Kuanguka kwa CCM - Unabii Utatimia!

Kuanguka kwa CCM - Unabii Utatimia!

Tuombe uhai. Natamani sana kuona CCM ikimeguka. Nadhani hili halitakuwa jambo baya kwa nchi bay ni kuacha CCM ikaendelea katika hali hii.
 
chama kimejigawa kwa maana ya kuwa na makundi amabyo hayataweza kuwa pamoja tena, kilichobakia ni lini hilo kundi lisilo na uwezo litajitoa rasmi?
 
Hizi habari za kuanguka kwa CCM zinakuwa kama muziki kwenye ndoto maridhawa wakati wa usingizi mwororo wa mchana.

Unapoamaka na kujikungu'ta unakuta CCM iliyo imara zaidi na ndoto zimekwisha.Tunapenda kuona CCM imekwisha lakini ndoto bado kabisa....labda 2050.
 
MAFISADI NA UFISADI unaofanywa na baadhi ya wajumbe au wanachama wa CCM ipo siku utaanguka na wataanguka ,ni kweli ufisadi upo popote paleduniani lakini UFISADI unaodidimiza maendeleo ya nchi ni ufisadi unaofaa kupingwa na kila binaadamu kwa jinsi anavyoweza,naujadili ufisadi wa nchi masikini kama Tanzania.
CCM LEO haiwezi kuwaambia wananchi iko sawa wakati ndani yake kuna ufisadi wa kutisha mpaka unaweza mtu ukaamini nchi ya Tanzania ni kwa ajili ya watu wachache na si nchi ya waTanzania wote,NDANI YA CCM LEO HII KUNA MAFISADI WA AINA TATU
AINA YA KWANZA NI MAFISADI WANAOPINGA KUITWA MAFISADI: hawa ni wale mafisadi ambao wao wanaona kama wanaonewa lakini ukweli ni kwamba ni kweli ni mafisadi wa kutisha na ndio wanaokisumbua na kukitingisha chama chao cha CCM,hawa ni kama wakina EDWARD LOWASA,CHENGE,ROSTAM AZIZ,SUBASH JITU PATEL, TAMIL SOMAIYA,YUSUPHU MANJI,hawa ndio mafisadi wanaona wanaonewa na kundi la linalowapinga wao wakidhani linaongozwa na SAMWELI SITA,wamekosea sana kudhani hivyo,kweli akili ni nyweli kila mtu ana zake..... hawa mafisadi nitawachambua mmoja baada ya mwingine kwani nimewafuatilia kwa muda mrefu nami si mtu wa kukurupuka hata kidogo.... hata kidogo.......
AINA YA PILI NI MAFISADI WANAOWATETEA MAFISADI KWA NJIA YEYOTE ILE: sina sahaka kabisa hawa wako wengi ndani ya chama,serikalini na hata mitaani,japo mimi hao wa mitaani hawanisumbui sana ndani ya CCM wako kama kina KINGUNGE NGOMBALE MWILU,SOPHIA SIMBA,MAKONGORO MAHANGA,LAURENCE MASHA,ndani ya serikali yuko mmoja ndio kama nguvu yao wanayoiamini EDWARD HOSEA(bw takukuru)
AINA YA TATU YA MAFISADI NI WA MITAANI hawa wanaweza kuwa walishastaafu siku nyingi lakini kwa kuwa wanauswahiba na mafisadi ndio wanaotembeza habari mbali mbali huko mitaani kwamba LOWASA NA WENZIE SI MAFISADI bali wameonewa hakuna haja ya kujua sana sana hawa
MAFISADI ni kweli kama wanavyozungumzwa na vyombo vingi vya habari wananguvu ya kutisha ndani ya serikali,na sasa wanajitahidi nguvu hiyo iwepo katika chama na niwasifu kwa hilo maana wameweza kumtingisha SPEAKER WA BUNGE LA NCHI YA TANZANIA SAMWELI SITA katika mkutano mkuu wa NEC YA CCM ,kama si mtazamo wa mwenyekiti wa CCM yao,muda huu tungekuwa tunazungumza mengine ndani ya nchi ya Tanzania
kwa waTanzania wengi musiojua UFISADI wao unakadiriwa kuwa ni TRILLIONI 22 ZA KITANZANIA,SISEMI KUWA NA PESA NYINGI NI UFISADI BALI WALIVYOZIPATA NDIO KUNAPELEKEA NIWAITE MAFIDASI,kila mmoja amezipata kinyume na katiba na sheria na nchi ya Tanzania.
wadau musishangae mkisikia mkisikia wanachanga bilioni nne kwa ajili ya kutaka kummaliza mbunge fulani asichaguliwe mwakani ,kwao ni kitu kidogo sana,kwani wanajua zitarudi tu,KAMA ROSTAM KAWEZA KUMPA SOPHIA SIMBA MILLIONI 400/- kuhakikisha anashinda uchaguzi wa UWT,na ameshinda sintoshanga anapopeleka BAISIKELI 200 KYELA KWA MWAKYEMBE,500 URAMBO KWA SITA,huyu waTanzania tuliharibu wenyewe pale tulipokubali awe katika BOARD MEMBER YA FDI(forign direct investiment ya dunia) akiiwakilisha Tanzania..........sijui viongozi wa wakati huo walikuwa wanalala usingizi wa namna gani sijui...huyu UMAFYA WAKE UKO KILA MAHALI mfano ni RAIA WA NCHI KAMA VENEZUELA,UEA,CANADA,OMAN,IRAN, huko kote ana ASSET ZISIZO KUWA NA KIKOMO,leo mwakiyembe anaposema atapambana naye mpaka kufa mimi naseme namtakia kila la kheri na waTanzania tumuombe kwa MWENYEZIMUNGU AWEZE KUFANIKISHA HILO....KILA LA KHERI DAKTARI MWAKYEMBE......... mtu ambaye anaweza kupokelewa kama Rais wa nchi anapotua Dubai International airport,nafikia kusema zaidi ya rais ni jeshi la UAE linampokea namna hiyo kila anapokwenda huko,Je leo kwanini asipange mambo ndani ya nchi masikini kama TANZANIA awezavyo? huyu anaweza kumuita waziri yeyote saa yeyote atakayo kama anaita mfanya kazi wake wa ndani .....LAWRENCE MASHA HAWEZI KUBISHA katika hili, huo ni mfano mmoja tu akibisha nitaijulisha dunia ni lini wapi,saa ngapi,mwaka gani,siku,tarehe ilifanyika hilo
nataka niseme hivi LOWASA ndio mtu wa kwanza kujuana na ROSTAM NA si JAKAYA kama wengi wanavyofikiri,ndio baada ya hapo wakajenga kitu tunaita PEMBE TATU,na mahusiano ya LOWASA NA ROSTAM NI KIBIASHARA ZAIDI KULIKO SIASA,isipokuwa wanapokutana wote watatu ndio wanajenga mahusiano ya KISIASA.

