Kiwanda cha Tumbaki (TTPL) Morogoro Kufungwa?

Kiwanda cha Tumbaki (TTPL) Morogoro Kufungwa?

Kukwepa kodi ni namna monya wapo ya kufanya biashara,ni lazima ujue namna bora ya kuhakikisha unalipa kiwango cha chini kabisa cha kodi..Sio kila kodi inakwepeka,kuna kodi kama payrol taxes na withholding taxes nyingine ambazo hazikwepeki na hazina exemption.Kodi pekee abayo mwekezaji anweza kukwepa ni corporate income tax ambayo kwa Tanzania ni kubwa sana nafikiri ni 30% kwa maana nyingine kuondoka kwa wawekezaji hao kunamaanisha kwamba faida ni ndogo ndo maana inabidi waondoke maana wananona kabisa kwamba kwa viwango vyetu vya kodi na gharama za uendeshaji watakuwa wanatekenyana wenyewe tu.

Kwa ufupi ni kwamba badala ya kufikiria kukusanya kodi lazima serikali ikae na wawekezaji mezani,na kutafuta win win situation.Sio kuwapa STRESS kama mlivowapa Acacia alafu bado tukakosa.
 
Ni simanzi kwa wafanyakazi na wakulima wa tumbaku. Viwanda vya Ku process tumbaku ya inchi nzima Morogoro vinafungwa na wawekezaji waleee wanaondoka.

Ikumbukwe viwanda hivi vipo Morogoro mjini na vimekuwa vikikusanya tumbaku toka inchi nzima. Hawa jamaa wanaondoka na sababu inasemekana wanadaiwa deni kubwa la kodi na serikali na mambo mengine.

Kwa mnaokumbuka, mweshimiwa Rais aliwahi ongelea hili siku anamtumbua Kebwe kwamba moja ya mapungufu ameshindwa kutatua mgogoro unaohusisha kiwanda hiki.

Mfanyakazi mmoja kaniambia wameisha aga tayari. Anasema msimu wa tumbaku karibu wafanyakazi mia nne toka sehemu mbalimbali za Morogoro walikua wanaajiriwa kwa shifts. Hao wote wanaongezeka kwenye pool ya wasio na ajira.

Wakulima wa tumbaku wata suffer pia na chain nzima inayotegemea kilimo cha tumbaku.

Hivi serikali imeshindwa kutatua huu mgogoro kweli ?
hakuna haja ya kubabaika watakuja wawekezaji wengine acheni hao waende hatubembelezi mtu
 
Hatari
Hapo Kuna Alliance One Na Philip Morris
Yaani Vinafungwa Na Wanaondoka Hivi Hivi
Hata mimi nashangaa.......walipe kwanza ndo wasepe. Kuondoka bila kulipa deni ni kuhujumu nchi.
 
Yule Chief Negotiator wetu, Prof. Kabudi kashindwa kukaa nao tuingie nao ubia?!

Au wameamua waondoke kwanza ili tuviendeshe wenyewe hivyo viwanda.?!
 
Kwani mzee wa chemistry anasemaje juu ya multiplier effect ya kufungwa kiwanda?
 
RC Wa Morogoro Bado Yupo Ofisini
Yaani Win Win Situation Hajaifanyia Kazi
 
Yule Chief Negotiator wetu, Prof. Kabudi kashindwa kukaa nao tuingie nao ubia?!

Au wameamua waondoke kwanza ili tuviendeshe wenyewe hivyo viwanda.?!
Mi naomba niongee kimakonde serikali ingewa nyenga nyenga huku tunatafuta kampuni nyingine sasa wakiondoka na kama watu 400 watakosa kazi ni bomu sana na itaathiri sana kwa mkoa wa morogoro ukipiga hesabu 400 mara 3 da palefu sana sasa haya wakiondoka haya matumbaku tutavuta wenyewe kama tulivyokua tunaambiwa kuwa korosho ziuzwe kwenye ma ofisi humu nchini
 
Kama hawalipi kodi hakuna kuwalealea na waende tu..hao Alliance one walianza kama Dimon ni wakwepaji wa kodi wazuri sana na wanatumia vizuri ile sheria ya kodi ya miaka kumi..walianza kama Dimon walipoona miaka kumi ya kuoperate bila kodi imeisha wakasajili tena kampuni na kuiita Alliance one wakapata tena msamaha wa kodi kwa miaka kumi naona wamenogewa sasa hata baada ya muda wa msamaha wa kodi ya miaka kumi ilipoisha wameendelea kukwepa kodi..TTPL nao ndio walewale nchi haiwezi kuendeshwa kijanja janja namna hiyo kuna vitu vingine sio vya kumlaumu raisi kwa kusema sijui kabana..Hapana mwacheni afanye kazi japokuwa na yeye ana mapungufu yake mengi tu ila kwa upande wa pili wa shillingi anakula nao sahani moja wanaorudisha maendeleo nyuma

Kuna uthibitisho ni wakwepa kodi?
 
