Kodi ya Maendeleo(kichwa), Uzembe na Uzururaji...

Kizazi cha vijana cha leo ni tofauti na cha miaka ya 1980 kutudi nyuma hadi 1961

Uwezo wa kufikiri wa vijana wakileo ni mdogo tena nimdogo kiasi cha kuhatarisha usalama wa nchi yetu!

Kuna njia nyingi za kurejesha ushupavu, uzalendo, na uwezo kifikra wa vijana wa leo na kesho, mfano kuboresha mfumo wa elimu yetu, kurejesha mafunzo ya mgambo yawe ni lazima kwa kila kijana, kuweka utaratibu wa kuitisha mikutano ya vijana kila mwaka kwa kila mkoa na wilaya,

Lakini yote hayo yanaweza kuwa msaada mbalada tu, mimi napendekeza KODI ya kichwa irejeshwe,

Iwekwe katika makundi, vijana waishio mjini watozwe kodi stahiki kama ni 10000 (elfu kumi)

Wale wa vijijini walipe nusu 5000 (elfu tano)

Hili litasaidia kuwafanya vijana kujituma/kuchakarika/kupigana kusaka pesa!

Licha ya kusaka pesa, vijana watakuwa na uchungu na nchi yao hasa wakisikia kuwa KODI yao inaibwa na kufichwa USWISI na kikundi kidogo mufilisi kilichopewa dhamani ya kuwaongoza!

Napendekeza Kodi ya kichwa irejeshweeee!

Yericho
Kimsingi serikali imeondoa direct tax kwa ajiri ya kuzima nguvu ya wananchi kuihoji juu ya matumizi na utendaji wake, ndio maana leo watu wachache sana tunalazimika kuilalamikia serikali na kuipush kutueleza kwa nini tunaendelea kuwa masikini wakati tuna rasilimali nyingi mwisho wa siku kwa sababu wengi wengi hatujawahi kuona dhahabu,almasi, wala kutembea mbuga za wanyama na hatujui thamani yake sokoni ni kiasi gani ukizingatia vitu hivyo haviko karibu hata kidogo na maisha yetu ya kila siku, baada ya muda mfupi tunasahau na tunakuwa wepesi sana kubadirishiwa sinema.

kama tutalipa kodi ya kichwa (kwa jina lolote lile) swali litakuwa where is our money going?? pasingetosha hapa
 
asante Mtemiwao, hapa tanzania kila mmoja analipa hiyo kodi sawa wafanyakazi wanalipa zaidi, ebu fikria kati ya mkulima anayetumia sukari na mwanafunzi anayenunua pen ni kiasi gani analipa, watu wa kuangalia ni wafanya biashara daima siamini kama wanalipa kodi kama mtumiaji wa mwisho ndo analipa kila kitu. hivyo kodi ya kichwa ipo na itaendelea lililobadirishwa ni jina tu.

hakuna mtu anajua kwamba analipa hizi kodi (vat), tunataka kodi ambayo mtu anaona kabisa imeondolewa kwenye kipato chake.
 
Mkuu kabla ya Serikali kurudisha kodi ya kichwa itupe kwanza taarifa ya MAPATO NA MATUMIZI ya kodi zote zinazokusanywa na Serikali ikiwa ni pamoja na mapato ya vitega uchumi vya nchi hii(bandari/madini/mbuga za wanyama/milima/na vingine vya kufanana na hivyo tofauti na hapo tutakuwa tunatoana tu nduki kama ilivyokuwa zamani.

inafanya hivyo lakini who cares kwamba haiko efficient au tunaibiwa, hauoni kuna watu wameanza kusema mambo ya dr slaa kuhoji mambo ya ufisadi ni old song. watu wachache sana wanaoona jinsi pesa inavyoondolewa mifukoni mwao na kwenda kwa mafisadi. hii kodi irudishwe alafu wewe mwenyewe utaona interests zako kwenye efficient government zatakavyoongezeka.
 
Ili kukabiliana na aibu ya rais wetu kuzunguka kwenye mataifa za watesi wetu kuomba omba na pia kuiwezesha serikali yetu kukusanya mapato ya kutosha kwa ajili ya shughuli za maendeleo ni kwanini serikali isirudishe kodi ya kichwa kwa kila mwananchi kuanzia at least miaka 25?

Haya imeanzishwa kukupitia simu za mikononi.

