendeleza, kukabiliana nazo na ukweli na kuchagiza wanaozitekeleza kubadili tabia.

Narudi kwako mdau; je, ni kauli gani zimewahi kutolewa na kiongozi au mgombea wakati wa kipindi cha uchaguzi ukaona zinaathiri mchakato mzima wa Uchaguzi?
 
Kabla, wakati na baada ya uchaguzi mbalimbali duniani huwa viongozi na wanasiasa wanatoa kauli mbalimbali katika kunadi sera zao na vyama vyao kwa ujumla. Kauli zinazotolewa huweza kuwa za nzuri za kujenga au zikawa kauli za chuki zenye lengo la kugawa na kubagua kundi fulani.

Hayati Mwalimu Nyerere aliwahi kusema kuwa wagombea wakishindwa kujinadi kwa sera zilizo saaafi ili wakubalike, basi wanaweza kutumia njia mbadala ambazo zinaweza kuwa za chuki na kugawa jamii, hivyo viongozi hao hawapaswi kabisa kuchaguliwa.

Pia, Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa, Antonia Guterres alitoa hadhari kuwa hotuba za chuki zinapaswa kuchukuliwa kama tunavyochukulia vitendo vyovyote vibaya, kwa kuzilaani, kutoziendeleza, kukabiliana nazo na ukweli na kuchagiza wanaozitekeleza kubadili tabia.

Narudi kwako mdau, JE, NI KAULI GANI ZA CHUKI ZILIWAHI KUTOLEWA NA KIONGOZI au MGOMBEA WAKATI WA UCHAGUZI UKAONA ZINAATHIRI MCHAKATO MZIMA WA UCHAGUZI?
baadhi kauli za mikwara na kubwekabweka za puppet na kigaila 🐒


hakuna Katiba mpya hakuna uchaguzi 🐒

hakuna uchaguzi utakaofanyika bila tume huru ya uchaguzi🐒

piga kura linda kura 🐒

hatutashiriki uchaguzi bila tume huru na katiba mpya 🐒

bila wagombea wetu walioenguliwa kurudishwa kwenye sanduku la kura hakuna uchaguzi 🐒
 
Jokate: Wanawake ifike mwisho kuwapigia kura wanaume

Hayati Magufuli: Mkimchagua mpinzani hatutaleta maendeleo

Hayati Lowassa; Sasa ni zamu ya kuwa na Rais Mlutherani

Katambi; Msimchague mwanamke (Salome Makamba) anaingia siku zake ....

Rais Samia; Hata ukipigia kura kwingine, CCM itaunda Serikali.

Hizi ni baadhi kati ya nyingi sana.
 
Back
Top Bottom