Kodi ya Maendeleo(kichwa), Uzembe na Uzururaji...

ktk kodi nilizokuwa sizipendi ni kodi ya kichwa na kodi ya baiskeli,yaani walikuwa wakikukosa ktk kodi ya kichwa basi baiskel watakudaka tu.
siku moja mwenzangu alizama majini na kupiga mbizi baada ya mgambo kutaka kumdaka na uzuri mgambo wale walikuwa na maviatu mazito ikawawia ngumu kuingia majini

mkuu umenikumbusha kodi ya baiskeli, jamaa walikuwa wakisimamisha baiskeli kwa kunyosha mkono juu kama trafiki anavyosimamisha gari, ole wako ukutwe hujabandika kale kanembo, viboko vitakuandama.
 
mkuu umenikumbusha miaka hiyo, Nakumba Dingi amewai kuchomoka usuku saa nane kuogopa kukamatwa.

Kulikuwa na mgambo mmoja wa kata yetu jina Saa Sita, huyo jamaa akikukamata utaimba Haleluya.
 
ktk kodi nilizokuwa sizipendi ni kodi ya kichwa na kodi ya baiskeli,yaani walikuwa wakikukosa ktk kodi ya kichwa basi baiskel watakudaka tu.
siku moja mwenzangu alizama majini na kupiga mbizi baada ya mgambo kutaka kumdaka na uzuri mgambo wale walikuwa na maviatu mazito ikawawia ngumu kuingia majini

^^
Ha ha tena zile baiskeli za swala, phoenix unakuta imebandikwa virisiti kila mahali, da! Niliwahi kuikataa barabara nikachanja mbuga za mashambani ! Usiombe wale jamaa walikuwa wanafanyia kazi sifa
^^
 
haaaa haaa mkuu umenukumbusha mbali sana nakumbuka nilikuwa kijijini kwa babu yangu alikuwa na baiskeli sasa akawa hajalipa kodi ya baiskeli nakwambia ukawa ni mwendo wa kuaki baiskeli ndani mpaka vuguvugu liishe,ile siku alipoitoa tu baiskeli kwenda nayo shamba wakamdaka wakachukua baiskeli wakaipeleka ofisi ya kijiji baada ya siku tatu ndio akaenda kulipia kodi.... ilikuwa hatari sana watu walikuwa wanalala mbele hatari
 
mshishangae sana kwani baada ya 30 years tutashangaa tena kwamba ilikuwaje tembo,twiga, dhahabu n.k zinasafirishwa nje ya nchi na watu wachache wanafaudu??? u know we africans are endowed with stupidity!! what changes is just time. YEAH I SAID IT!!
 
Utawala wa awamu ya pili na tatu kama sikosei,nadhani kodi ya kichwa ilisitishwa wakati wa jk.
 
nakumbuka nilipomaliza shule drs la saba nilishkwa kwajili ya kodi.walinichapa sna japo nilijitetea hawakunielewa.nakumbuka nilikuwa naenda kusaga na mama alikuwa mgonjwa nyumbni,pamoja nakujitetea kwangu hawakunielewa,zaidi zaidi walinipa kisago.nikapelekwa ofisi ya kata,nilimwomba mtendaji wakata,hakunielewa.mama aliposikia nimekamatwa alikuja kunitoa,alichoambulia ni matuc toka kwa mtendaji wakata.mama alirudi nyumban kuuza mbuzi ili anitoe.akauza mbuzi akalipa kodi angu na baiskeli.NIKIKUMBUKA ILE ADHA YA KODI YA KICHWA SINA HAMU ILITESA SNA WATU
 
mkuu umenikumbusha mbali sna yaani mwalimu angekuwepo muda huu nadhani mchakato wa katiba ungeshakua tayari
maana watu wangelabwa viboko
 
Amani na iwe kwenu wanajamvi!

Basi hata ilipotimia miaka mitatu baada ya vita vya Kagera,uchumi ulikuwa bado haujatengamaa! vijana wakawa wanakimbia vijiji vyao na kwenda mijini.Basi, mwalimu akaona namna ya kuwaondo mijini na kujenga uwajibikaji hasa miongoni mwa vijana, akatangaza bajeti chokonozi.kodi zikaongezeka maradufu na kodi iliyo kuwa maarufu enzi za mkoloni ikafufuliwa.iliitwa KODI YA KICHWA. Wakati ule ilikuwa ni shs 1500 kwa kichwa! yaani kila raia aliye timiza miaka 18 na ambae hayuko shule alitakiwa kulipa hiyo kodi.

Basi shs 1500 ya wakati ule ilikuwa ni kubwa sana na mbaya zaidi hata ukiwa na baiskeli ulitakiwa kuilipia kodi ya shs 500 kwa mwaka.Mijini ilikuwa ukikamatwa kwa koso lolote, kitu cha kwanza ungeulizwa umelipa kodi ya kichwa?Kama umelipa basi unaanza kuonekana kama raia mwema vile.mijini kulikuwa hakukaliki, vijijini hakukuwa na usumbufu sana, hivyo vijana wakitaka kuja mjini walitafakari mara mbili kabla ya kufanya uamuzi wowote.

Ikaja majira ya joto ya mwaka 1984, nasafiri kutoka shule kwenda likizo fupi ya mwezi Septemba, nikashuka kwenye gari nikajisogeza kwenye hoteli ya karibu nipate chai,Mara Mgambo kama watano wakanikamata, haya tuoneshe chiti chako kama umelipa kodi! nikawajibu sina.Kwa spidi ya umeme nikaingizwa kwenye gari lao,wakasema, twende wahujumu wa Nchi nyie.