Hawa jamaa wanaondoka na sababu inasemekana wanadaiwa deni kubwa la kodi na serikali na mambo mengine.


Tunaambiwa usafiri wa anga ni aghali sana, lakini wao kila siku wanarusha ndege mara Tabora mara Dar
 
Ni simanzi kwa wafanyakazi na wakulima wa tumbaku. Viwanda vya Ku process tumbaku ya inchi nzima Morogoro vinafungwa na wawekezaji waleee wanaondoka.

Ikumbukwe viwanda hivi vipo Morogoro mjini na vimekuwa vikikusanya tumbaku toka inchi nzima. Hawa jamaa wanaondoka na sababu inasemekana wanadaiwa deni kubwa la kodi na serikali na mambo mengine.

Kwa mnaokumbuka, mweshimiwa Rais aliwahi ongelea hili siku anamtumbua Kebwe kwamba moja ya mapungufu ameshindwa kutatua mgogoro unaohusisha kiwanda hiki.

Mfanyakazi mmoja kaniambia wameisha aga tayari. Anasema msimu wa tumbaku karibu wafanyakazi mia nne toka sehemu mbalimbali za Morogoro walikua wanaajiriwa kwa shifts. Hao wote wanaongezeka kwenye pool ya wasio na ajira.

Wakulima wa tumbaku wata suffer pia na chain nzima inayotegemea kilimo cha tumbaku.

Hivi serikali imeshindwa kutatua huu mgogoro kweli ?
Kama issue ni kutolipa kodi waondoke tu! Na imekuwaje wakae siku zote hizo bila kulipa kodi?

Ingekuwa nchini kwao wasingelipa kodi?
 
Mi naomba niongee kimakonde serikali ingewa nyenga nyenga huku tunatafuta kampuni nyingine sasa wakiondoka na kama watu 400 watakosa kazi ni bomu sana na itaathiri sana kwa mkoa wa morogoro ukipiga hesabu 400 mara 3 da palefu sana sasa haya wakiondoka haya matumbaku tutavuta wenyewe kama tulivyokua tunaambiwa kuwa korosho ziuzwe kwenye ma ofisi humu nchini
Usiogope tutabanana humu humu, watawala wasipotengeneza tatizo watakuwa cha kuwaeleza kwenye kampeni.
Kampeni ijayo, mtaambiwa mchagueni x huyo, atanisaidia kufanya kazi. Na tumeshaongea na muwekezaji kwa ajilu ya kiwanda cha tumbaku, mtapata ajira na mtauza tumble kwa bei nzuri. Kisha mtashangilia na maisha yatakwenda.

Ndivyo nchi yetu ilivyo, usi panic, utajipa pressure.
 
Dah!una uhakika na unayoandika hapa mkuu.Hebu acha ushabiki
Kukwepa kodi ni namna monya wapo ya kufanya biashara,ni lazima ujue namna bora ya kuhakikisha unalipa kiwango cha chini kabisa cha kodi..Sio kila kodi inakwepeka,kuna kodi kama payrol taxes na withholding taxes nyingine ambazo hazikwepeki na hazina exemption.Kodi pekee abayo mwekezaji anweza kukwepa ni corporate income tax ambayo kwa Tanzania ni kubwa sana nafikiri ni 30% kwa maana nyingine kuondoka kwa wawekezaji hao kunamaanisha kwamba faida ni ndogo ndo maana inabidi waondoke maana wananona kabisa kwamba kwa viwango vyetu vya kodi na gharama za uendeshaji watakuwa wanatekenyana wenyewe tu.

Kwa ufupi ni kwamba badala ya kufikiria kukusanya kodi lazima serikali ikae na wawekezaji mezani,na kutafuta win win situation.Sio kuwapa STRESS kama mlivowapa Acacia alafu bado tukakosa.
 
Back
Top Bottom