Kuanguka kwa CCM - Unabii Utatimia!

Kuanguka kwa CCM - Unabii Utatimia!

Tatizo sio CCM. Tatizo ni kushindwa kwetu kuiwajibisha.

CCM kuondoka sio suluhisho kwani kitakuja chama tawala kingine na kuvurunda kama CCM.

Suluhisho tujifunze kuwajibisha chama na serikali.

Nasisitiza: TATIZO SIO CCM

You are kidding!
ofcourse am sure you know for real TATIZO NI CCM
 
Tatizo sio CCM. Tatizo ni kushindwa kwetu kuiwajibisha.

CCM kuondoka sio suluhisho kwani kitakuja chama tawala kingine na kuvurunda kama CCM.

Suluhisho tujifunze kuwajibisha chama na serikali.

Nasisitiza: TATIZO SIO CCM


Tatizo ni CCM.......Na sasa hata wale mliowaona wamelala kule Malampaka na Namtumbo wameanza kuona na kujua Ukweli!!Ipo siku isiyokuwa na jina na wala haipo mbali CCM itaanguka anguko la kutoamka!!
 
Lisemwalo lipo....................ila na sisi tubalikeeeeeee tunapigwa mabomu bado tunawakumbatia,tunalazwa kwenye madarasa wakati tuna kwetu BADO hatuoniiii???????? JAMANI mpaka wachukue wake zetu ndo tutareact????? migao ya umeme kwa ujanja wa watu fulani.....TULIANZA NA ARI,NGUVU,KASI MPYA IKASHINDIKANA TUKARIBU MAISHA BORA KWA KILA MTZ,NAYO BILABILA SASA KILIMO KWANZA.duh haah haaa haaaaaa WADANGANYIKA TUNASONGA.😕😕
 
Tumuombe Mheshimiwa Rais asigombee Urais Mwaka ujao wa 2010. Pia tubadilishe katiba ya nchi yetu na kuwa na utaratibu kuwa kuanzia mwaka 2010 mtu atakuwa Rais wa Tanzania kwa kipindi kimoja tu cha miaka mitano tu. Pia itabidi tuweke sheria kuwa kila mwaka wakati wa kipindi cha BUNGE la BAJETI Wabunge wetu wataifanyia tathmini ya utendaji Serikali ya Rais aliyeko madarakani na kutoa uamuzi kama inapasa kuendelea kutuongoza kwa kipindi kingine cha mwaka mmoja au laa. Uamuzi huu BUNGE letu litaufanya kupitia njia ya kura ambapo utaratibu unaopendekezwa ni kwa hoja kuungwa mkono ya 2/3 ya Wabunge wa Chama tawala na 2/3 ya Wabunge wa Vyama vya Upinzani.

Naomba kuwasilisha na siku njema kwenu wote.
 
Jamani eeeh, naomba kuelimishwa kidigo. Kuna nchi nyingine mbali na Tanzania ambayo Chama Chake kimetawala tangu uhuru wao? Naamini ni chache sana- kama zipo. Kwa maana hii, kuanguka kwa SI SI EM ni dhahiri!
 
CCM will definitely go one day! But i dont believe that day is soon! Sababu:

1. Kuna sehemu nyingi sana nchini hawajui anything beyond CCM.

2. Watu wengi wamewekeza ndani ya CCM, na hao watu wahatapenda kuona investment yao inaisha. Hawa ndo mafisadi. Msidhani mafisadi ni watu wanaoiba pesa za umma tu, bali hata wafanyabiashara wakubwa waliowekeza CCM wanaopata dili ndogo ndogo ambazo hatujazi-shtukia. Hivyo kuiondoa CCM, sio vita against chama tu, bali ni vita against an elite group of mafisadi ready to pump money and everything else in order to keep CCM in power.

3. Watanzania wengi hawajui maana ya maisha bora. They think in personal terms badala ya jamii na nchi kwa ujumla. Hii ndo sababu kuu watu wanapokea rushwa katika uchaguzi kwa kusudli wao binafsi kupata mlo. Sio kila mtu lazima awe tajiri, but we can all live a better life. Some of us were never meant to be wealthy, but have enough to live our lives. Bongo kila mtu anataka kuwa millionaire. Wapi na wapi jamani?!
 
