Kuazima gari ni ustaarabu?

Kuazima gari ni ustaarabu?

jigili

JF-Expert Member
Joined
Sep 9, 2011
Posts
351
Reaction score
347
Kuna jirani yangu amekuja leo kwangu anaazima gari awapeleke jamaa zake kutoka sehemu moja kwenda nyingine.Jirani mwenyewe japo namfahamu kwa sura lakini hata jina lake silifahamu kwa sababu si miongoni mwa majirani ambao tuna ukaribu sana.Swali likanijia huyu bwana anafunga safari kuja kuazima gari kama fyekeo hivi akipata nalo ajali atakuja na maelezo gani?
Lazima tujifunze kuishi kwa kile mwenyezi Mungu alichotukadiria
 
Kuna jirani yangu amekuja leo kwangu anaazima gari awapeleke jamaa zake kutoka sehemu moja kwenda nyingine.Jirani mwenyewe japo namfahamu kwa sura lakini hata jina lake silifahamu kwa sababu si miongoni mwa majirani ambao tuna ukaribu sana.Swali likanijia huyu bwana anafunga safari kuja kuazima gari kama fyekeo hivi akipata nalo ajali atakuja na maelezo gani?
Lazima tujifunze kuishi kwa kile mwenyezi Mungu alichotukadiria

Ndugu yangu pole hicho ni kitu cha kawaida sana kumuazima rafiki yako wa karibu acha kuzunguka tu unaweza kumpatia akasfir nalo mfano mza - dar inategemea mmeshibana vp suala la ajali hata mwenye nalo unaweza pata!
 
Wa karibu haina shida lakini huyu ni jirani tu unakutana nae mtaani na kusalimiana! jina humfahamu japo unajua nyumba aliyopanga lakini ukiambiwa kaonyeshe chumba chake hujawahi hata kanyaga?
 
Kuna majirani au marafiki ambao kweli mnakuwa mmeshibana hata akiazima hupati shida kumpa lakini mtu ambaye hata nikikuuliza jina langu kamili hunifahamu kisa umeniona mshikaji wa kitaaa.
 
Uchumi wako ni wa kiwango fulani, ndiyo maana huoni tabu kumwazima fyekeo. Uchumi wako ungekuwa wa kiwango fulani kingine usingeona tabu kumwazima gari. Nakublina nawe kwamba jamaa anakosea kujaribu kwenda kinyume na hali zenu za uchumi.
 
Inategemea ni kiasi gani mmeshibana na huyo muazimaji na ustaarabu wake. Mwingine anaweza kuwa hajali kabisa kwenye mahandaki ya Dar analipigiza mtindo mmoja lakini lingekuwa la kwake asingefanya hivyo.
 
Gari sio kitu chakuazima bana bora nikupe nauli ya tax

Kwani gari ina nini usiazime mwenzio? Kama kitu cha maana sana mbona ukifa huzikwi nayo?
Cha msingi
1.mufahamiane,
2.Ajue kuendesha,
3.ujue shughuli anayoenda kufanyia.
Tuache ulimbukeni ukiwa na gari ndo kujiona umemaliza.
 
Wa karibu haina shida lakini huyu ni jirani tu unakutana nae mtaani na kusalimiana! jina humfahamu japo unajua nyumba aliyopanga lakini ukiambiwa kaonyeshe chumba chake hujawahi hata kanyaga?

Hiyo nayo kali!
Ukitapeliwa utasema nini?
Ebu pima anaondoka nalo moja kwa mmoja utafanya nini,baada ya mwezi anarudi ukiuliza Gari anakuambia umechanganyikiwa lini umenipa gari lako na kivipi unipe gari lako!
Haya banah!
 
Namuazimisha mtu wa karibu, sio vinginevyo
 
Kuna jirani yangu amekuja leo kwangu anaazima gari awapeleke jamaa zake kutoka sehemu moja kwenda nyingine.Jirani mwenyewe japo namfahamu kwa sura lakini hata jina lake silifahamu kwa sababu si miongoni mwa majirani ambao tuna ukaribu sana.Swali likanijia huyu bwana anafunga safari kuja kuazima gari kama fyekeo hivi akipata nalo ajali atakuja na maelezo gani?
Lazima tujifunze kuishi kwa kile mwenyezi Mungu alichotukadiria

Mkuu gari sio ------,sio kila mtu anagari,gari huazimwa kwa mweye gari,yaan unakuta jamaa yako ana gari sema imesumbua labda ghafla akakuomba yako labda awahi mahali then unaweza kumpa!not otherway around mkuu.
 
Kuna jirani yangu amekuja leo kwangu anaazima gari awapeleke jamaa zake kutoka sehemu moja kwenda nyingine.Jirani mwenyewe japo namfahamu kwa sura lakini hata jina lake silifahamu kwa sababu si miongoni mwa majirani ambao tuna ukaribu sana.Swali likanijia huyu bwana anafunga safari kuja kuazima gari kama fyekeo hivi akipata nalo ajali atakuja na maelezo gani?
Lazima tujifunze kuishi kwa kile mwenyezi Mungu alichotukadiria

Heshimu gari baba .gari siyo kiungo mtu anazaliwa nacho.
 
Back
Top Bottom