WIKI IJAYO nitaeleza walijipanga vipi kuhakikisha wanaingiza nguvu zao ndani ya chama nikianzia na UCHAGUZI WA NEC YA CCM YAO YA SASA ilivyo kuwa hapo ndio waTanzania mutajua HATMA YA CCM IKO WAPI KATIK SIKU ZA BAADAE?

KAMATI YA MZEE MWINYI inaendelea na kazi tusubiri ,nitachambua humu mjengoni wanaopinga UFISADI wamejipanga namna gani kuhakikisha wanakabiliana nao kila kukicha,tuishie hapo

ALUTA CONTINOUR

MTAFITI
mtafiti@yahoo.com
 
Amina, na ije siku hiyo, Mungu ni mwema, kilio cha watz kimesikiwa masikioni mwa Mungu wetu, na Mungu anaenda kujibu maombi yetu. tumeonewa vya kutosha, tumepumbazwa vya kutosha, tumefumbwa mdomo vya kutosha, tumeibiwa vya kutosha, sasa umebakia muda wa Mungu kuinuka ili maadui wetu watawanyike. siku hiyo naikumbuka, kwasababu ccm itakunjwa kama karatasi. just as the world utakavyokunjwa kama karatasi siku ya mwisho, so comes for ccm soon. wale walioishi kwa kutegemea dili za viongozi wa ccm kujenga viwanda na kuiba mabilioni, wataaibika na kila mtu ataona uchi wao. hakika itakuwa wakati wa aibu kubwa kwa waonezi wa tz. Mungu ibariki Tanzania, Mungu tukomboe na mashati haya ya kijani.
 
Mnazungumzia chama kumeguka au baadhi ya wanachama kutoka? Maana ya kumeguka ni pale baadhi ya viongozi wakitoka wanafuatwa na kundi kubwa la wanachama na hivyo kufanya chama husika kupunguza kwa kiasi kikubwa wanachama wake. Lakini kwa CCM hao wabunge 11 wapiganaji wakitoka leo, hawatakuwa na impact yeyote ya kuita kumeguka kwa chama kwani hawana wafuasi wakutosha ambao watatoka nao.
 