Kila mwezi utakuwa unakatwa Sh. 1,000 kwenye simu yako kama kodi

Sidhani kama utalalamika.
 
Haya imeanzishwa kukupitia simu za mikononi.

Kila mwezi utakuwa unakatwa Sh. 1,000 kwenye simu yako kama kodi

Sidhani kama utalalamika.

Sintolalamika, Lakini I wish wangeanzisha direct tax ambayo hakuna mtu atakwepa ili kuona wale wanaolala na kula bure alafu bado wanaishabikia serikali hii watakuwa na ujanja gani.

EMT
Serikali hii hata ikikusanya matrilion na matrillion ya mapesa haiwezi kuleta mabadiriko, inamapungufu makubwa sana na kuhusu mheshimiwa kuzunguka hovyo nalo hawezi kuacha kwa sababu sio kweli kwamba huwa anakwenda kutafuta pesa huko.
 
inafanya hivyo lakini who cares kwamba haiko efficient au tunaibiwa, hauoni kuna watu wameanza kusema mambo ya dr slaa kuhoji mambo ya ufisadi ni old song. watu wachache sana wanaoona jinsi pesa inavyoondolewa mifukoni mwao na kwenda kwa mafisadi. hii kodi irudishwe alafu wewe mwenyewe utaona interests zako kwenye efficient government zatakavyoongezeka.

Sipo mbali na wewe kimawazo mkuu,me nnatamani ingerudishwa hata leo tatizo lililopo ni wananchi wachache sana wanaojua kuwa kila wanaponunua bidhaa yoyote huwa wanakatwa na kodi papo hapo..Kodi ya kichwa ingerahisisha sana mabadiliko katika uongozi na kuwa na uchumi imara,sababu wananchi nao wangekuwa imara sana katika kuhoji na kutenda.Wapo wananchi wanaoamini kila wanaposikia mabilioni kadhaa yameibwa basi hawastuki na hudhani katika huo wizi hakuna fedha yao iliyoguswa.
 
Ili kukabiliana na aibu ya rais wetu kuzunguka kwenye mataifa za watesi wetu kuomba omba na pia kuiwezesha serikali yetu kukusanya mapato ya kutosha kwa ajili ya shughuli za maendeleo ni kwanini serikali isirudishe kodi ya kichwa kwa kila mwananchi kuanzia at least miaka 25?

Ningekuwa na muda ningejifunza kupigana na kusnaiip watu kama nyie niwapeleka sayari nyingine....wazo lako la kipuuzi sana nafikiri utakuwa na ubongo kama mawazo yako ya kipuuzi.....umenibo kupita kiasa na wazo lako bovu na chefuzi

Namsihi Mwenyezi Mungu anifanyie wepesi hasira initoke
 
Ningekuwa na muda ningejifunza kupigana na kusnaiip watu kama nyie niwapeleka sayari nyingine....wazo lako la kipuuzi sana nafikiri utakuwa na ubongo kama mawazo yako ya kipuuzi.....umenibo kupita kiasa na wazo lako bovu na chefuzi

Namsihi Mwenyezi Mungu anifanyie wepesi hasira initoke

Nini? hautaki kulipa kodi?
 
Nani anaikumbuka, kila mwenye kichwa akiwa mtu mzima alilipa kodi mbaya kabisa ya kichwa na wasioweza hasa maskini walikiona cha mtema kuni kucharazwa bakora, kulala jela na kufungwa.

Wazee wetu walikimbilia kusikojulikana muda wa msako wengine ni waathirika wa kodi hiyo maana umaskini uliongezeka zaidi.

Sasa kuna kodi ya simu, baada ya serikali kuona ya kuwa kila mtu mwenye akili timamu ana simu, kodi hii imerejeshwa huko, kila mtu analia, analalamika, ana machungu na hivyo kila raia hata mtoto mdogo ambaye mazingira yanamlazimu kuwa nayo simu hasa wagonjwa, vilema, walio katika hali ya dharura kuhitaji msaada wa mawasiliano ili wawasiliane na wenye kutoa msaada nk nao pia kodi hii wataitoa sasa pengine kushindwa

mwananchi mwenzangu unakubali kurudishwa kwa kodi ya kichwa kwa mlengo wa kodi ya simu? Karibuni uwanjani kutoa mapendekezo ya kufanya
 
Kwa hali halisi jinsi serekali yetu ilivyo muda si mrefu utasikia kila mwananchi anatakiwa kulipa kodi ya kichwa japo mimi hii kodi ya sim-card naiona kama kodi ya kichwa iliyokuja ki-siasa bila wao wenyewe kujua. Hii inatokana na viongozi wetu kutokuwa na uwezo mpana na kubuni vyanzo vya mapato wanaishia kuwakamua watu wa hali ya chini.
Haya bwana...! Lakini Mungu yupo tutaona.
 