Njiani nikawa nawasikia vijana wanasikitika, mmoja akasema aah tena nilikuwa sitaki kuja mjini mie, sasa ona nitaenda limishwa vibarua mie mpaka nipate kodi yao.Hawkuwa na namna ilibidi kodi ilipwe.

Mkubwa wa wale mgambo akanisogelea na kuniuliza, na wewe ni nani? nikamwambia jina langu na kwamba mimi ni mwanafunzi nasoma kidato cha tatu Malangali sekondari.Akamwita mkusanyaji kodi aniulize maswali kwa kiingereza ili athibitishe kama kweli ninasoma.Kumbe wamejiroga,Nikamwambia before you ask me anything let me tell you my history in brief! niliongea kwa tornation ya kimarekani kabisa, basi yule mkubwa wao akasema kumbe kweli anasoma, mpeni begi lake aende.
Hali ile ingeendelea na kiwango cha kodi ya kichwa ikaongezwa, unafikiri kuna mtu angecheza pool asubuhi? unadhani watu wanekimbilia kuja mijini bila kujipanga? Karibu tena kodi ya kichwa!!!
 
Amani na iwe kwenu wanajamvi!

Basi hata ilipotimia miaka mitatu baada ya vita vya Kagera,uchumi ulikuwa bado haujatengamaa! vijana wakawa wanakimbia vijiji vyao na kwenda mijini.Basi, mwalimu akaona namna ya kuwaondo mijini na kujenga uwajibikaji hasa miongoni mwa vijana, akatangaza bajeti chokonozi.kodi zikaongezeka maradufu na kodi iliyo kuwa maarufu enzi za mkoloni ikafufuliwa.iliitwa KODI YA KICHWA. Wakati ule ilikuwa ni shs 1500 kwa kichwa! yaani kila raia aliye timiza miaka 18 na ambae hayuko shule alitakiwa kulipa hiyo kodi.

Basi shs 1500 ya wakati ule ilikuwa ni kubwa sana na mbaya zaidi hata ukiwa na baiskeli ulitakiwa kuilipia kodi ya shs 500 kwa mwaka.Mijini ilikuwa ukikamatwa kwa koso lolote, kitu cha kwanza ungeulizwa umelipa kodi ya kichwa?Kama umelipa basi unaanza kuonekana kama raia mwema vile.mijini kulikuwa hakukaliki, vijijini hakukuwa na usumbufu sana, hivyo vijana wakitaka kuja mjini walitafakari mara mbili kabla ya kufanya uamuzi wowote.

Ikaja majira ya joto ya mwaka 1984, nasafiri kutoka shule kwenda likizo fupi ya mwezi Septemba, nikashuka kwenye gari nikajisogeza kwenye hoteli ya karibu nipate chai,Mara Mgambo kama watano wakanikamata, haya tuoneshe chiti chako kama umelipa kodi! nikawajibu sina.Kwa spidi ya umeme nikaingizwa kwenye gari lao,wakasema, twende wahujumu wa Nchi nyie.

Njiani nikawa nawasikia vijana wanasikitika, mmoja akasema aah tena nilikuwa sitaki kuja mjini mie, sasa ona nitaenda limishwa vibarua mie mpaka nipate kodi yao.Hawkuwa na namna ilibidi kodi ilipwe.

Mkubwa wa wale mgambo akanisogelea na kuniuliza, na wewe ni nani? nikamwambia jina langu na kwamba mimi ni mwanafunzi nasoma kidato cha tatu Malangali sekondari.Akamwita mkusanyaji kodi aniulize maswali kwa kiingereza ili athibitishe kama kweli ninasoma.Kumbe wamejiroga,Nikamwambia before you ask me anything let me tell you my history in brief! niliongea kwa tornation ya kimarekani kabisa, basi yule mkubwa wao akasema kumbe kweli anasoma, mpeni begi lake aende.
Hali ile ingeendelea na kiwango cha kodi ya kichwa ikaongezwa, unafikiri kuna mtu angecheza pool asubuhi? unadhani watu wanekimbilia kuja mijini bila kujipanga? Karibu tena kodi ya kichwa!!!
Hahaha!! Ulimwaga yai lugha ya malkia
 
Hahaha!! Ulimwaga yai lugha ya malkia
Yap, nilitaka wajue kuwa mimi nasoma kiukweli na sibahatishi.ingawa nilikuwa sina kitambulisho wakaniachia. ila kodi ya kichwa ilikuwa mtihani kweli yaani ilibidi watu wafanye kazi kwa bidii ili walipe kodi zote ndio wawe huru.Kama hujalipa kodi ilikuwa siyo rahisi kutoka sehemu moja kwenda nyingine usiulizwe cheti cha kodi.
 
Kuna mahusiano gani kati ya 'uzembe na uzurulaji na 'kodi ya kichwa?
Vijana wa siku hizi shida tupu yaani kila kitu utafuniwe tu? huwezi kujiongeza? maana ni kwamba kama wewe hujalipa kodi ilikuwa siyo rahisi kutembea mjini usikamatwe na kuulizwa, umelipa kodi? kwahiyo vijana walilazimika kufanyakazi ili walipe kodi na wawe huru.yaani uliufurahia uhuru baada ya kuwa umelipa kodi.
 
Back
Top Bottom