Resilience
JF-Expert Member
- Jan 4, 2023
- 897
- 4,187
Nimeona viongozi wa vilabu vya mpira ndio wanahangaika na watu wanaotengeneza jezi feki. Najiuliza ni halali kisheria mtu kutengeneza jezi feki Tanzania?
Mbona kwenye bidhaa nyingine watu huchukuliwa hatua kali za kisheria? Au wanaotengeneza ndio vigogo wenye nchi? Tukiendelea hivi haiwezekani hawa viongozi wa vilabu wakashambuliwa na wananchi au wana mtandao wa biashara hizi zisizolipa hata kodi?
TRA na Polisi mpo wapi kwenye hujuma hizi za kiuchumi?
Pia soma: Kontena zaidi ya 2 ya Jezi feki zinazokadiriwa kuwa na thamani ya zaidi ya Tsh. Bilioni 2 zakamatwa