Sokomoko
JF-Expert Member
- Mar 29, 2008
- 1,915
- 130
Binafsi ninamheshimu sana Said Kubenea kwani ni miongoni mwa waandishi wenye misimamo hasa kwa yale wanayoamini kuwa ni kweli, lakini wasiwasi wangu unakuja baada ya kusoma makala zake nyingi nimegundua zinamhusu Lowassa, kitu kilichonifanya nidhani kuwa kuna tatizo kati ya wawili hawa na si ufisadi kama anavyochukulia Kubenea kama mwanvuli.
Maana kila toleo, tena kwenye ''front page'', utakuta mara Lowasa hivi, mara Lowasa vile, ilimradi tu amseme Lowasa.
Sio kama ninamsemea Lowasa, hapana. Ila tu kama kweli Kubenea unania ya dhati ya kupambana na ufisadi, basi sema juu ya ufisadi na sio Lowasa tu kila siku, mbona kuna mafisadi wengi tu nji hii.
Leo ni Jumanne, kesho Mwanahalisi litakuwa mtaani, habari kuhusu Lowassa ninatarajia kuikuta tena kwenye front page.
Hata watu wa haki za bina damu wanasema "hate the the vice and not the person".
Nakushauri bwana Kubenea utafute namna nyingine ya kukemea ufisadi la sivyo watu wataanza kupoteza imani na wewe.
Kuna usemi wa kiswahili "pilipili iliyo shambani inakuwashia nini" Sioni mantiki ya wewe kulete hii topic ilhal unajua kuwa hivi sasa ule mkataba "mbovu" kupita jote wa ujenzi wa jengo la UVCCM ndio unajadiliwa kwenye vikao vya CCM sasa unataka kutuambia Kubenea atakuwa amefanya dhambi kuipa "mshiko" story aliyoibua! Nina wasiwasi kuwa umetumwa! na sipendi kusema unamtetea Lowasa! kwani sio kweli! huyu ndie alpha na R.A ni Omega wa Richmond asiposakamwa Lowasa asakamwe nani? katibu kata anaekula rushwa ya elfu 10? Be analitical plz.
Kubenea ndio alikuwa wa kwanza kuandika kwa kina kuhusu ufisadi wa UVCCM baada ya kuibuliwa na mhe Nape Nnauye kwahiyo anahaki ya kufanyia follow up mpaka atakapo ona mwisho wake! na wengi tunanunua nakala kujua inaendeleaje? si alitishia kushitaki?? nadhani hiyo ndio solution na sio kukutuma uje na mada inayochefua angalia wengine humu kwenye forum wana mimba changa usije kuwatapisha. "Kubena he is hunting what he can kill he cant hunt what he cant kill" unataka aandike ufisadi wa mtu asie kuwa na ushahidi nae? ili iweje? elewa yeye ni mwandishi na anawakilisha chombo cha habari na anapaswa kuandoka habari zenye ukweli na zilizofanyiwa uchunguzi wa kina na sio fununu na majungu ya vijiweni maana mengi yanasemwa kwenye vijiwe vyetu vya kahawa lakini havina uthibitisho. Waacheni waandishi wa play they are part jamani msiwasakame! na mkumbuke kumtetea fisadi ni ufisadi pia.