Kubenea, njoo uone barabara zako za Sinza

Kubenea, njoo uone barabara zako za Sinza

Habari wakuu.

Mimi ni mkazi wa Sinza. Nipo kimasomo.

Kwakweli barabara za hapa Sinza zinatia kinyaa. Barabara ni mbovu mno. Si kwa watembea Kwa miguu wala wenye vyombo vya Usafiri.

Mbunge wa Ubungo mhe. kubenea embu kuja huku ujionee raia wanavyopata shida. Kata kama haina serikali bhana.

Taarifa uzipate.

Nawasilisha
Kubenea kama ni maendeleo binafsi afanye sasa asiwekeze kwenye kutafuta ubunge tena. Fungu lake la kiinua mgongo aongezee mtaji ajichanganye kivingine hana tena miaka mingine mitano.
 
Hili halitaki tochi,serikali hii inapiga vita upinzani,hata ukichaguliwa na wananchi,inaizinisha peas Kwa sehemu za CCM tu,Sasa ikiwa mkoa wa Dar upo chini ya upinzani,halafu waongozaji wakuu akina bashite wewe unategemea nini,Kubenea anataka kufanya mengi lakini,majambazi ya chama tawala yanatawala Kila kitu,Hawaii Jamaa wanatawala kila kitu,lakini haya yana mwisho,ikiwa wananchi watamua,utawala huu unabagua wananchi sababu ya kutoungwa mkono.mimi natabiri 2020 CCM itakwenda tu
Ingefaa hata angelizungumza bungeni ili tufahamu serikali kwa makusudi kabisa imegoma kukarabati za Sinza....
 
Hujui usemalo. Tangu lini wabunge wakajenga Barabara?
Serikali kuu na mamlaka za serikali za mitaa ndio wenye majukumu hayo. Au unaogopa kuilaumu serikali yako. Usipojenga hoja zenye mashiko, usitarajie mabadiliko.
You are milking a bull.
Siamini kama hili jibu limetoka kwenye mkono wako....

Kwa hiyo unataka kuniambia kuwa mbunge hawajibiki kabisa na kero za wananchi ikiwemo na hiyo bara bara....!!??

Hebu jivue kwanza mahaba alafu ujibu kwa ufasaha..ndugu...
 
Msomi hata hujui mwenye majukumu ya kutengeneza barabara?
Zipo barabara za Tanroads na Zipo barabara za Manispaa.
Ni wapi ulisoma au kusikia ujenzi wa barabara ni jukumu la Mbunge?
Miongoni mwa kazi za mbunge ni kuwakilisha kero za wananchi kwa serikali ili zitafutiwe ufumbuzi...na ubovu wa bara bara ni miongoni mwa kero za wanachi wa eneo hilo....kwa hawana haki ya kumuuliza mbunge wao ambaye ni muwakilishi wao....!!??
 
Binafsi, nimesiyisha kwenda sinza kwakweli.

Especially ile njia ya uzuri. Ni mbovu mno
Mashimo yaliyoko kule ni kama watu walichimba misingi ya nyumba barabarani.
 
Kwa hiyo serikali inawaziba hata midomo huko bungeni wasiongelee hata kuongelea kero za wawakilishi wao.....

Hili la ubovu wa bara bara ya Sinza ulishawahi kusikia Kubenea kalilalamikia....!!??au hii nayo sio kero....!!??
kwa vile ni upinzani hata akiongea kaka, watampuuza tu, na hakuna lolote litafanywa
 
Kabla ya Kubenea alikuwepo Mnyika. Hakuna cha maana alichofanya na watu walilalamika sana humu na kuapa kutomchagua tena. Alichofanya alienda gombea jimbo jingine na kumwachia Kubenea, naye hakuna la maana linaloendelea. Hilo jimbo bila CCM hakuna atakayelirekebisha; kubali au kataa.

Sitaki mapovu mie sio ccm ila najua chadema wamebanwa hapo hawawezi furukuta.
Wewe ni wa hovyo kabisa,mbona mashimo yapo uhuru road,kawawa roa,posta mya huku na sehemu nyingi tu hapa dsm?,kama mkulu amezishikilia rupia aende akamnyang'anye?,kwani jukumu la kuzitengeneza hizo barabara ni kubenea au ni serekali kupitia kodi zetu?.Jitafakari na tumia akili na sio makalio.
 
Kabla ya Kubenea alikuwepo Mnyika. Hakuna cha maana alichofanya na watu walilalamika sana humu na kuapa kutomchagua tena. Alichofanya alienda gombea jimbo jingine na kumwachia Kubenea, naye hakuna la maana linaloendelea. Hilo jimbo bila CCM hakuna atakayelirekebisha; kubali au kataa.

Sitaki mapovu mie sio ccm ila najua chadema wamebanwa hapo hawawezi furukuta.
Mbona husemi kabla ya Mnyika alikuwepo nani? Hivi mnafikiri changamoto za jimbo la Ubungo ni barabara za Sinza peke yake? Btw, kwanini mnang'ang'ana na mbunge badala ya kushirikiana na mbunge kuibana serikali, na mnadai nyie ni wasomi! Hovyoo....
 