Mambo si rahisi kihivyo. Itachukua miaka mingine 20 CCM kushindwa katika nchi hii. Nadhani, wale wenye maono na kuionea huruma nchi hii, wajitahidi kugombea ubunge ili upinzani angalau wawe karibu na 50% ya wabunge wote ili waweze kudictate miswada ya kupitishwa kwa maslahi ya nchi. Hata kwenye demokrasia komavu zenye uchumi komavu imechukua miaka mingi chama cha upinzani kuchukua madaraka. Zanzibar yawezekana upinzani kuchukua lakini si Tanzania. Na hali hii inabidi hata watawala wa sasa wajue ili yakitokea Zanzibar wasitume jeshi kwenda kuzima kama vile mapinduzi yametokea.
 
Marehemu Karume alikuwa anajigamba kuwa hakutakuwepo uchaguzi Zanzibar kwa miaka hamsini. Miaka sita baadaye alikuwa dead. CCM kama any other empire in history will see its demise in our lifetime. You can quote me on that.
 
Mwanakijiji uliyosema au unachotabiria ni kweli. Kwa wale wenye kumbukumbu nzuri walejee kwa kile kilichotekea SOVIET UNION na chama chao cha kikomunist. Ilikuwa asubuhi na mapema watu walipoamka Boris Yelsini alitangaza kuvunjika kwa dola la KISOVIET. Mali zote za chama zikawa za serikali. Magazeti kama PRAVDA na Komsoskaya yakaambiwa wachukue mitambo yao waondoke kwenye majengo ya umma na wala si ya chama. Majengo yote yaliyokuwa yanatumiwa na chama Yelsin Borisi akayatia makufuli. Wat hawakuamini kilichotokea. Huo ndiyo ukawa mwisho wa Chama tawala katika dola kubwa duniani. Kwa wale wenye kumbukumbu zaidi waziweke hapa ili akina KINGUNGE na wenzake wasome alama za nyakati. Nawasilisha hoja MKUU.
 
Wapinzani mteueni Dr. Slaa kama Mgombea Urais wenu na Mumtangaze Rasmi Kabla ya Januari 2010. Na Maalim Seif Awe Mgombea Mwenza. Pia Tangazeni Kuwa Profesa Ibrahim Nguyuru Haruna Lipumba atakuwa Waziri mkuu akisaidiwa na Zitto Kabwe kama Naibu Waziri Mkuu. Mrema Mpeni Tena Mambo ya Ndani. Kiongozi wa Upinzani Bungeni kwa sasa awe Waziri wa Fedha na Uchumi. Dr Adolf Faustin Kazimoto Mkenda (Nishati na Madini akiwa kama Mbunge wa Kuteuliwa). Na kuanzia Januari Moja 2010 muwe na saa tatu kila siku kwenye Radio zote na TV zote hapa nchini mkiwasiliana na Watanzania wote moja kwa moja. Kazi kwenu na Jumamosi Njema
 
Hongera mwanakijiji,Kitila na wengine,Dawa ya CCM ni kuungana vyama vya upinzani na kuiondoa CCM madarakani,naomba wana jamii wote tuwe wa kwanza kutia sahihi barua itayoandaliwa na washika dau wakiongozwa na Docebit Kitila kwenda kwa vyama vya upinzani kuwaambia kuwa Watanzania tuntaka chama kimoja cha upinzani chenye nguvu.Tofauti zilizojitokeza Tarime,Busanda na kwa Kabuye zizikwe na vyama viungane kuwang'oa hawa mafisadi madarakani.au walio katika vita ya ufisadi ndani ya chama tawala wajiondoe waanzishe chama kingine kwani utabiri mwingine utakuwa umetimia kuwa wapinzani bora watatoka CCM.Maana tunaona dalili zote za kusambaratika za CCM.
Wainzani ungana pamoja ondoa ccm madarakani.
 