Hawana wafuasi? Unadanganyika,kupinga ufisadi ni mass issue,like mass movement. Mawaziri walipojaribu kupita mikoani wakihubiri usafi wa serikali je,hukusikia walivyokuwa wakizomewa na wananchi wa kawaida sana na sio wasomi. Take care,unaishi nje au Tanzania?
There is mass support for the ant-corruption crusaders.labda wewe huwasaport.
 
CCM kama taasisi, sioni ikianguka siku za karibuni. Naitazama CCM kama chupa lililobeba kimiminika fulani. Mabadliko ninayobashiri ni kwa kimiminika hicho kumwagika au kumwagwa, na kingine kuingia ndani kuziba ombwe (vacuum) hilo. Wataondoka watu ndani ya CCM (labda hao mafisadi na wengine wenye hatari ya kukikwamisha), na wataingia wengine na sera mbadala, na chama kitaendelea kuwepo.

Kinachonipa imani kuwa CCM haianguki ni kwanza kukosekana kwa chama mbadala hadi sasa, chenye coverage kubwa kama CCM. Pili, CCM inaonekana hadi sasa kama ndio 'power house', watu wanaosaka madaraka wanaamini ni rahisi kuyapata kupitia CCM kuliko chama kingine,na pia wananchi kuamini hadi sasa kuwa viongozi wa CCM ndio viongozi wa nchi, ndio maana hata sasa huu mgogoro ulioko ndani ya CCM unawatisha wengi, badala ya kuwafurahisha kuwa sasa CCM inaanguka! Wananchi wengi hawafurahii kuanguka kwa CCM, badala yake wanahofia hali hiyo, kwani inaelekea kulipeleka pabaya taifa, kutuelekeza kwenye hatari ya kukosa uongozi unaoaminika mbele ya wananchi.
 
Bila ya kuwa na chama mbadala, tunaweza kukiangusha CCM na kuleta a Chiluba like replacement.In essence kuruka majivu na kukanyaga moto.

Hii ndiyo sababu kubwa Wananchi wa Tanzania wanapiga kura kwa principle ya "Zimwi likujualo halikuli likakwisha". I am very sorry to point this out, lakini hatujapata upinzani uliojionyesha kuwa na a nationwide following na ku demonstrate kwamba uko ready for the prime time.

Swala sasa hivi si kuishinda CCM, CCM are basically shooting themselves in the foot.Swala ni kwamba akitolewa CCM aje nani?


Hizi hadithi za 'ikitolewa CCM aje nani' ndizo zinazotukwamisha. Wananchi wengi sasa hawakitaki hiki chama cha majambazi kwa sababu hakiwasaidii katika kuleta maendeleo na badala yake kinawanyonya na kuwakandamiza. Tunahitaji kujipanga na kuwa na chama kikubwa kitakachotokana na wananchi wenyewe (mass party). Hatuzungumzii vyama bureaucratic kama NCCR Mageuzi. Viongozi wa chama hiki watakuwa viongozi waadilifu ambao sisi wananchi tutawa-endorse. Baada ya hapo twende kwenye general elections. Hapo ndipo utakapoona nguvu ya umma. Tukifanya maamuzi na kuhamasisha wananchi kote mijini na vijijini tutafanikiwa tu.
 
Wengi mmekosea mnatafuta ambako siko. Cha msingi ni kama wananchi wameelewa, hadi wanadanganyika watakapoelewa ni karne. Siku zote wanasema "risk takers" katika "marketing" iwe ya bidhaa, wazo, mfumo wowote, asilimia 5% tu ndio huwa wapo tayari kujaribu kitu kipya.

Wabunge 11 wapiganaji wakitoka, bila nguvu ya umma nyuma ni kazi bure. Hata hao wabunge wapiganaji hawajajiandaa na malengo wanayotaka yatokee. Kikubwa zaidi ni kuwaangusha mafisadi wachache, lakini mfumo mzima unabaki. Je wapo tayari kupoteza kila kitu kwa sasa ? Waende wakawaelimishe wananchi na wapate nguvu ya umma?

Ukitaka kujifunza nguvu ya umma, yaangalie maisha ya Mahatma Gandhi, aliishi kijijini kwa miaka kadhaa, akishirikiana na umma wa watu wa vijijini na alipokuwa amekusanya nguvu ya kutosha, aliung'oa utawala wa kiingereza.

Tatizo la wanasiasa wetu wanataka kuanzia na watu wa mijini, na kuwaacha watu wa vijijini, ambao ndio wengi na ambao wanaweza kukipa chama chochote nguvu ya kisiasa.