Nyie watu, huu ujinga utaisha lini jamani? kwa nini uiangalie barabara mbovu kisha uanze kumlilia Mbunge????? Bajeti ya ujenzi wa barabara siku hizi imehamishiwa kwa wabunge?????
Kwa Kubenea sio sawa kwa sababu ni Chadema ila kwa Mwamoto wa CCM ni sawa.
 
Kabla ya hao walikuwepo viongozi wa ccm lkn hawakufanya kitu chochote hebu tuache unafiki serikali haitengi bajeti ulitaka atoe pesa mfukoni
 
Mbona husemi kabla ya Mnyika alikuwepo nani? Hivi mnafikiri changamoto za jimbo la Ubungo ni barabara za Sinza peke yake? Btw, kwanini mnang'ang'ana na mbunge badala ya kushirikiana na mbunge kuibana serikali, na mnadai nyie ni wasomi! Hovyoo....
Hizo barabara zipo chini ya halmashauri, halmashauri ya Ubungo ipo chini ya UKAWA, meya Boniface Jacob amevimba mashavu tu anahangaika na Makonda anaacha majukumu yake ya muhimu.
 
Kabla ya Kubenea alikuwepo Mnyika. Hakuna cha maana alichofanya na watu walilalamika sana humu na kuapa kutomchagua tena. Alichofanya alienda gombea jimbo jingine na kumwachia Kubenea, naye hakuna la maana linaloendelea. Hilo jimbo bila CCM hakuna atakayelirekebisha; kubali au kataa.

Sitaki mapovu mie sio ccm ila najua chadema wamebanwa hapo hawawezi furukuta.
Mbunge anatengeneza kwa hela yake au?
 
Habari wakuu.

Mimi ni mkazi wa Sinza. Nipo kimasomo.

Kwakweli barabara za hapa Sinza zinatia kinyaa. Barabara ni mbovu mno. Si kwa watembea Kwa miguu wala wenye vyombo vya Usafiri.

Mbunge wa Ubungo mhe. kubenea embu kuja huku ujionee raia wanavyopata shida. Kata kama haina serikali bhana.

Taarifa uzipate.

Nawasilisha
Hadi sasa hujaweka picha mkuu, mantiki ya thread iko wapi sasa
 
Siamini kama hili jibu limetoka kwenye mkono wako....

Kwa hiyo unataka kuniambia kuwa mbunge hawajibiki kabisa na kero za wananchi ikiwemo na hiyo bara bara....!!??

Hebu jivue kwanza mahaba alafu ujibu kwa ufasaha..ndugu...
Huelewi usemacho. Soma post yangu ukiwa na akili tulivu, utanielewa.
 
Huelewi usemacho. Soma post yangu ukiwa na akili tulivu, utanielewa.
Kwa hiyo unataka kuniambia kuwa mbunge hawajibiki na hilo......!!??

John Mnyika alivyosimamia uchongaji wa bara bara huko kibamba maana yake ameingilia mambo yasiyo muhusu.....!!??

Kwa hiyo mbunge amechaguliwa na wananchi kwa ajili ya kutunga sheria tu.....!!?

Nitajie ninani ambaye ni muwakilishi wa kero za wananchi huko bungeni...!!??

Au kwako ubovu wa bara bara sio miongoni mwa kero za wananchi...!!!??
 
Mimi sioni kama wabunge wanatujali wananchi, sehemu nyingi tuu miundombinu imeharibika lkn hata mbunge kuja kuwafariji tuu raia inakuwa shida? Wananchi tuwe makini sana na wabunge wetu 2020 tusifanye makosa.
Pale itakapofika siku watanzania tukatambua huduma za jamii si mtaji wa wanasiasa kuombea kura ila ni jukumu la serikali kutekeleza majukumu yake kwa sababu ndio inayokusanya kodi... ndipo hapo taifa litapiga hatua na hizi kelele zitaisha.
 
Mbona husemi kabla ya Mnyika alikuwepo nani? Hivi mnafikiri changamoto za jimbo la Ubungo ni barabara za Sinza peke yake? Btw, kwanini mnang'ang'ana na mbunge badala ya kushirikiana na mbunge kuibana serikali, na mnadai nyie ni wasomi! Hovyoo....

Kabla ya Mnyika barabara zilikuwa angalau zinapitishwa greda mara chache. Baadhi ya sehemu kulianza hata kuwekwa vibarabara vya lami. Barabara ya Legho to darajani ilikuwa inapigwa greda na ilianza kutengenezwa na sehemu nyinginge jimboni zilikuwa zina afadhali. Baada ya kuchagua upinzani mambo yote yamekwama. Hili jambo wewe hulijui na malumbano haya yalikuwepo na Mnyika alishindwa kufurukuta na kuamua kukimbia jimbo. Usiropoke kama kitu hukijui, issue ya usomi imetoka wapi hapo. Piga kimywa huna ujualo.
 
Back
Top Bottom