Mimi siwaamini tu ....... hivi ukilichoma moto chaka walilojificha nyoka wa sumu kali, halafu akatoka simba kuukimbia huo moto kuelekea ulipo, je utampokea ? bila shaka jibu ni hapana. basi wote ni wabaya tu kama waliweza kuishi pamoja bila mkwaruzano mpaka ulipotoea moto ndipo waanze kukimbiana hiyo haibali ubaya wao. na waungue wote pamoja period
 
Ni kweli. Nilikaa kwenye mazungumzo ya faragha watu wachache na kiongozi mmoja mkuu wa ki-taifa (PM) wa zamani. Alitoa maoni mengi na moja ni kuwa JMK pamoja na kuwa na nia nzuri na nchi lakini nchi inamshinda na itaendelea kumshinda kutokana na uswahiba wake na wajanja wachache (na akawataja majina watu kama sita hivi). Ajabu ni kuwa mwezi mmoja baadaye huyu huyu bwana akiwa kwenye NEC Butiama, hakusema lo lote la kumsaidia JMK na nchi zaidi ya kusema kuwa kuna haja ya CCM kuwa na mshikamano na mtazamo mmoja. Go figure!

Unafiki na urafi ndio utawamaliza yetu macho

***********
amani yetu inatumiwa vibaya
 
Hivi CCM ifanye nini ili mjue imeshaanguka? Tanzania hatuna chama tawala. ni makundi tu ya kila mtu na iwake ndo yanatawala hapa. hakuna chama tawala....wengi mnafikiri ili CCM ianguke ni mpaka waondoke madarakani kisheria. hawawezi kuondoka madarakani kwasababu hakuna viongozi wala chama mbadala wa kukabidhiwa hiyo mikoba...JK na wenzake waondoke sasa hivi, wakiache chama gani madarakani? Hakuna.
 
CCM imeshakuwa ngoma iliyovuma lazima ipasuke tu, aina tiba tene. Maana watanganyika wameshaamka, wameshapata ujasiri wa kusema. Kinachohitajika hapa sasa hivi ni mbadala wa CCM make wapo wengi ndani ya CCM ambao kazi na shughuli zao zote zinategemea CCM na serikali yake hivyo wanaogopa kutoka kulinda chakula cha watoto. Hivyo watakapo ona kuna Chama makini ambacha kinaweza kuwahakikishia shughuli zao wataondoka tu CCM. Upinzani muhimu ujengwa na nguvu ya kiuchumi ya chama!!
 
Anguko la CCM ni kubwa! Anguko hili linaashiria mwisho wa zama za kidhalimu za utawala wa chama hiki kinachojiita cha 'mapinduzi' kumbe ni cha 'maangamizi' ya Watanzania. Chini ya CCM Watanzania walio wengi wamekuwa wakiishi kwa mashaka makubwa, hata wasijue watakula nini next. Kwa upande mwingine ni chama kilichotengeneza tabaka la matajiri kupindukia - utajiri walioupata kwa kupora raslimali za nchi huku wakiwapumbaza wananchi kwa ngojera za 'amani na utulivu' ili waendelee kuwakandamiza zaidi. Kwa kuwa Mungu anawapenda watu wake anatuletea ukombozi kwa kukiangamiza chama hiki cha majambazi kwa kuwatumia madomokaya kama akina Sofia Simba na Kingunge kukamilisha maangamizi hayo na kuwafunulia watu wake nuru mpya. Mungu amelihurumia taifa lake alilolipa upendeleo wa pekee kwa kujaza raslimali lukuki ambazo zimeporwa bila huruma na maharamia (tena wengine kutoka nchi za mbali kama Uajemi). Naamini Mungu atawaongoza watu wake na kubadilisha fikra duni zilizojengeka kwenye akili zao za kuwasujudia watawala dhalimu na kuchukua hatua zinazostahili. Lazima tufahamu kwamba hatuna nchi nyingine ya kukimbilia kama ilivyo kwa wenzetu akina Rostam. Hivyo tunapaswa kuamka sasa na kuipigania nchi yetu. Mungu ibariki Tanzania!
 
Back
Top Bottom