CCM imepata mtelezo.Ikitaka kupitisha jambo lolote bungeni bila vikwazo vya upinzani inamuambia Tulia aongoze bunge.
CCM sasa inaweza kuamua lini wapinzani wawepo bungeni na lini wasiwepo kwa kutumia msimamo wa UKAWA dhidi ya Tulia.
Haya ni matokeo ya maamuzi ya hasira ya Mbowe. Yatagharimu UKAWA na nchi pia wakati mwingine.
Kuna makosa makuu matatu wanaUKAWA (wale wanaofikiri) tunayajutia sana.Kosa la kwanza ni kukubali Lowassa awe mgombea wetu wa urais.Kosa la pili ni kugomea uchaguzi wa Zanzibar.Na kosa la tatu ni hili la kumgomea Tulia.TUNGOJE.
No, si kweli mkuu na sikubaliani na wewe kwa 100%!
CCM ina wabunge zaidi ya 250 na UKAWA/UPINZANI ni si zaidi 120!!
Kwa tofauti hiyo ya idadi hata kama hawa wangekuwa wanahudhuria kila kikao wakati wote na CCM wakataka kupitisha jambo lolote wangeshindwaje?
Ninakubaliana na wewe ktk moja tu, kuwa sasa wanaweza kupitisha chochote pasipo upinzani mkubwa.
Hata hivyo, hii hata haina maana yoyote kwa sbb kama jambo lililopitishwa ni baya basi litabaki kuwa baya tu na litawaathiri wananchi wote na kama ni kupingwa basi litapingwa tu huku nje!!
Rejea bunge la katiba. Pamoja na kuachiwa na kuipitisha "katiba pendekezwa" kwa mbwembwe za kila dizaini, iko wapi? Je, haikugeuka kuwa kitanzi cha kwao wenyewe? Samwel Sitta yuko wapi?
Uliona ugumu wa uchaguzi wa mwaka jana?
Hii watacheka kwa muda na kudhani wamewaweza, lakini ukweli ni kuwa hiki ni kitanzi chao cha hapo badae...waingereza wanasema ita back fire!
Ni vyema sana mkashindana kwa hoja humo humo na mkawashinda kuliko kujengewa dhana ya kutoaminiwa na upande mmoja kwa sbb za upendeleo, ukiukaji wa taratibu na ubabe tu usio na kichwa wala miguu!!
Una habari kuwa ujinga huu tayari unafungamanishwa na Rais Magufuli na serikali kwa ujumla? Unajua madhara yake? Utazuia watu kutoamini haya?
Mkubwa siasa haziko bungeni tu. Uwanja wa siasa na harakati za kisiasa zina eneo pana sana. Tena huku nje ndiko siasa hasa zinakofanyika!!
Unakumbuka sakata la Buzwagi mwaka 2006/7 dhidi ya Zitto KABWE? Wakamwadhibu Zitto Kabwe kutohudhuria vikao kadhaa, wakachekelea sana na kudhani wamemuua kisiasa yeye binafsi na CHADEMA ili kuficha uchafu wa CCM na serikali yao chini ya zulia!
Matokeo yake unayakumbuka? Ili back fire kwa CCM na kuiporomosha serikali kwa kishindo kikuu na leo Zitto huyo politically stronger than ever hata akienda kugombea jimboni Chato kesho na Magufuli, anachaguliwa tu!!
Na unafuatilia lakini jinsi huyu mama anavyopondwa na kuitwa majina ya kila aina kwa sbb ya hiki anachokifanya anapokuwa amekalia kiti cha spika?
Trust me. Hata wale wenye akili walioko humo humo CCM na serikalini, wanaoona mbali, hawaungi mkono ujinga huu unaofanywa na huyu mama aliyepachikwa hapo!!