Umewahi kulipa kodi ya kichwa (Kodi ya maendeleo) na unakumbuka nini?

Bombabomba

JF-Expert Member
Dec 23, 2017
1,725
2,008
Nikiwa Mwanafunzi wa SM miaka ya 80s nilianza kupata adha ya kodi hii kwa kushuhudia watu wazima wakibaki ndani ya nyumba siku nzima kujificha. Msimu wa maembe mwezi Desemba walikuwa wakishinda mashambani/mafichoni wakila maembe siku nzima. Nilijiuliza kwa nini wakamatwe?

Nilivyomaliza form VI nilitumia kitambulisho changu miaka 3 mbele kujiokoa dhidi ya ulipaji kodi lakini Juni 30, 2001 mgambo walinivizia home saa 9 usiku nikijipanga kutorokea vijijini kukusanya mazao nikakamatwa. Nikalazimika kulipa kodi na adhabu pia na kipande cha baiskeli na kuishiwa mtaji.

Julai Rais Mkapa aliifuta kodi hii sumbufu. Kulikuwa na Migambo wababe sana kizazi kile. Kiukweli sitasahau adha hii maishani mwangu.

Karibuni wahenga tujikumbushe Maisha yale ya kukamatwa na Migambo kwa kushindwa lipa kodi.
 
Lol..hayo mambo kumbe yalikuwepo? Naanza LA kwanza 98! by that time bi mdash yuko ministry of works..kumbe watu mnakimbizwa porini huko..tah..maisha haya! Najionaga muheengaaa! Hiyo kodi ilikua bei gani?
 
Mie nakumbuka African Pub maeneo ya magomeni kota, nilikuwa nakutana sana pale na mzee mrisho na mzee mzuzuri,
 
Lol..hayo mambo kumbe yalikuwepo? Naanza LA kwanza 98! by that time bi mdash yuko ministry of works..kumbe watu mnakimbizwa porini huko..tah..maisha haya! Najionaga muheengaaa! Hiyo kodi ilikua bei gani?
Wakati huo naokumbuka mimi, ilikuwa Tshs 4,000. Halafu kulikuwa na vilisti flani vya kulipia baiskeli. Watu walikuwa wanakimbia baiskeli zao balaa.
 
Hio kitu ilinitesa saaana nlishapigana saaana na migambo wa huko bush kwetu
Nlimpa bigup mh mkapa kuiondoa
Na hio sera yakuifuta kodi ya kichwa ndio ilimpa kura kwa asilimia kubwa saana wakat wa kampen yake
 
Madogo wanadhani hii nchi ilikuwaga ni sehemu ya pepo!pamepitwa!!!sema Che Nkapa aliona isiwe ishu akaja na VAT hii huchomoi.
 
Nikiwa Mwanafunzi wa SM miaka ya 80s nilianza kupata adha ya kodi hii kwa kushuhudia watu wazima wakibaki ndani ya nyumba siku nzima kujificha. Msimu wa maembe mwezi Desemba walikuwa wakishinda mashambani/mafichoni wakila maembe siku nzima. Nilijiuliza kwa nini wakamatwe?

Nilivyomaliza form VI nilitumia kitambulisho changu miaka 3 mbele kujiokoa dhidi ya ulipaji kodi lakini Juni 30, 2001 mgambo walinivizia home saa 9 usiku nikijipanga kutorokea vijijini kukusanya mazao nikakamatwa. Nikalazimika kulipa kodi na adhabu pia na kipande cha baiskeli na kuishiwa mtaji.

Julai Rais Mkapa aliifuta kodi hii sumbufu. Kulikuwa na Migambo wababe sana kizazi kile. Kiukweli sitasahau adha hii maishani mwangu.

Karibuni wahenga tujikumbushe Maisha yale ya kukamatwa na Migambo kwa kushindwa lipa kodi.

Ndugu leo umenikumbusha matukio ya muda sana, kifupi mimi sikuwah kulipa hii kodi kwa sababu ya umri wangu,lakini nilishuhudia vibweka na vimbwanga vingi vya hii kodi na ile kodi ya baiskeli ya kila mwaka.
Na ilifikia mahali huko nilikokuwa naishi kulikuwa na Muembe Dodo, huu mwembe ulipachikwa jina la "Mwembe Kodi", wale migambo walikaa hapo kusubiria watu wanaotoka mashambani, na hiyo njia ni common lazima upite, like Chalinze vile kama unaenda Moro, sasa kuanzia mida ya saa 6 mchana kwenda mbele utawakuta jamaa wamekaa pale wanasubiri watu wanaotoka shamba wawadai kodi au wawakamate kwa kutolipa kodi.

Ila pia nilishuhudia watu wakikamatwa hasa vijana wa kiume na walikuwa wakiishi kwa taharuki sana msimu wa utafutaji wa wakwepa kodi. Mimi binafsi japo nilikuwa sijafikia umri wa kulipa kodi ila mgambo aliwah kunikamata kwakua Baiskel yetu ya familia haikuwa imelipiwa kodi (Kwa wasiofaham basikeli nazo zilikuwa zinalipiwa kodi ya halmashaur kisha zinawekwa alama kuwa umelipa kodi mwaka husika), baada ya kukamatwa na mgambo akaichukua baiskeli akaipeleka polisi, mie sikwenda huko polisi nikaitelekeza kabisaaa, sasa kuna mama mmoja namfahamu ni polisi,nikaenda kumwambia juu ya tatizo la basikeli yetu, akaniambia niende kituoni nikaichukue, ila kabla sijaenda yule mgambo (ambaye alikuwa jirani yangu) aliileta ile baiskeli nyumbani.

Kodi ya kichwa ilikuwa ni unyanyasaji mkubwa na ilikuwa ya upendeleo, CCM members wengi hawakuwa wakilipa
 
Dah hiyo kodi ilikuwa nuksi sana + kulazimishwa kucheza mgambo home kulikuwa hakukaliki, ni mwendo wa maporini tu.
 
Back
Top Bottom