Angalia mkakati wa marehemu Sam Walton, mmiliki wa WALMART. Alijua kwa kipindi chake asingeweza kushindana na Kmart, JC Penney na maduka mengine makubwa.

Alianzia kijijini, mji mdogo Marekani usio na watu zaidi ya 3,000 , akijiimarisha kwenye maeneo ambayo maduka makubwa hayakufikiria kwenda kufanya biashara. Alipokusanya nguvu kiasi, akasogea miji midogo na hatimaye akaingia miji mikubwa, kabla makampuni makubwa hayajatahamaki, akawa ameshaingia majiji makubwa na hawakuweza kuidhibiti WALMART.

Wanasiasa na wengine wote, tunajifunza nini katika mfano huu, nguvu ya kuitikisa CCM haimo ndani ya kikundi cha wabunge au viongozi , bali katika kuuamsha umma wa watanzania na ambao kwa kiasi kikubwa wako vijijini. Naomba kutoa hoja.
 
Swala si kuanguaka kwa CCM pekee,ila je ikianguka CCM kweli tunaye mtu wakuja kushika hatamu ambayo CCM wataiacha?kwani kwa kweli wapinzani mara nyingi wana wanatuangusha tu.si kwamba natetea CCM au napenda waendelee,ila yasije tukuta yale ya kenya ambako wapinzani waliingia lakini wameleta uozo ule ule wa KANU.....
 
Swala si kuanguaka kwa CCM pekee,ila je ikianguka CCM kweli tunaye mtu wakuja kushika hatamu ambayo CCM wataiacha?kwani kwa kweli wapinzani mara nyingi wana wanatuangusha tu.si kwamba natetea CCM au napenda waendelee,ila yasije tukuta yale ya kenya ambako wapinzani waliingia lakini wameleta uozo ule ule wa KANU.....

Ukisikia mawazo finyu ndiyo haya hapo juu. Kuanguka kwa CCM maana yake ni kuwa tutaanza kujenga utamaduni wa kuwang'oa madarakani wote wale wanaopewa ridhaa ya kuongoza lakini wakaboronga. Mawazo ya eti heri zimwi likujualo ni mawazo mgando na ndiyo yameiwezesha CCM kukaa madarakani miaka nenda rudi huku taifa likiendelea kudidimia katika dimbwi la uchafu na umasikini.

Hivyo CCM imejijengea kiburi hadi kutamba kuwa hata wakilikoroga namna gani, sisi wananchi ndio inabidi tulinywe. Ni matusi makubwa kwa mtu yeyote kufikiria kuwa ndani ya Jamhuri ya Tanzania, hakuna wengine nje ya CCM wanaoweza kuliongoza taifa. Imefikia hatua kwamba CCM hata ikimsimamisha chizi wa kutupwa bado yaweza kuibuka na ushindi kama tunavyoshuhudia hivi leo.

Kudai kuwa hakuna chama mbadala ni dalili ya utapiamlo wa akili na CCM ingependa kulikuza wazo hili kama mtaji wa kubaki madarakani. Kama ninavyosema siku zote, yahitaji uwe jasiri wa ajabu kujiita mwana CCM katika Tanzania ya leo - ni ujasiri unaoongozwa na ujinga, uroho na ulafi wa madaraka, period. Kama Tanzania ilivyowezekana bila Nyerere, itawezekana bila CCM.
 
Swala si kuanguaka kwa CCM pekee,ila je ikianguka CCM kweli tunaye mtu wakuja kushika hatamu ambayo CCM wataiacha?kwani kwa kweli wapinzani mara nyingi wana wanatuangusha tu.si kwamba natetea CCM au napenda waendelee,ila yasije tukuta yale ya kenya ambako wapinzani waliingia lakini wameleta uozo ule ule wa KANU.....

hata wakija wapinzani wenye uozo huu huu ni afadhali kuliko hali ilivyo hivi sasa kwa sababu angalau hao CCM na wapinzani watakao twaa nchi wata tambua kwamba wananchi nao wana nguvu ya kubadilisha chama na sio kuburuzwa buruzwa tuu,

CCM ikianguka itabidi wajipange kwa adabu zaidi kuweza kurudi madarakani sio kama wanavyo fanya sasa hivi ulafi wa kuiba kukomba chakula cha wanetu hadharani tena bila hata kunawa mikono

mimi naomba CCM ishindwe haraka sana ili wajue kuheshimu waliowapa dhamana ya vyeo walivyonavyo
 