Kwakweli hilo nmelisoma kwenye vitabu,lakini inakoelekea ni huko refer hawala ya fedha,Ngoswe penzi kitovu cha uzembe-halihitaji uwe mtabiri sana kama shekhe yahaya,wakati hayo yote yanatokea ndo kwaanzaaa wamiliki(makampuni) Migodi wanazidi kupata discount ya tax-Akili mgando za wapumbavu hapa dawa yake ni kuwaangusha kwenye box 2015 tu!!

Sent from my BlackBerry 9300 using JamiiForums
 
Kodi ya kichwa ilishaleje toka kitambo sema tu jina limebadilishwa lakini kimsingi tunalipa kodi kwa njia nyingi kubwa hasa kwa kununua bidhaa.
 
Fri, 05 Sep 1698
As part of a set of sweeping reforms designed to modernise his empire, Tsar Peter I of Russia implemented a tax on beards on this day in 1698.Peter had just returned from a grand tour of Western Europe in August, in which he was impressed by European customs he thought superior to Russian. Among them, European men were clean-shaven. Inspired by what he saw on this trip and influenced by advisors in Western Europe, Peter was determined to westernise his empire, starting with its customs and dress. During his welcoming reception back in Russia, Peter purportedly embraced the nobles who gathered to welcome him, then withdrew a giant pair of scissors and began cutting off their beards.That was the beginning of a social modernisation campaign in which courtiers, state officials, and the military were required to shave their beards and adopt modern clothing styles.Not everyone obeyed Peterâs command. Long, flowing beards embodied Orthodox ideals of manhood, integrity, and piety, and Russian men had worn beards with pride for centuries. Many even considered it a sin to shave their facial hair. Among those who refused to part with their beards were the Boyars, members of the old Russian aristocracy.At the same time that Peter was searching for a way to enforce his new rule, he was also desperately in need of money. Russia was fighting the Great Northern War with the Swedish Empire, which required unprecedented resources.Peter decided to impose a tax on beards, effectively enforcing his program for social modernisation as well as collecting state revenue in one strategic move.Excepting clergy and peasants, Russian men who wanted to keep their beards were required to pay a hefty tax of 100 rubles per year. Those who paid the tax were given a "beard token," which they were required to carry at all times. It was a copper or silver coin with a Russian Eagle on one side and the lower part of a face with nose, mouth, and beard, on the other. The token was inscribed with two phrases: "the tax has been taken" and "the beard is a superfluous burden."Other reforms followed Peterâs beard tax. He ordered nobles to wear Western-style clothing, put an end to arranged marriages, adopted the Julian calendar, and sent many Russians to be educated in the West.While many felt Peter brought Western, Enlightenment ideals to Russia, others felt he betrayed its traditions. The beard tax was eventually abolished in 1772.
 
Ninampango wa kutengeneza move ya tukio hili la kodi ya kichwa, lilikuwa lenye burudani kubwa, enzi hizo nakumbuka mwenyekiti wa kijiji alikuwa akituambia dawa ya kodi ya kichwa ni miguu yako, ukiwaona wanakuja kukukamata basi wewe ni kukimbia tu, ila ukishikwa utajuta, wanaweza kukuvizia usiku nyumbani kwako, basi ilikuwa ukiwa shambani ukawaona unaanza kukimbia, japo baadae walizuia kushika mtu akiwa shamba.

Vijana wa enzi hizi wanakosa mengi sana, ulikuwa ukimaliza darasa la 7 tu kazi kwako, mtu ulitamani usimalize shule. Yaani ilikuwa maisha ya kuwindana kama swala na simba.
 
ktk kodi nilizokuwa sizipendi ni kodi ya kichwa na kodi ya baiskeli,yaani walikuwa wakikukosa ktk kodi ya kichwa basi baiskel watakudaka tu.
siku moja mwenzangu alizama majini na kupiga mbizi baada ya mgambo kutaka kumdaka na uzuri mgambo wale walikuwa na maviatu mazito ikawawia ngumu kuingia majini
 
Back
Top Bottom