100%; nakukubali yaani wewe ndiye Mtanzania halisi unayethamini Watanzania kuliko watanzania wenyewe wanavyojithamini; very well said kwa mzalendo halisi
 
Bw. Mkumbo,

Nakuheshimu sana kwa mchango wako mzuri na maoni yako ambayo umekuwa ukiyatoa mara kwa mara. Isitoshe umewahi kuwa mwalimu wangu pale UDSM na kiongozi wangu ukiwa katika Serikali ya DARUSO. Aidha, natambua vyema kuwa wewe ni Mwanasaikolojia na Mwanafalsafa anayechipukia nchini. Katika kukutambua hivyo, nalazimika kutafuta kupata maoni yako hususan kwenye hili la 'umoja wa wapinzani' kwa kuwa linanitatiza na nimeshindwa kupata majibu.

Suala la Umoja wa Wapinzani naliona kama jambo linalovutia kinadharia hasa likishahabishwa na ile methali yetu ya 'Umoja ni nguvu..utengano ni udhaifu' ingawa tafsiri yake si ya moja kwa moja kiasi hicho. Katika hili nina swali moja tu la msingi nalo ni: "Je, kinachowaunganisha wapinzani wa Tanzania ni nini hasa?"

Kwa uelewa wangu mdogo sioni haswa kinachohitaji wao kuungana. Kwanza si wamoja (homogeneous) kiitikadi, ki agenda,kimalengo na kifalsafa. Ni kikundi cha vyama vya siasa vilivyo nje ya madaraka. Na kama kuungana kwao ni dhidi ya CCM basi ni aheri wasiwepo kabisa tuwe na chama kimoja tu. Historia na uzoefu wa Kenya kwa mfano umetufundisha vizuri tu juu ya muuungano wa wapinzani dhidi ya chama tawala ambao mwisho wake unaishia kuvurugana kwa kukosa maono baada ya kukamilisha lengo la kukitoa chama tawala. Je, unataka kuniambia kuwa CCM ikitoka madarakani nayo ikiwa chama cha upinzani kijiunge na kutengeneza umoja na wapinzani dhidi ya chama tawala kipya?

Ikumbukwe kuwa, tatizo la nchi yetu si CCM pekee. Tunahitaji kwanza kujibu maswali magumu kuhusu falsafa na itikadi (hili ndilo chimbuko la maono ya nchi) inayotakiwa kuongoza nchi yetu; maridhiano juu ya maadili ya taifa ambayo yataweka sifa, vigezo,wajibu na matarajio ya watu juu ya viongozi na viongozi juu ya wananchi na mwisho kabisa kupata viongozi watakaobanwa na misingi hiyo. Vinginevyo, hata wapinzani waungane vipi hakuna jipya tutakalofanikiwa nalo.

Wananchi wetu wanahitaji maendeleo na ahueni ya maisha ili waweze kutimiza ndoto zao kwa kutumia vipaji na uwezo wao walionao. Wananchi wetu wakipewa fursa hiyo wanayo majibu ya maswali magumu ya kimaendeleo yanayotukabili. Majibu ya changamoto zetu za maendeleo hayako nje ya nchi ambako tunahangaika sana kuyatafuta. Tunahitaji utawala unaotambua na kuyashughulikia haya iwe CCM au upinzani.

Aliyoyanena Mwanakijiji ni maono. Ni imani yangu kuwa Mwanakijiji hakutoa maono yake dhidi ya CCM tu kama chama ila kwa kuwa CCM ndio chama chenye dhamana ya dola. Ni imani yangu CHADEMA ingekuwa madarakani na kuenenda kama ilivyo CCM sasa, Mwanakijiji angeandika maono yake "Kuanguka kwa CHADEMA unabiii unatimia". Ndivyo navyomuona Mwanakijiji na naheshimu sana misimamo yake.

Mwalimu Mkumbo, nitafurahi kupata majibu.
 
Sheria ilikuwa inazuia muungano technically maana inabidi msajili chama upya na taratibu zote zinaanza upya. Lakini nasikia msajili wa vyama "ameshinikiza" mabadiliko ya sheria ili vyama viruhusiwe kuungana bila kulazimika kusajili hicho chama upya. Alituaidi katika mkutano wa CHADEMA wa Septemba pale PTA kuwa mswada utakuwa tayari na utapelekwa katika bunge la mwezi wa pili.

Nafikiri sisi wapinzani hatujatia pressure ya kutosha kubadilisha hii sheria.

Kitila,
Avatar yako imenifurahisha, nakumbuka Mwenge Sec, School. Thanks for your confidence and unshakable standpoint
 
Back
Top Bottom